settings icon
share icon
Swali

Waumini wanawezaje kuwa katika ulimwengu, lakini wasiwe wa ulimwengu?

Jibu


Tunaposoma "ulimwengu" katika Agano Jipya, tunasoma neno la Kigiriki 'anga.' Anga mara nyingi inahusu dunia iliyokaliwa na watu wanaoishi duniani, ambayo hufanya kazi pasipo na udhibiti wa Mungu. Shetani ndiye mtawala wa "ulimwengu" huu (Yohana 12:31; 16:11; 1 Yohana 5:19). Kwa ufafanuzi rahisi kwamba neno dunia linamaanisha mfumo wa ulimwengu ulioongozwa na Shetani, tunaweza kufahamu zaidi madai ya Kristo kwamba waumini sio tena wa ulimwengu — hatutahukumiwa tena na dhambi, wala hatufungwi tena na kanuni za ulimwengu. Kwa kuongeza, tunabadilishwa kuwa mfano wa Kristo, na kusababisha tamaa yetu katika mambo ya dunia kupungua tunapokomaa katika Kristo.

Waumini katika Yesu Kristo wamo duniani-kimwili -lakini wao sio wa ulimwengu, sio sehemu ya maadili yake (Yohana 17: 14-15). Kama waumini, tunapaswa kujitenga mbali na ulimwengu. Hii ndiyo maana ya kuwa mtakatifu na kuishi maisha takatifu, kutakaswa. Hatupaswi kushiriki katika shughuli za dhambi ambazo ulimwengu huendeleza, wala hatutakiwi kuwa na akili mbaya, yenye uharibifu ambayo ulimwengu huandaa. Badala yake, tunapaswa kuyalainisha mawazo yetu, kuwa sambamba na yale ya Yesu Kristo (Warumi 12: 1-2). Hii ni shughuli ya kila siku na ya kujitolea.

Pia tunapaswa kuelewa kuwa kuwa katika ulimwengu, lakini sio wa ulimwengu, ni muhimu kama tutakuwa mwanga kwa wale walio katika giza la kiroho. Tunapaswa kuishi kwa njia ya kuwa wale walio nje ya imani wanaona matendo yetu mazuri na namna yetu na kujua kwamba tuna kitu "tofauti." Wakristo wanaofanya kila jitihada za kuishi, kufikiri na kutenda kama wale wasiomjua Kristo hufanya makosa. Hata wale wasiomtambua Mungu wanajua kwamba "kwa matunda yao mtawajua" (Mathayo 7:16), na kama Wakristo, tunapaswa kuonyesha matunda ya Roho ndani yetu.

Kuwa "katika" ulimwengu pia inamaanisha tunaweza kufurahia mambo ya ulimwengu, kama vile viumbe vyema ambavyo Mungu ametupa, lakini hatupaswi kujitosa ndani ya kanuni za ulimwengu, wala tusijiridhishe ma mambo ya ulimwengu. Kujiridhisha sio wito wetu tena katika maisha, kama ilivyokuwa hapo kale, lakini badala yake ibada ya Mungu.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Waumini wanawezaje kuwa katika ulimwengu, lakini wasiwe wa ulimwengu?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries