settings icon
share icon
Swali

Tutajifunza yapi kukota kwa uhai wa Samweli?

Jibu


Samweli, linalomaanisha "kumsikia Mungu," alimpewa Mungu na mamaye, Hana, jinsi alivyoahidi hata kabla ya yeye kuingia duniani (1 Samweli 1:11). Hana ambaye alikuwa tasa na alisali kwa uchungu mno kwa ajili ya mwana hadi Eli mhubiri akamdhania kuwa mlevi (1 Samweli 1). Bwana akajibu toba ya Hana, na, kwa kutii aliyoahidi, akamtolea Mungu mtoto huyo ambaye ni Samweli. Samweli alipotolewa matiti, karibia miaka mine, alichukilia matabahuni kumtumikia Mungu kwa uongozi wa Eli kuhani mkuu (1 Samweli 1: 22-25). Hata alipokuwa mwana, Samweli alipewa naivera ya kitani, lililohifadhiwa kwa kuhani wakati akihudumu kwa Mungu katika hekalu kule Shilo, ambapo paliwekwa sanduku la Mungu (1 Samweli 2:18; 3: 3). Kawaida, watoto wa muhubiri ndio wangemrithi mzazi katika huduma yake; ila, watoto wa Eli, Hophni na Finehasi, walikuwa waasi maana walikuwa malaya na kudhihirisha kutoshughulika katika kumtolea Mungu kafara (1 Samweli 2:17, 22). Ingawa, Samweli akazidi kukua akapata kibali kwa Bwana na watu pia (1 Samweli 2:26).

Zamani pale maono na unabii havikuchukuliwa, Samweli alisikia kuwa aliitwa na kuamini kuwa ni Eli aliyemwita wakati wa kiza. Ingawa kijana Samweli alifanya ibada pale hekaluni, bado alikuwa hamjui Mungu bado, na neno la Bwana lilikuwa bado halijafunuliwa kwake. (1 Samweli 3: 7). Hiyo mara tatu ya kwanza Bwana alimwita Samweli, mwana huyo alimwendea Eli. Eli baadaye akafahamu yaliyokuwa yakijiri na kumwarifu Samweli kumitikia Mungu mara atakapoita. Ndipo, "Bwana akaja akasimama,akaita vile vile kama kwanza, Samweli akasema Nena Bwana kwa kuwa mtumishi wako anasikia" (1 Samweli 3:10). Bwana akampa neno la kuhukumu amchukulie Eli. Siku iliyofuata, Samweli alijipa moyo wa Imani, akamjuza Eli yote, japokuwa maneno yale yalikuwa habari ya kusikitisha kwa Eli na jamii yake (1 Samweli 3: 11-18). Eli aliitikia kwa kukubali. Ujuzi wa Samweli kama nabii utajulikana Israeli yote, na Bwana akajivunua kwa taifa lake kupitia Samweli (1 Samweli 3: 20-21).

Wafilisti, maasidi wa kitambo wa Israeli, walivamia taifa la Bwana. Watoto wa Eli walikufa kwenye mapambano, na sanduku la agano likanyakuliwa na kuchukuliwa Filistia. Alipopata taarifa kuhusu kufa kwa watoto wake, Eli akafa vile vile. Miezi kadhaa baadaye, Wafilisti wakarejesha agano Israeli, pale likasalia Kiriath Jearimu kupita miaka ishirini. Waisraeli walipojimwaga kwa Bwana kwa usaidizi dhidi ya Wafilisti waliowadhulumu, Samweli akawaambia watupe sanamu za uongo walizokuwa wakiomba. Katika utawala wa Samweli, pia kwa uwezo wa Bwana, Wafilisti walizimwa, na kukawa na kipindi cha furaha miongoni mwao. (1 Samweli 7: 9-13). Samweli akatambulika kuwa kuhani katika Israeli.

Ilivyo katika watoto wa Eli, watoto wawili wa Samweli, Yoeli na Abiya, walitenda makosa kwa Mungu kwa kupokea rushwa na kupotosha hukumu. Samweli aliwafanya watoto wake waamuzi, ndipo wazee wa Israeli wakamwambia Samweli kuwa kwa maana amekuwa ajuza na watoto wake hawakufuata mienendo yake, basi na awafanyie mfalme awaamue mfano wa mataifa mengine (1 Samweli 8: 1) -5). Neno hilo mwanzo likawa baya machoni pa Samweli, naye akasali Mungu kulihusu. Bwana akamwambia Samweli kwamba hawakukukataa wewe,bali wamenikataa mimi ili nisiwe mfalm juu yao. Mungu akaambia Samweli kutoka na kuisikiliza sauti yao walakini akawaonya na kuwaonyesha desturi ya mfalme atakayewamiliki (1 Samweli 8: 6-21).

Wakati ule, Sauli, Mbenjamini, alipakwa mafuta na Samweli kuwa mtawala wa kwanza wa Israeli (1 Samweli 10: 1). Ingawa, Samweli alimwita Bwana awape onyesho Waisraeli maovu yao ya kujitakia mfalme wa ulimwengu badala ya Mungu (1 Samweli 12: 16-18). Muda uliposonga, Samweli alitambua kuwa Sauli hajamridhisha Mungu katika kuwatawala taifa lake kwa maana Sauli alifanya upumbavu (1 Samweli 13: 11-13). Samweli bila kukawia akamuonya Sauli kuwa Bwana alishapata atakayekuwa mfalme kumliko (1 Samweli 13:14). Sauli alipozidi kufanya upumbavu, Samweli akamkataa kuwa mtawala (1 Samweli 15:26). Samweli akarejea maskani, hakuenda tena kuonana na Sauli, walakini alimlilia (1 Samweli 15:35). Bwana alimwamuru Samweli kumtambua mtawala katika nyumba ya Yese (1 Samweli 16: 1), na Samweli akampaka mafuta aliyekuwa kitindamimba wa Yese, Daudi (1 Samweli 16:13). Samweli akapoteza uhai kabla ya Daudi kuwa mtawala, ingawa, "nao Israeli wote wakakusanyika wakamwomboleza" (1 Samweli 25: 1).

Maisha ya Samweli yalikuwa ya maana kwenye historia ya Israeli.Aliwapaka mauta watawala wawili wa mwanzo wa Israeli,kwa kuwa alikuwa kuhani, pia ndiye wa tamati kwenye makuhani wa Israeli,na kutambulika na umati kama nabii mkuu (Matendo 13:20). Samweli amejulikana akiwa na Musa na Haruni kuwa waliomtambua Bwana naya akawaitikia (Zaburi 99: 6). Mwishowe kwenye masimulizi ya Israeli, pale Waisraeli walipoishi katika kutomtii Bwana, Mungu akanena kwamba walizidi hata ulinzi wa Musa na Samweli, wakuhani wakutambulika katika Israeli (Yeremia 15: 1). Haya ni mambo dhahiri kuwa nguvu za maombi ya Samweli-na uzito wa maasi ya Israeli kwa nyakati za Yeremia.

Mengi yatasomwa kutoka kwa uhai wa Samweli. Zaidi, tunatambua utawala wa Bwana kule Israeli, hata kama ni nani taifa walimpendelea kuwaongoza. Tuna uwezo kukubalia chochote ama yeyote kuingia kwenye patakatifu pa roho zetu, walakini Bwana atabaki kuwa mkuu na hawezi ruhusu waasi kwenye utawala wake katika uhai wa wanaomuishia.

Si rahisi kufahamu jinsi Samweli alitaabika akiwa angali kijana kutoa uamuzi wa kweli kutokana na aliyoonyeshwa kuhusu Eli. Kwa kungamua tu,hata katika umri kidogo,Samweli alimtumikia Mungu kwanza hadi tangu kitambo. Kuna wakati mwingine tunaweza kuhisi kudhulumiwa na wanaotawala, ila, jinsi Samweli alivyodhihirisha mara kadhaa, ni Bwana tu angepaki kuabudiwa. Ulimwengu unaweza tuona wasio thamani tunapokuwa na imani thabiti. Bila tishio, tutakuwa na ujasiri kuwa Bwana atawaamua waliomtumainia na kuaminia Injili yake (Zaburi 135: 14).

Ingawa Samweli alijawa kutoamini kuhusu kuacha taifa liwe na mtawala, alifanya haraka kutafuta maoni ya Bwana kuhusu matakwa hayo na akaitikia mwelekeo alioutoa (1 Samweli 8: 6-7). Tunaweza tafuta ushauri wa Bwana kwenye uhai wetu, ila si wengi tuko radhi kuitikia mwelekeo wake, kama pale inapokuwa inakinzana mna matarajio yetu? Watawala haswa wanapaswa jifunza kutoka kwa maonyesho ya nguvu za Samweli alioupata kutoka kwa kumtegemea Bwana iliyoanzishwa na maisha ya maombi yaliyo thabiti. Samweli aliyekuwa mtu aliyekomaa katika sala, na jamii yake ikamuinamia kwa sababu hiyo (1 Samweli 12:19, 23). Hata kama Samweli aliahamu maovu kwenye uhai Sauli, hakukoma kumuombea na kumlilia. Bila shaka, Samweli alifafanua jinsi ilivyo makosa kukosa kuwafanyia toba wale aliowaongoza. Ila kwa haraka tutawaona wenzetu kusidi ukombozi tunapomwangalia akiingia kwenye dhambi. Hata ivo, malengo ya Mungu kwa kila mmoja utakuja kuwa,ila haifai kuwa kizuizi cha kuendelea kusali na kuwashughulikia wanyonge kwa imani yao (Warumi 15: 1, 1 Wathesalonike 5:14).

Maudhui makuu kote uhai wa Samweli ni kuwa Bwana tu apewe ukuu na utukufu. Alipotimiza kuwateua watoto wake watawala, alisikitika sana kuahamu kuwa wanawe hawakuwa na uwezo kutawala. Alipomwomba Bwana kuhusu uamuzi wa taia kuhitaji mtawala,hapakuwepo na mapendeleo dhidi ya watoto wake. Samweli alitii mwongozo wa Bwana kuwapea watu kile walichohitisha.

Kifungu cha maana kwenye uhai wa Samweli yanajumuisha aliyosema kwa Mfalme Sauli: "Naye Samweli akasema: Je, Bwana huzipenda sadaka za kuteketezwa na dhabihu sawasawa na kutii sauti ya Bwana? Angalia kutii ni bora kuliko dhabihu, na kusikia kuliko mafuta ya beberu"(1 Samweli 15:22). Kulitii Neno la Mungu na lipewe fursa ya kwanza.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Tutajifunza yapi kukota kwa uhai wa Samweli?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries