settings icon
share icon
Swali

Biblia inasema nini kuhusu kuambukisha roho?

Jibu


Wazo la "kuambukisha roho" ni kweli kwamba mtu anaweza kuambukisha roho mbaya kwa mtu mwingine kwa kugusa au kuwa karibu naye. Wale wanaofundisha dhana hii huwaambia wengine wasijiunge na marafiki au wanajamii ambao wanaweza kuwambukisha roho hiyo. Hakuna msingi wa maandiko kwa dhana ya kuambukisha roho kwa kugusa au kuwa karibu na mtu mwingine au kwa njia nyingine yoyote. Bila shaka, tunaweza kuathiriwa na tabia mbaya au tabia za dhambi za wengine, lakini kuzitambua hizi pepo kama viumbe vya roho ambazo zinaweza kuambkishwa kwa wengine sio la kibiblia.

Biblia inasema kuna aina mbili za viumbe wa roho, malaika ambao hawakuanguka, watakatifu na malaika waliomfuata Shetani katika uasi wake. Malaika ambao hawajafanya dhambi huitwa roho wa watumishi (Waebrania 1:14), na tunaambiwa kwamba Mungu huwatuma kuwatumikia wale ambao watakuwa warithi wa wokovu, yaani, wale wanaoamini katika Kristo kama Mwokozi wao. Malaika waliojiunga na Shetani katika uasi wake wamehifadhiwa katika giza (Yuda 1: 6) na hufanywa viumbe wa kiroho (mapepo) wakfu kwa uovu.

Biblia inaandika mfano mmoja tu wa pepo wanaambukishwa kutoka kiumbe mmoja hadi mwingine. Iliyotokea wakati Yesu alihamisha kikosi cha mapepo kutoka kwa watu na wakaingia ndani ya kundi la nguruwe (Mathayo 8: 28-34). Yesu hakurudia muujiza huu, wala hakuwahi kuwaonya wanafunzi Wake (au sisi) kuhusu roho za kuambukisha. Hakuna sababu ya mzaliwa katika Kristo kumwogopa Shetani au malaika wake walioanguka. Ikiwa tutamtoroka, atatukimbia pia. "Basi mtiini Mungu. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia" (Yakobo 4: 7). Kama waumini wa kweli, mwili wetu ni hekalu la Roho Mtakatifu. Tunaweza kuwa na uhakika kwamba Roho Mtakatifu hawezi kuruhusu pepo katika hekalu lake.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Biblia inasema nini kuhusu kuambukisha roho?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries