settings icon
share icon
Swali

Je! koinonia ni nini?

Jibu


Koinonia ni neno la Kiyunani ambalo linatokea mara 20 katika Biblia. Maana ya kimusing ya koinonia ni "ushirika, kushiriki pamoja, chakula." Tukio la kwanza la koinonia lapatikana katika Matendo 2:42, "Nao wakawa wanadumu katika mafundisho ya mitume, katika ushirika, katika kumega mkate na katika kusali." Ushirika wa Kikristo ni nguzo muhimu ya maisha ya Mkristo. Waumini katika Kristo wanafaa kuja pamoja kwa upendo, Imani, na kuhimizana. Hicho ndicho kiini cha koinonia.

Wafilipi 2: 1-2 inasema kwamba, "Kama kukiwa na jambo lolote la kutia moyo katika kuunganishwa na Kristo, kukiwa faraja yoyote katika upendo wake, kukiwa na ushirika wowote na Roho, kukiwa na wema wowote na huruma, basi ikamilisheni furaha yangu kwa kuwa na nia moja, mkiwa na upendo huo moja, mkiwa wa roho na kusudi moja." Koinonia ni kukubaliana na kila mmoja, kuunganishwa kwa kusudi, na kuhudumu pamoja. Koinonia yetu na kila mmoja wetu inategemea koinonia yetu ya kawaida na Yesu Kristo. Yohana wa Kwanza 1: 6-7 inasema, "Kama tukisema kwamba twashirikiana naye huku tukienenda gizani, twasema uongo, wala hatutendi lililo kweli. 7Lakini tukienenda nuruni, kama yeye alivyo nuruni, twashirikiana sisi kwa sisi na damu yake Yesu, Mwana wake, yatusafisha dhambi yote."

Mfano mzuri sana wa jinsi koinonia inapaswa kuonekana unaweza kupatikana katika utafiti wa kifungu "kila mmoja" katika Biblia. Maandiko yanatuamuru tujitolee sisi kwa sisi (Warumi 12:10), tuheshimiane (Warumi 12:10), tuishi kwa umoja sisi kwa sisi (Warumi 12:16; 1 Petro 3: 8), tukubaliane (Warumi 12:10) 15: 7), tutumikianeni kwa upendo (Wagalatia 5:13), muwe wenye fadhili na wenye huruma (Waefeso 4:32), kuonyana (Wakolosai 3:16), kuhimizana (1 Wathesalonike 5:11; Waebrania 3:13), tutiane moyo kwa upendo na matendo mema (Waebrania 10:24), kuwa na ukarimu (1 Petro 4: 9), na kupendana (1 Petro 1:22; 1 Yohana 3:11; 3:23; 4: 7; 4: 11-12). Hivyo ndivyo koinonia ya kweli ya kibiblia inapaswa kuonekana.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je! koinonia ni nini?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries