settings icon
share icon
Swali

Je, kifungu cha kipekee ni gani?

Jibu


"Kifungu cha kipekee" ni maneno ya Yesu katika Mathayo 5:32 na 19: 9 "isipokuwa kwa habari ya uasherati." Inatoa kifungu cha "kipekee" cha kuoa tena baada ya talaka kuzingatiwa uzinzi. Mathayo 5:32 inasema, "lakini mimi nawaambia, Kila mtu amwachaye mkewe, isipokuwa kwa habari ya uasherati, amfanya kuwa mzinzi; na mtu akimwoa yule aliyeachwa, azini." Vivyo hivyo, Mathayo 19: 9 inasema, "Nami nawaambia ninyi, Kila mtu atakayemwacha mkewe, isipokuwa ni kwa sababu ya uasherati, akaoa mwingine, azini; naye amwoaye yule aliyeachwa azini." Hivyo, ni nini hasa "kutokuwa na uaminifu katika ndoa," na kwa nini ni kifungu cha kipekee kwa maneno ya Yesu kwamba kuoleka baada ya talaka ni uzinzi?

Maana ya Mathayo 5:32 na 19: 9 ii wazi. Ikiwa mtu anapata talaka na kisha kuolewa tena, inachukuliwa kuwa uzinzi isipokuwa kifungu cha kipekee kinatumika kwao. Maneno ya "kutokuwa na uaminifu katika ndoa" ni tafsiri ya neno la Kiyunani porneia, neno ambalo tunapata neno letu la kisasa "ponografia." Maana muhimu ya porneia ni "ngono ya upotoshavu." Katika vitabu vya Kigiriki karibu wakati huo huo kama Agano Jipya, porneia ilitumiwa kurejelea uzinzi, uasherati, ukahaba, zinaa ya maharimu, na ibada ya sanamu. Inatumiwa mara 25 katika Agano Jipya, mara nyingi hutafsiriwa "uasherati."

Maana ya porineia katika Agano Jipya inaonekana kuwa dhana ya jumla ya ngono ya kupotosha. Maneno mengine ya Kiyunani hutumiwa kutaja aina maalum za ngono ya kupotosha, ni kama uzinzi. Kwa maana hii katika akili, kwa mujibu wa kifungu cha kipekee, ushiriki wowote katika uovu wa kijinsia / uovu ni kinyume na maneno ya Yesu kwamba kuolewa baada ya talaka ni uzinzi. Ikiwa mwenzi mmoja amefanya uzinzi, au tendo lolote la ngono ya kupotosha, na matokeo yake kuwa talaka, basi mwenzi "asiye na hatia" yu huru kuoa tena bila kuchukuliwa kuwa ni uzinzi.

Tafadhali elewa, ingawa, kifungu cha kipekee si amri ya talaka na / au kuoa tena. Yesu hakusema kwamba ikiwa kutakuwa na uaminifu katika ndoa wanandoa wanapaswa talakana. Yesu hakusema kwamba ikiwa talaka itatokea kutokana na uovu wa ndoa, mke asiye na hatia anapaswa kuoa tena. Kwa zaidi, Yesu anatoa fursa ya talaka au kuolewa tena kuwepo. Hakuna vile Yesu anatangaza kuwa talaka na na kuoa tena kuwa chaguo bora au pekee. Toba, msamaha, ushauri, na urejesho ndivyo Mungu ananuia kwa ndoa zilizoharibiwa na kutokuamiana. Mungu anaweza kuponya ndoa yoyote ambayo wote wawili wanajitolea kwake na wako tayari kufuata Neno Lake.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je, kifungu cha kipekee ni gani?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries