settings icon
share icon
Swali

Tutajifunza yapi kutoka kwa uhai wa Mtawala Sauli?

Jibu


Sauli mwanzo wake ulikuwa mwema lakini baadaye vitendo vyake visivyo vya utiifu vingekuwa nguzo, uongozi wa utukufu wa Bwana katika wana wa Israel. Ni vipi mtu aliyekuwa karibu sana na Bwana tangu awali kugeuka ghafla na kutoka kwa upendo wa Bwana? Ndivyo tufahamu vile uhai wa Sauli na matendo yake yalivyokosa mwelekeo, tunapaswa kufahamu jambo kumhusu. Mtawala Sauli ndiye nani, na tutajifunza yapi kuhusu uhai wake?

Sauli, katika Kiibrania lilitamkwa kama shaw-ool, lilimaanisha "kuulizwa." Sauli aliyekuwa mtoto wa Kishi katika kabila la Benjamini. Sauli alitoka kwa jamii iliyo tajiri (1 Samweli 9: 1) naye alikuwa mrefu kuliko watu wote, mweusi na mzuri kwa kuonekana. Bibilia inanakiri kuwa "wala katika wana wa Israeli hawakuwako mtu mzuri kuliko yeye; tangu mabega yake kwenda juu" (1 Samweli 9: 2). Ndiye aliyechaguliwa na Bwana ili kuelekeza wana wa Israeli waliokuwa wamesambaratika, jumuia ya makabila waliokuwa hawana mtawala kando na Bwana wala hawakuwa na mfumo maalum wa utawala. Kwa nyakati za shida,watawala waliinuka bali hawakujumuisha ukuu wa makabila ya taifa la Israeli kuwa moja. Muda mrefu kama Sauli hajaanza utawala, kuhani Samweli ndiye aliyekuwa mkuu wa kidini wa Israeli wala si mtawala. Bila shaka, Israeli iliongozwa na viongozi waliothathimini maswala ya kijamii (1 Samweli 8). Hata hivyo, hawakuwa wamejihami katika nyakati za mapambano. Haionekani ukweli kona kuwa Samweli na Sauli waliishi kwa nyakati ngumu. Wafilisti ndio maasidi walioteuliwa wa Israeli, na mapambano yalishuka miongoni mwao mara kwa mara (1 Samweli 4). Watu walimsumbua Samweli kuwachagulia kiongozi kwa kutamani kuwa sawa na nchi zingine zilizowazunguka kwa sababu ya tishio la mashambulizi ya kila mara (1 Samweli 8: 5).

Hata kama matakwa yao ya mtawala hayakumridhisha Samweli, Bwana aliwakubalia. Jamii zilikuwa zimemhasi Bwana kama mtawala wao, wakamkana, na kuabudu sanamu zingine (1 Samweli 8: 6-8). Bwana akamwamuru Samweli kumpaka mtawala mafuta sambamba na matakwa ya watu, zaidi hayo "uwaonye sana na kuwaonyesha desturi ya mfalme atakayewamiliki" (1 Samweli 8: 9). Basi likawa jukumu la Samweli kumchagua mtawala katika miongoni mwa taifa. Sauli akachaguliwa kwa kisiri kuwa mtawala wa kwanza wa taifa lote la Israeli (1 Samweli 10: 1) kama bado hajateuliwa kwa uwazi na Loti (1 Samweli 10: 17-24).

Uongozi wa Sauli katika Israeli uling'oa nanga bila shaka hadi 1010 BC, ila amani haikudumu. Kati ya matendo makuu kwa uhai wa Sauli ulikuwa ni kuwa thabiti kati ya Wafilisti katika Bonde la Ela. Goliathi hapa aliwadhulumu Waisraeli siku 40 hadi pale kijana mchunga kondoo Daudi alimtoa uhai (1 Samweli 17). Kando na tendo hilo la kuogofia na kusitaajabisha, Sauli alisalia kiongozi asiyebingwa katika jeshi. Uzuri wake ulikuwa kwamba uongozi wake uliimarika kupitia ushindi kule Jabesh-Gileadi. Alifanywa mtawala kule GIlgali,kama kipengele katika ushindi wake. (1 Samweli 11: 1-15). Alichukua usukani kutawala nchi kwa sababu ya ushindi mwingi vile sifa zake zilienea hadi zenithi zake. Ingawa,matukio mengi maovu yaliyofuatana, kutoka kwa kutoa saka isiyokubalika (1 Samweli 13: 9-14) ilikuwa chanzo cha kuanguka kwa utawala wake. Kuanguka kwa Sauli kulifululiza aliyoendelea kuangamiza Waamaleki na wanyama wao alivyoamuru Bwana (1 Samweli 15: 3). Kutotii shauri ya Mungu,alionelea kutoangamiza uhai wa mtawala Agagi ikiwemo mifugo aliyoipendelea. Kwa jaribio la kuficha dhambi kwa kumdanganya Samweli, na ivo,kudanganya Mungu (1 Samweli 15). Kutotii kwake ulikuwa tamati, ikiwa Mungu angechukua Roho Wake kutoka kwa Sauli (1 Samweli 16:14). Pengo kati ya Mungu na Sauli ni kati ya yale matendo ya kuhuzunisha kwenye Bibilia.

Vile Sauli angeruhusiwa kuwa mtawala uhai wake wote, aliingiwa na roho mbaya iliyomtesa na kumsababishia mawimbi ya uwazimu (1 Samweli 16: 14-23). Nyakati za mwisho za Sauli zilikuwa za kushangaza maana alistahimili nyakati nyingi za kuteseka. Bila shaka, kijana aliletwa katika kasisi ya mfalme aliyejulikana kama Daudi aliyekuwa wa maana katika kubadilisha taabu iliyomkumba kupitia muziki uliositili heshima ya mfalme kwa kiwango kidogo. Mfalme akamuitikia Daudi kama mmoja wake, ila hya yote yakawa toauti wakati Daudi alikuwa mwanajeshi aliyetambulika katika haki yake. Ila, wimbo uliotajika wakati ule ukawa "Sauli amewaua elfu zake, na Daudi makumi elfu yake" (1 Samweli 18: 7). Sauli alipogundua kuwa Mungu alikuwa pamoja na Daudi, mtawala akatafuta kumuangamiza Daudi kwa kila naasi aliyopata. Daudi alifaulu kujiepusha mara nyingi aliojaribiwa kwa kuhifadhiwa na mtoto wa mtawala, Jonathani, na binti ya mfalme, Michaeli.

Mwishowe katika utawala wa Mfalme Sauli maisha yake yalishusha huduma yake kwa nchi na bahatia zake binafsi. Alitumia wakati, nguvu na kujigharimu Zaidi akijaribu kumuanngamiza Daudi badala ya kutunza ushamiri wa mafanikio yake ya hapo mbeleni, na kwa sababu yake Wafilisti wakatafakari kuwa Waisraeli wangepata ishindi dhidi yao.Wafilsti wakajikusanya dhidi ya Israeli pale Samweli alikata roho. Sauli akashikwa na woga na akapanga kutafiti kuhusu Mungu, bali hakupewa majibu kupitia Urim ama manabii. Hata kama Sauli aliangamiza waganga na mapepo kutoka taifa hilo, Sauli akajikinga na kutafuta mganga kule Endori binafsi. Akamwagiza kumtafuta Samuel. Ikawa kuwa Bwana aliingilia na kumpatanisha Samweli na Sauli kukutana. Samweli akamkumbusha Sauli kuhusu maono ya mbeleni kuwa utawala wake ungenyakuliwa kutoka kwake.Hakukoma kumwarifu Sauli kuwa Wafilisti watashambulia Israeli na Sauli na watoto wake wataangamizwa (1 Samweli 28). Wafilisti walitimiza, na ikawa vivyo,wakavamia Israeli na kuangamiza watoto wa Sauli, akiwemo Yonathani. Sauli alipata majera sana na kuagiza mmiliki wa silaha zake kumuangamiza ndio Wafilisti wasipate kumdhulumu. Kwa waga, mmiliki silaha hakuitikia, ndivyo Sauli akajiangushia silaha yake binasi, ikafuatwa na mmiliki wa silaha aliyetenda vile vile.

Mafunzo matatu tutajifunza kutoka kwa uhai wa Mfalme Sauli. Mosi, mheshimu Mungu na tafuta kutenda matakwa Yake. Tangu uongozi wake ulipoanza, Sauli alikuwa na nafasi murwa ya kuwa mfalme ambaye wafalme wengine wote waliokuja baadaye wangeweza kumrejelea, na kujieka mizani. Kile angeweza kutenda ni kumtafuta Bwana kwa roho yake yote, azitii amri za Mungu zote alizotoa, na kuweka sawa matakwa yake na mapenzi Mola, na ufalme wake ungekuwa wa kumheshimu Mola. Licha ya wengine wengi, Sauli alifuata mkondo tofauti na Kumuasi Mungu. Uasi wake halisi unaonekana pale ambapo Mungu alimwagiza kuwaangamiza Waamaleki wote, ila Sauli akamuhifadhi na kutomuua mfalme na baadhi ya bidhaa zilizobakia baada ya vita. Saulo pia alimuhifadhi Hamani Mgagiti aliyekuwa mwanawe mfalme ambaye baadaye angeazimia kuwaangamiza Wayahudi (tazama kitabu cha Esta). Zaidi ya hayo Sauli aliongeza matatizo yake kwa kumdanganya Samweli kuhusu hilo tukio. Aliwazingizia majeshi kuwa ndio walihifadhi ile mifugo nzuri ili kuzitoa kama dhabihu kwa Mola (1 Samweli 15). Licha ya tukio hili na mengine mengi kuhusu wakati wa utawala wake, yazingatia ukweli kwamba hangeweza kuaminika kuwa atakayetekeleza mapenzi ya Mungu.

La pili tunalojifunza sio kuharibu uwezo tuliojaliwa. Hamna swali kuwa Mtawala Sauli alitumia visivyo uwezo Bwana alimpatia. Majivuno kwa mara kadhaa hutuingia rohoni pale watu wanatuinamia na kututukuza. Wakati fulani, "matibabu ya nyota" yatatuanya kuelewa kuwa tu maana na thamini ya kustahili utukufu. Haya yanapotokea, tunamweka Mungu kando kuwa ni yeye anayethabiti na kutawala kote mwenyewe. Bwana angechagua Sauli kwa maana alikuwa amenyenyekea, ila kwa nyakati unyenyekevu uliingiwa na majivuno na kujipenda iliyoharibu uongozi wake.

Funzo lingine kwetu ni kutawala jinsi Mungu atakavyo sisi kufanya. 1Petro 5: 2-10 hatimaye ni mwelekeo mwema wa kuongoza watu ambao Mungu amewatia mikononi mwetu: "Lichungeni kundi la Mungu lililo kwenu, na kulisimamia, si kwa kulazimishwa bali kwa hiari kama Mungu atakavyo,si kwa kutaka fedha ya aibu, bali kwa moyo.Wala si kama wajifanyao mabwana juu ya mitaa yao bali kwa kujifanya vielelezo kwa lile kundi. Na mkuu atakapodhihirishwa, mtaipokea taji ya utukufu ile isiyokauka. Vivyo hivyo ninyi vijana watiini wazee. Naam ninyi nyote jifungeni unyenyekevu mpate kuhudumiana kwa sababu Mungu huwapinga wenye kiburi lakini huwapa wanyenyekevu neema. Basi nyenyekeeni chini ya mkono wa Mungu ulio hodariili awekweze kwa wakati wake huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu. Mwe na kiasi na kukesha;kwa kuwa mshitaki wenu Ibilisi kama simba angurumaye huzunguka zunguka akitafuta mtu ammeze. Nanyi mpingeni huyo mkiwa thabiti katika imani mkijua ya kuwa mateso yale yale yanatimizwa kwa ndugu zenu walioko duniani. Na MUngu wa neema yote aliyewaita kuingia katika Kristo mkiisha kuteswa kwa muda kidogo yeye mwenyewe atawatengeneza na kuwathibitisha na kuwatia nguvu. "Ni vipi ingekuwa mbadala ikiwa katika uhai wa Sauli angetii amri hizi. Mtawala Sauli hngekuwa na upungufu wa ushauri wa hekima ambao angehitaji. Katika kutotii Mungu na kupuuza mashauri yake ya busara, Sauli alikubalia kuzoroteka wa kiroho wa taifa lake kudidimia Zaidi, kuwaondosha Zaidi kutoka kwa Bwana.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Tutajifunza yapi kutoka kwa uhai wa Mtawala Sauli?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries