settings icon
share icon
Swali

Je, ni mifano gani isiyopingika ya uingiliaji wa Mungu?

Jibu


Uingiliaji wa Mungu ikiwekwa kwa ufupi ni, Mungu kuingilia katika masuala ya ulimwengu. Kuingilia kati kwa Mungu kunaweza kuwa Mungu anasababisha kitu fulani kutokea au Mungu kuzuia kitu kutokea. Wasioamini, wasio na imani, na wasaidizi wanaweza kupata maelezo mengine kwa ajili ya matukio ya ajabu zaidi. Waumini wengine wanaona mifano ya uingiliaji wa Mungu kila mahali, wakiona kuwa matukio inayonekana ghafla kama maelekezo ya wazi kutoka kwa Mungu yaelekee kwenye upande mmoja badala ya mwingine. Kwa hiyo, je, Mungu huingilia katika mambo ya ulimwengu? Ikiwa ndio, je, kuna mifano yoyote isiyoweza kuepukika ya uingiliaji huu wa Mungu? Je! Mungu ameacha alama yoyote za kidole katika kazi ya mikono yake?

Muumini anaweza kuelezea mifano mingi ya kuingilia kati kwa Mungu. Kila kitu kutokana na kushindwa kwa Jeshi la Kihispania hadi kuwepo kwa Israeli ya sasa inanukuliwa kama uthibitisho kwamba Mungu ameingilia kati katika historia. Bila shaka, kuna pia miujiza ya Biblia, iliyoandikwa na mashahidi wa macho na matukio, na uumbaji yenyewe- "mbingu simesema," kama Haydn alivyosema.

Lakini, kwa mtu asiyeamini kwamba Mungu yupo, aginositiki, na wasio amini yale yaliyofumbuliwa, kuna maelezo mengine kwa kila kitu. Hivi karibuni kulikuwa na kipindi katika runinga ambacho kilipeperusha nchini Marekani ambacho kilijaribu kuelezea miujiza ya Biblia. Kipindi kimoja kiliangazia uvuko wa Bahari Nyekundu (angalia Kutoka sura ya 14). Wanasayansi walikuja na nadharia kadhaa, ikiwa ni pamoja na madaraja ya ardhi ya muda mfupi yaliyosababishwa na shughuli za mlipuko wa maji chini ya maji au tetemeko la maji chini ya maji ambalo lilisababisha kimbunga, ambacho lilisababisha kina cha maji kuwa chini sana wakati ambapo Musa na Waisraeli walivuka Bahari Nyekundu. Ingawa nadharia ziliwezekana kisayansi, hakukuwa na ufafanuzi wa jinsi tukio lililotokea kwa wakati wa Waisraeli kuvuka, lakini Wamisri wakaangamizwa wakati walijaribu kuwafuata. Hata kama tukio hilo lingeweza kuelezewa kwa kawaida, linatambulisha sifa za kukataa muujiza wa tukio hilo. Lakini, tena, kwa mtu anayekataa kuwepo na / au kazi ya Mungu duniani, muujiza wowote unaweza kuelezewa kama ulifanyika kwa bahati mbaya, pepo, au udanganyifu. Ikiwa unatafuta sababu za kutoamini, kuwa na uhakika utapata baadhi.

Kwa upande wa kinyume cha mtazamo ni waumini ambao wanaona karibu kila kitu kama mfano wa kuingilia kwa Mungu. Mpango mzuri juu muujiza wa ajabu kutoka kwa Mungu. Mkondo wa ghafla wa upepo au kukutana kwa ghafla na rafiki ni wazi ishara kutoka kwa Mungu wa kueleka upande tofauti. Wakati mawazo haya ni ya kibiblia zaidi kuliko mbinu ya aminiye kuwepo kwa Mungu lakini anakana kunuliwa kwa yaliyo fiche anaweza kuchukua, inaleta shida kubwa. Ufafanusi kuwa takribani kila kitu kuwa na mwingilio wa Mungu kunaweza kusababisha hitimisho kubwa sana. Tunapenda kusoma katika mambo tunayotaka. Inajaribu kusoma maumbo ya wingu ili kupata "ushahidi" kwa kile tunachotaka mapenzi ya Mungu yawe badala ya kutafuta kweli mapenzi ya Mungu kwa njia ya kibiblia (Warumi 12: 1-2).

Kuzungumza Kibiblia, Mungu huingilia kati katika mambo ya ulimwengu (angalia Mwanzo hadi Ufunuo). Mungu ni Mwenye nguvu (Zaburi 93: 1, 95: 3; Yeremia 23:20; Warumi 9). Hakuna kinachotokea kwamba Mungu hajakipangia, kusababisha, au kuruhusu. Sisi daima tunazungukwa na uingiliaji wa Mungu, hata wakati hatujui au tumepofuka kwa hilo. Hatutajua kamwe nyakati zote na njia zote Mungu anaingilia katika maisha yetu. Uingiliaji wa Mungu unaweza kuja kwa namna ya muujiza, kama vile uponyaji au ishara isiyo ya kawaida. Uingiliaji wa Mungu pia unaweza kuja kwa namna ya tukio linaloonekana kama la ghafla linatuongoza kwa namna Mungu anataka tuelekee.

Lakini Biblia haitufundishi kutafuta maana ya siri ya kiroho katika matukio ya kila siku ya maisha. Wakati tunapaswa kuwa na ufahamu kwamba Mungu anaingilia kati, hatupaswi kutumia kila dakika tukijaribu kuamua ujumbe wa siri kutoka hapo juu. Waumini hutafuta Neno la Mungu kwa uongozi (2 Timotheo 3: 16-17) na huongozwa na Roho Mtakatifu (Waefeso 5:18). Tunapaswa kutii chanzo kimoja ambacho tunajua kwamba Mungu amenena kweli, katika Neno Lake (Waebrania 4:12).

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je, ni mifano gani isiyopingika ya uingiliaji wa Mungu?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries