settings icon
share icon
Swali

Kwa nini kuepuka usherati ni muhimu sana?

Jibu


Mungu aliwapa mwanamume na mwanamke furaha ya mahusiano ya ngono ndani ya mipaka ya ndoa, na Biblia imeweka wazi umuhimu wa kudumisha kuepuka usherati ndani ya mipaka ya muungano huo kati ya mume na mke (Waefeso 5:31). Watu wanafahamu athari nzuri ya zawadi hii kutoka kwa Mungu lakini wameichukulia kuwa zaidi ya ndoa na katika hali yoyote. Falsafa ya kidunia ya "ikiwa inahisi vizuri, fanya" imeenea kote katika tamaduni, hususani Magharibi, hadi ambapo kuepuka usherati huonekana kama ya kale na ambayo haihitajiki.

Lakini angalia kile ambacho Mungu anasema kuhusu kuepuka usherati. "Unapaswa kutakaswa, , mwepukane na uasherati; kila mmoja wenu ajue kuuweza mwili wake katika utakatifu na heshima;si katika hali ya tamaa mbaya, kama Mataifa wasiomjua Mungu… Maana Mungu hakutuitia uchafu, bali tuwe katika utakaso. "(1 Wathesalonike 4: 3-5, 7). Kifungu hiki kinaelezea sababu za Mungu za kuepuka usherati katika maisha ya watoto wake.

Kwanza, "tumetakaswa," na kwa sababu hiyo tunapaswa kuepuka usherati. Neno la Kigiriki linalotafsiriwa "kutakaswa" linamaana halisi "kutakaswa, kuwa takatifu, kutengwa kwa kazi ya Mungu. Kama Wakristo, tunapaswa kuishi maisha ya kutakaswa kwa sababu tumekuwa takatifu kwa kubadilishana dhambi zetu kwa ajili ya haki ya Kristo juu ya msalaba na tumefanywa viumbe vipya kabisa katika Kristo (2 Wakorintho 5: 17-21). Hali zetu za zamani, na uchafu wetu wote, ngono na vinginevyo, vimekufa, na sasa maisha tunayoishi, tunaishi kwa imani kwa Yeye aliyekufa kwa ajili yetu (Wagalatia 2:20). Kuendelea katika usherati ni kupinga hayo, na kufanya hivyo, kwa kweli, ni sababu ya halali ya kuuliza kama tumewahi kuzaliwa tena. Utakaso ni mchakato ambapo tunakuwa zaidi na zaidi kama Kristo, ni ushahidi muhimu wa ukweli wa wokovu wetu.

Pia tunaona katika 1 Wathesalonike 4: 3-5 umuhimu wa kudhibiti miili yetu. Tunapoingia kwenye uasherati, tunatoa ushahidi kwamba Roho Mtakatifu hajatujaza kwa sababu hatuna moja ya matunda ya kiroho-kujidhibiti. Waumini wote wanaonyesha matunda ya Roho (Wagalatia 5: 22-23) kwa kiwango kikubwa au cha chini kulingana na ikiwa sisi tunamruhusu Roho kuwa na udhibiti. Tamaa isiyo dhibitiwa ni kazi ya mwili (Wagalatia 5:19), si ya Roho. Kwa hiyo, kudhibiti tamaa zetu na kuishi maisha takatifu ya kuepuka usherati ni muhimu kwa mtu yeyote anayesema anamjua Kristo. Kwa kufanya hivyo, tunaheshimu Mungu na miili yetu (1 Wakorintho 6: 18-20).

Tunajua kuwa sheria za Mungu na nidhamu zinaonyesha upendo Wake kwetu. Kufuata yale anayosema inaweza kutusaidia tu wakati wetu duniani. Kwa kuepuka usherati kabla ya ndoa, tunaepuka kuathiriwa kihisia ambayo inaweza kuathiri mahusiano ya baadaye na ndoa. Zaidi ya hayo, kwa kuweka malazi ya ndoa safi (Waebrania 13: 4), tunaweza kupata upendo kamilifu kwa wenzi wetu wa ndoa, ambao unafuata upendo mkubwa wa Mungu kwetu.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Kwa nini kuepuka usherati ni muhimu sana?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries