settings icon
share icon
Swali

Je, ni lazima nikiri dhambi yangu ya uzinzi kwa mke wangu?

Jibu


Ikiwa tunapaswa kukiri au la dhambi ya uzinzi kwa mpenzi weut wa ndoa na ni taharuki kwa Wakristo wengi ambao wamepata uzoefu wa mbaya wa kuanguka katika uzinzi. Kwa kawaida "wataalamu" wa kidunia huwahimiza wazinzi kufunga vinywa vyao juu ya uzinzi wao, kukiri kutaharibifu mbaya zaidi. Tatizo na hii ni kwamba huzuia dhamiri ya mtu na hairuhusu marejesho ya mahusiano ambayo kuungama ni lengo la kuhusisha. Yakobo 5:16 inasema, "Ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi, na kuombeana, mpate kuponywa."

Mtume Paulo alisema kwa hekima, "Nami ninajizoeza katika neno hili niwe na dhamiri isiyo na hatia mbele za Mungu na mbele ya watu siku zote" (Matendo 24:16). Ingawa uzinzi ni dhambi dhidi ya Mungu, hasa, Biblia pia inasema kwamba miili yetu sio yetu wenyewe, bali pia kwa yule tulioleka naye (1 Wakorintho 7: 4). Tendo la kimwili la ngono ni ishara ya jinsi wanandoa wamefanywa mwili mmoja wakati Mungu akiwaunganisha pamoja katika ndoa (1 Wakorintho 6: 15-16). Kwa sababu hizi, mtu aliyefanya uzinzi anapaswa kuomba na kuruhusu Roho Mtakatifu kumwongoza, akikiri uzinzi katika wakati unaofaa.

Dhamiri ya hatia haitaondoka tu kwa kujaribu kuipuuza. Inaweza, kwa kweli, kusababisha matatizo ya kisaikolojia na hata ya kimwili. Ingawaje inaweza kuwa vigumu kwa mtu yeyote kumwambia mume au mkewe kuwa hakuwa mwaminifu, si lazima tu kwa utimilifu wa ndoa, bali pia kwa uhusiano kati ya mtu na Mungu, ili dhamiri yao iwe wazi na watakuwa na uwezo wa kuishi maisha takatifu na halali.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je, ni lazima nikiri dhambi yangu ya uzinzi kwa mke wangu?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries