settings icon
share icon
Swali

Teolojia ya Biblia ni nini?

Jibu


Teologiolojia ya kibiblia ni utafiti wa mafundisho ya Biblia, iliyopangwa kulingana na muda wao na historia. Tofauti na teolojia ya utaratibu, ambayo inaweka mafundisho kulingana na mada maalum, teolojia ya kibiblia inaonyesha matukio ya ufunuo wa Mungu kama ulivyoendelea katika historia. Teolojia ya Kibiblia hutenganisha na kuelezea mafundisho ya kiteolojia ya sehemu maalum ya Maandiko, kama vile teolojia ya vitabu vitano vya kwanza vya Agano la Kale au teologia iliyo na ndani ya maandishi ya Yohana, nk. Inaweza kuzingatia kipindi fulani cha wakati, kama teolojia ya miaka ya umoja wa ufalme. Kikundi kingine cha teolojia ya kibiblia kinaweza kufunza mada fulani katika Biblia: utafiti wa "walio baki," kwa mfano, inaweza kutafuta jinsi mada hiyo inavyoelezwa na kuendelezwa katika Maandiko.

Wengi humsifia J. P. Gabler, mwanachuoni wa Ujerumani wa kibiblia, kwa kuanzisha teolojia ya kibiblia. Alipokuwa akiapishwa kama profesa mwaka wa 1787, Gabler alitafuta tofauti kubwa kati ya teolojia ya kimantiki (utaratibu au mafundisho) na teolojia ya kibiblia. Kwa Gabler, theolojia ya kibiblia lazima iwe na uchunguzi wa kihistoria wa kile kilichoaminiwa na kufundishwa katika vipindi mbalimbali vya historia ya kibiblia, bila kutegemea mambo ya kisasa ya kidini, mafundisho, falsafa, au kiutamaduni. Kwa ujumla, kanuni ambazo Gabler alitaka zilikuwa sahihi, na alishawishi maendeleo ya teolojia ya kibiblia kwa miaka mingi ijayo.

Hata hivyo, ni lazima ieleweke kwamba hakuna kitu kama kujifunza Biblia kwa uzingatifu kamili. Kila mkalimani huleta fikra fulani katika mafunzo ya Biblia. Vikwazo hivi vina ushawishi mkubwa juu ya mchakato wa kutafsiri Maandiko. Matokeo yake ikiwa ni kwamba mafundisho ya teolojia ya kibiblia linatambuliwa na kila maoni na tofauti ya kile Biblia inafundisha. Theolojia ya Kibiblia inategemea kabisa jinsi mtaalamu anavyoitafsiri. Njia zinazotumika katika kutafsiri Maandiko ni muhimu kwa teolojia ya kibiblia. Theolojia ya mtu fulani ya kibiblia haiwezi kuwa bora kuliko njia ambazo anatumia kutafsiri Maandiko.

Hapa kuna tofauti ya msingi kati ya teolojia ya utararibu na ya kibiblia: Teologia ya utaratibu inauliza, "Je! Bibilia kwa ujumla inasema nini juu ya malaika?" Na kisha inachunguza kila kifungu kinachohusiana na umalaika, hufanya hitimisho, na kuandaa habari zote pamoja ya mafundisho kuhusu malaika. Hivyo basi tunapata kwamba kutoka Mwanzo hadi Ufunuo, kuna jumla ya ukweli wa Mungu uliofunuliwa juu ya jambo hilo.

Teolojia ya Kibiblia anauliza, "Kuelewa kwetu kwa malaika kulikuaje katika historia ya kibiblia?" Na kisha huanza na fundisho la vitabu za kwanza tano za agano la kale kuhusu malaika na huonyesha ufunuo wa Mungu wa maendeleo ya viumbe hivi katika Maandiko. Katika mchakato huo, mwanateolojia wa kibiblia anatoa hitimisho kuhusu jinsi fikra. Za watu kuhusu malaika ilivyobadilika, wakati ukweli zaidi ulipofunuliwa. Hitimisho la utafiti huo ni, kwa kweli, kuelewa kile Biblia inasema juu ya malaika, lakini pia huweka ujuzi huo katika "picha kubwa zaidi" ya ufunuo wa Mungu wote. Teolojia ya Kibiblia inatusaidia kuona Biblia kama mshikamano mzima, badala ya kuwa mkusanyiko wa pointi zisizohusiana na mafundisho.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Teolojia ya Biblia ni nini?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries