settings icon
share icon
Swali

Je! Ni nini kipawa cha kutia moyo?

Jibu


Kipawa cha kutia moyo au kuhimiza hupatikana katika orodha ya Paulo ya vipawa katika Warumi 12:7-8. Neno lililotafsiriwa kuwa "kutia moyo" au "kuhimiza" ni neno la Kigiriki paraklésis, lililohusiana na neno paraclete. Paraklésis kimsingi inamaanisha "wito kwa upande wa mtu."

Paraklésis hubeba wazo la kumleta mtu karibu pamoja ili "kumhimiza," "kumwonya," "kumtia moyo," "kumpa furaha," na "kumfariji". Vitendo hivi vyote hufanya kipawa cha kutia moyo. Kwa mfano, mara kwa mara Paul aliwaonya na kuwahimiza wasomaji wake wafanye kazi kwenye kitu alichoandika. Mfano mzuri ni Warumi 12:1-2, ambapo Paulo anawahimiza Warumi kuwasilisha miili yao kwa Mungu kama dhabihu iliyo hai. Kwa kufanya hivyo, wangejua na kuelewa mapenzi ya Mungu.

Kwa kupendeza, wakati Yesu alizungumza na wanafunzi Wake usiku wa kukamatwa kwake, alizungumza juu ya Roho Mtakatifu kama "Msaidizi" au "Mfariji" (Yohana 14:16, 26; 15:26), ndio maana Roho Mtakatifu wakati mwingine hujulikana kama "Paraclete," Yeye anayekuja pamoja kuhimiza na kututia moyo.

Mtu mwenye kipawa cha kiroho cha kutia moyo anaweza kutumia kipawa chake katika mipangilio ya umma na ya kibinafsi. Kuhimiza ni muhimu katika ushauri, ufundishaji, ushauri, na kuhubiri. Mwili wa Kristo umejengwa kwa imani kama matokeo ya huduma ya wale walio na kipawa ch kutia moyo.

Kipawa cha kutia moyo au kuhimiza hutofautiana na kipawa cha kufundisha katika himizo hilo linalenga katika matumizi ya Biblia. Kwa maana mtu mwenye kipawa cha kufundisha anazingatia maana na maudhui ya Neno, na mwenye kipawa cha kuhimiza analenga katika matumizi ya Neno. Yeye anaweza husisha kwa wengine, kwa makundi na kibinafsi, kwa kuelewa, huruma, na uongozi wa kusaidia. Kufundisha inasema, "Hii ndiyo njia unapaswa kwenda"; kuhimiza inasema, "Nitakusaidia kwenda njia hiyo." Mtu mwenye kipawa cha kuhimiza anaweza kusaidia mtu mwingine kuhama kutoka kwa kukosa rajua na kuwa na matumaini.

Pengine mfano bora wa Kibiblia wa mtu mwenye kipawa cha kutia moyo ni Barnaba. Jina lake halisi ni Yusufu, lakini mitume walimwita "Barnaba," linalomaanisha "mwana wa kutia moyo" (Matendo 4:36). Tunamwona Barnaba katika Matendo ya Mitume 9:27 akija pamoja na Paulo aliyebadilika karibuni na kumtambulisha kwa kanisa hadhari. Katika Matendo 13:43 Barnaba anawahimiza waumini kuendelea katika neema ya Mungu. Katika Matendo 15: 36-41 Barnaba anachagua Yohana Marko kama mwenzi wa huduma, licha ya Marko kuacha jitihada ya kimisionari ya awali. Kwa maneno mengine, Barnaba alimpa Marko fursa ya pili. Yote kupitia kwa huduma ya Barnaba, alionyesha ushahidi wa kipawa cha kuhimiza, kuwaita wengine kwa upande wake ili kuwasaidia, kuwafariji, na kuwahimiza kuwa wafanisi zaidi kwa Kristo.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je! Ni nini kipawa cha kutia moyo?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries