settings icon
share icon
Swali

Kitabu cha Henoko ni kipi na je kinafaa kuwa kwenye Bibilia?

Jibu


Kitabu cha Henoko ni moja kati ya mchanganyiko ya hekaya nyingi [kinachohusishwa kiuongo na mistari yake ambayo waandishi wake hawatambuliki] kazi ambaayo inajihusisha na Henoko, babu mkuu wa Nuhu; ambaye ni Henoko mwana wa Yaredi [Mwanzo 5:16]. Henoko pia ni mmoja wa watu watatu kwenye Bibilia ambao walipelekwa mbinguni wakiwa hai [wengine Zaidi na wa kipekee ni pamoja na Eliya na Yesu],jinsi bibilia inavyo sema "Henoko akaendaa pamoja na Mungunaye akatoweka ;maana Mungu alimtwaa" [Mwanzo 5:24; pia tazama Waebrania 11:5]. Kwa kawaida,tamko "kitabu cha Henoko" inahashiria 1Henoko, ambacho kimenakiriwa katika lugha ya Kiithiopia.

Kitabu cha Bibilia cha Yuda kinanakiri kutoka kitabu cha Henoko sura ya 14-15, "Henoko aliyekuwa wa saba kutoka Adamu,alitabiri kuhusu hao wanaume: "Tazama,Bwana anakuja na maelfu ya maelfu wa watakatifu wake kuhukumu kila mmoja, na kuwafunga wote wa miungu na njia zao zizotakatifu zilizotendwa kwa njia isiyo ya kweli, na maneno yote makali ya watenda dhambi waliyonena dhidi yake." Ila haya maneno hayamaanishi kuwa kitabu cha Henoko kilielekezwa na Mungu na hivyo kiwemo kwenye Bibilia.

Nukuu la Yuda silo tu la kipekee katika Bibilia lisilokuwa na misingi ya kibibilia.Paulo Mtumwa anataja Wakrete katika Tito 1:12 ila hiyo haimaanishi kuwa tunafaa kuyapa idhini yoyote ya ziada maandishi ya Wakrete. Hayo pia ni ya kweli na Yuda sura 14-15. Yuda kunukuu kutoka kitabu cha Henoko haiashirii kuwa kitabu chote cha Henoko kilielekezwa na Roho, ama hata kuwa na ukweli wowote. Kinachomaanisha hapa ni kuwa baadhi ya vifungo vina ukweli. Inashangaza jinsi hata wasomi hakuna anayeamini kuwa kitabu cha Henokoni kweli kiliandikwa na Henoko anayetajwa kwenye Bibilia. Henoko alikuwa vizazi saba kutoka Adamu, kabla ya mafuriko [Mwanzo 5:1-24]. Tibitisho kwa hakika hilo ni ukweli kama alivyotabiri Henoko- isingekuwa hivyo bibilia haingemrejelea, Na Henoko, mtu wa saba baada ya Adamu, alitoa maneno ya unabii juu ya hao" [Yuda 1:14] Haya maelezo ya Henoko yalisimuliwa kwa tamaduni, na kisha baadaye kunakiriwa kwenye kitabu cha Henoko

Tunafaa kukichukulia kitabu cha Henoko na uzito [na vitabu vingine kama hivyo] kama vile tunavyofanya maandishi mengine ya kiroho. Baadhi ya maneno yanayosemwa na manabii wa uongo yana ukweli na usawa, ila kwa wakati mwingine mengineyo yana uongo na yasiyo kweli kihistoria. Ikiwa utavisoma hivi vitabu, unafaa kuvichukulia kuwa vinapendeza ila vyenye uongo kwenye nakala za kihistoria, sio kama neno la Mungu lililoongozwa na Roho mtakatifu.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Kitabu cha Henoko ni kipi na je kinafaa kuwa kwenye Bibilia?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries