settings icon
share icon
Swali

Je! Biblia inasema nini juu ya hali ya kutosali?

Jibu


Maombi ndiyo nguzo kwa maisha ya mkristo katika kutembea na Mungu. Sala inatuunganisha kwa Mungu, sala ni njia inayofaa ya kupenda na kuungana na wengine. Sala inafanya nafasi moyoni mwa anayesali kwa sauti ya Mungu ya kusahihisha. Biblia inasema "kuomba daima" (1 Wathesalonike 5:17), kwa hivyo chochote kingine isipokuwa mtazamo wa daima wa maombi na ushirika na Mungu ni dhambi. Kitu chochote kinachozuia uhusiano wetu na Mungu au kinachosababisha kujitegemea ni dhambi.

Tunaweza kuangalia vitendo vya Adamu na Hawa katika Mwanzo 3 kama aina ya hali ya kutosali. Walikula kutoka mti wa ujuzi wa mema na mabaya na wakawa na aibu kuzungumza na Bwana kama alivyokuja kukutana nao katika bustani. Wao walitengana na Mungu katika dhambi zao; mawasiliano yao na Yeye yameharibuwa. Hali ya kutosali ya Adamu na Hawa ilikuwa dhambi, na ilitokana na dhambi.

Je! Unaweza kufikiria mtu anayesema kuwa rafiki yako ilhali kamwe hajazungumza na wewe? Uhusiano wowote uliokuwa huko bila shaka unakuwa namatatizo. Vivyo hivyo, uhusiano na Mungu unatatizika bila mawasiliano. Haliya kutosali ni kinyume na kuwa na uhusiano mzuri na Mungu. Watu wa Mungu watakuwa na hamu ya asili ya kuwasiliana na Bwana wao. "Asubuhi, Bwana, unasikia sauti yangu; asubuhi naweka maombi yangu mbele yako na kusubiri kwa hamu "(Zaburi 5: 3). Amri za Biblia za kuomba zinaambatana na ahadi za ajabu: "Bwana yuko karibu na wote wanaomwomba, kwa wote wanaomwita kwa kweli" (Zaburi 145: 18).

Kristo ni mfano wetu bora wa hali ya maombi. Yeye mwenyewe alikuwa mtu wa sala (angalia Luka 3:21, 5:16, 9:18, 28; 11: 1), na aliwafundisha wafuasi wake kuomba (Luka 11: 2-4). Ikiwa Mwana wa Mtu aliona haja ya kibinafsi ya kuomba, tunapswa kuona haja Zaidi ya kuomba.

Hali ya kutoomba hupuuza karama ya maombezi ambayo Mungu ametupa. Tunaagizwa kuomba kwa ajili ya ndugu na dada zetu katika Kristo (Yakobo 5:16). Paulo mara nyingi aliomba maombi ya watu wa Mungu kwa niaba yake (Waefeso 6:19, Wakolosai 4: 3, 1 Wathesalonike 5:25), na alikuwa mwaminifu kuwaombea (Waefeso 1:16; Wakolosai 1: 9). Nabii Samweli aliona sala kwa ajili ya watu wa Israeli kama sehemu muhimu ya huduma yake: " Walakini mimi, hasha! Nisimtende Bwana dhambi kwa kuacha kuwaombea ninyi" (1 Samweli 12:23) ). Kulingana na Samweli, kutokuwa na maombi ni dhambi.

Kutosali ni kinyume cha amri ya Mungu ya kupenda wengine. Na sio tu kuombea kwa watu ambao ni rahisi kuombea. " Basi, kabla ya mambo yote, nataka dua, na sala, na maombezi, na shukrani, zifanyike kwa ajili ya watu wote." (1 Timotheo 2: 1). Yesu anatuambia kwamba tunapaswa pia kuombea wale wanaotutesa (Mathayo 5:44). Huu ni ujumbe wa Kristo, kumpenda na kuunga mkono kila mtu kwa sala, hata wale ambao ni vigumu kuwapenda.

Maombi hufanya nafasi kwa sauti ya urekebisho ya Mungu. Usio wa maombi unapunguza uwezo wetu wa kusikia Kristo wakati anatunongonezea maneno ya kurekebisha au kuhukumiwa kwa roho zetu. Waebrania 12: 2 inatukumbusha kwamba Kristo ni "mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu." Bila ya Roho Wake kuwa ndani ya mioyo yetu, tutatembea kwenye barabara mbaya ya kufuata hukumu yetu wenyewe. Tunapoomba mapenzi ya Mungu yafanyike "duniani kama ilivyo mbinguni" (Mathayo 6:10), mapenzi yetu wenyewe yaliyo kinyume hufunuliwa.

Mathayo 26:41 inatoa ushauri mwingine: "Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni; roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu." Usio wa maombi hugupika mioyo yetu na majaribu ambayo inatuzunguka na inaongoza kwa dhambi zaidi. Sisi huwa wenye hekima kwa njia za mioyo yetu kwa njia ya Mwangaza na mwongozo wa Roho. Na ni kwa nguvu ya Roho kwamba maombi yetu yanafaa (tazama Warumi 8: 26-27).

Maombi ni kiungo chetu na uhusiano na Mungu. Kristo alionyesha kinyume cha kutokuwa na maombi katika kutembea kwake duniani na kuweka mfano wa maisha yaliyojazwa na maombi.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je! Biblia inasema nini juu ya hali ya kutosali?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries