settings icon
share icon
Swali

Je, utafsiri wa kibiblia ni nini?

Jibu


Utafsiri wa Kibiblia ni somo la kanuni na mbinu za kutafsiri maandiko ya Biblia. 2 Timotheo 2:15 inawaamuru waumini kushiriki katika kanuni za utafsiri: "Jitahidi kujionyesha kuwa umekubaliwa na Mungu, mtenda kazi. . . ukitumia kwa halali neno la kweli. "Madhumuni ya somo la kanuni za utafsiri wa kibiblia ni kutusaidia kujua jinsi ya kutafsiri vizuri, kuelewa, na kuitumia Biblia katika hali halisi.

Sheria muhimu zaidi ya utafsiri wa kibiblia ni kwamba Biblia inapaswa kutafsiriwa kifasaha. Tunapaswa kuelewa Biblia kwa maana yake ya kawaida au wazi, isipokuwa kifungu hicho kinakusudiwa kuwa kiashiria au ikiwa mfano wa hotuba umetumiwa. Biblia inasema kile inachomaanisha na inamaanisha kile isemacho. Kwa mfano, wakati Yesu anaongea kuhusu kuwalisha " watu elfu tano" katika Marko 8:19, sheria ya utafsiri inasema tunapaswa kuelewa elfu tano kifasaha — kulikuwa na umati wa watu wenye njaa waliokuwa takribani elfu tano ambao walilishwa kwa mkate halisi na samaki na Mwokozi mtenda miujiza. Jaribio lolote la "kuifanya kiroho" idadi au kukataa muujiza halisi ni kufanya udhalimu kwa maandishi na kupuuza lengo la lugha, ambalo ni kupasha ujumbe. Watafsiri wengine hufanya makosa ya kujaribu kusoma kati ya mistari ya Maandiko ili kutoa maana maalumu ambazo haziko katika maandishi halisi, kama kwamba kila kifungu kina ukweli wa kiroho uliofichwa ambao tunapaswa kufumbua. Utafsiri wa Kibiblia hutuweka waaminifu kwa maana inayokusudiwa ya Maandiko na mbali na kutaja mistari ya Biblia ambayo inapaswa kueleweka kifasaha.

Sheria ya pili muhimu ya utafsiri wa kibiblia ni kwamba vifungu lazima vitafsiriwe kihistoria, kwa lugha, na kwa muktadha. Kutafsiri kifungu kihistoria inamaanisha ni lazima tutafute kuelewa utamaduni, historia, na hali ambayo imesababisha maandiko. Kwa mfano, ili kuelewa kikamilifu kukimbia kwa Yona katika Yona 1: 1-3, tunapaswa kuchunguza historia ya Waashuri kuambatana Isiraeli. Kutafsiri kifungu kwa lugha inahitaji mtu kufuata sheria za lugha na kutambua tofauti za Kiebrania na Kigiriki. Kwa mfano, wakati Paulo anaandika juu ya "Mungu mkuu na Mwokozi wetu, Yesu Kristo" katika Tito 2:13, sheria za lugha zataja kwamba Mungu na Mwokozi ni maneno yanayoambatana na yote yanaashiria kwa Yesu Kristo-kumaanisha, Paulo kwa hakika anamwita Yesu "Mungu wetu mkuu." Kutafsiri kifungu kimuktadha ujumuisha kutia maanani muktadha wa mstari au kifungu wakati unapojaribu kufahamu maana. Muktadha unajumuisha vifungu chache kabla na baada ya, sura, kitabu, na kwa ujumla, Biblia nzima. Kwa mfano, maneno mengi ya kushangaza katika Mhubiri yanafafanuliwa zaidi wakati yanawekwa katika muktadha wake-kitabu cha Mhubiri kiliandikwa kutokana na mtazamo wa kidunia "chini ya jua" (Mhubiri 1: 3). Kwa kweli, maneno chini ya jua yanarudiwa takribani mara thelathini katika kitabu, kuandaa muktadha wa yote ambayo ni "ubatili" katika ulimwengu huu.

Sheria ya tatu ya utafsiri wa kibiblia ni kwamba Maandiko daima ni mkalimani bora wa Maandiko. Kwa sababu hii, mara mingi tunalinganisha Maandiko na Maandiko wakati tunapojaribu kufahamu maana ya kifungu. Kwa mfano, hukumu ya Isaya ya tamaa ya Yuda ya kutafuta msaada wa Misri na kutegemea kwao wapanda farasi wenye nguvu (Isaya 31: 1) ulitiwa motisha, kwa sehemu, na amri ya wazi ya Mungu ya kuwa watu wake wasiende Misri kutafuta farasi (Kumbukumbu la Torati 17:16) ).

Watu wengine huepuka kusomea utafsiri wa kibiblia kwa sababu wanaamini kimakosa kuwa watapunguza uwezo wao wa kujifunza ukweli mpya kutoka kwa Neno la Mungu au kuzuia mwanga wa Roho Mtakatifu wa Maandiko. Lakini hofu zao hazina msingi. Utafsiri wa Kibiblia ni kuhusu kutafuta tafsiri sahihi ya maandiko yaliyoongozwa na Roho Mtakatifu. Madhumuni ya utafsiri wa kibiblia ni kutulinda kutokana na kutumia maandiko vibaya au kuruhusu mapendeleo kutia doa kuelewa ukweli. Neno la Mungu ni ukweli (Yohana 17:17). Tunataka kuona ukweli, kujua ukweli, na kuishi kikweli tunavyoweza, na hiyo ndiyo sababu utafsiri wa kibiblia ni muhimu.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je, utafsiri wa kibiblia ni nini?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries