settings icon
share icon
Swali

Mathayo alikuwa nani katika Biblia?

Jibu


Mathayo katika Biblia alikuwa mmoja wa wanafunzi wa Yesu. Kitabu cha Injili cha Mathayo, pamoja vingine vya Injili vya Luka, Yohana, na Marko, ni vitabu ambavyo vina mwongozo na vina historia sahihi ya maisha ya Kristo. Injili yake Mathayo ni ndefu zaidi kati ya nne na wasomi wengine wanaamini kuwa ndio ilikuwa kwanza kuandikwa.

Kabla ya Mathayo kuwa mwanafunzi wa Kristo, alikuwa mtoza ushuru katika mji wa Kafarnaumu (Mathayo 9: 9; 10: 3). Luka na Marko humwita Mathayo Lawi, mwana wa Alfayo(Marko 2:14, Luka 5:27). Ingawa Luka na Marko hawajasema wazi kuwa, "Lawi na Mathayo ni mtu mmoja," kwa sababu ya muktadha tunaweza kuona kwamba majina hayo yanatumika kwa mtu mmoja. Simulizi ya Mathayo ya wito wake inalingana hasa na simulizi za wito wa Lawi katika Luka na Marko, kwa lugha na wakati pia. Pia, sio jambo lisilo la kawaida kwa mtu kupewa jina tofauti baada ya kukutana na Mungu. Abramu akawa Abrahamu, Yakobo akawa Israeli, Simoni akawa Petro, na Sauli akawa Paulo. Inawezekana kwamba Mathayo (maanake"zawadi ya Mungu") lilikuwa jina ambalo Yesu alimpa Lawi baada ya uongofu wake.

Watoza ushuru walichukiwa kabisa na utamaduni wao wenyewe kwa sababu walifanya kazi kwa serikali ya Kirumi na kujitajirisha wenyewe kwa kukusanya kodi kutoka kwa watu wao wenyewe-mara nyingi wakikusanya kiasi kikubwa (ona Luka 19: 8). Inawezekana kwamba Mathayo alikuwa tajiri, kwa kuwa Luka anasema kwamba Lawi aliandaa "karamu kubwa ya Yesu" na "umati mkubwa" waliohudhuria (Luka 5:29).

Watoza ushuru kama vile Mathayo walionekana na wasomi wa kidini kama watu wenye dhambi sana, hivyo kwamba hata kushiriki pamoja nao ingeweza kuharibu mara moja sifa ya mtu mzuri (Mathayo 9: 10-11). Wakati Yesu alikuwa akila chakula cha jioni katika nyumba ya Mathayo, pamoja na watoza ushuru wengine na wenye dhambi waliohudhuria, Mafarisayo waliwauliza wanafunzi wa Yesu kuhusu chaguo lake la marafiki. Jibu la Yesu ni mojawapo ya maelezo ya wazi ya moyo wa Mungu na Injili Yake kwa mwanadamu: " Wenye afya hawahitaji tabibu, bali walio wagonjwa.

Sio afya ambao wanahitaji daktari, lakini wagonjwa. . . . sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi. "(Mathayo 9: 12-13). Yesu alikuja kuokoa sio "wema," watu wanaojihesabia wenye haki, bali wale ambao walijua kuwa sio wema-watu ambao walikiri kwamba walihitaji wokovu (tazama Mathayo 5: 3).

Haiwezekani kuokoa mtu anayedai kuwa hahitaji kuokolewa. Wengi wa wafuasi wa Yesu walitoka kwa umasikini, waliokataliwa, wagonjwa, wenye dhambi, wenye uchovu (Mathayo 11:28). Yeye hakuwahukumu watu hao; Aliwasamehe na kuwahimiza. Hukumu kali ya Yesu ilikuwa kwa Mafarisayo, walimu wa Sheria, na waandishi wa Sheria waliojihesabia kuwa wema, wenye kustahili, na bora zaidi kuliko "watoza ushuru na wenye dhambi" waliokuwa karibu nao (Mathayo 9:10; 23: 13-15).

Mathayo alikuwa mmoja wa watoza ushuru ambao Yesu aliwaokoa. Alipoitwa na Yesu, mara moja Mathayo alitoka kwa kibanda chake cha kukusanya kodi na akamfuata Bwana (Mathayo 9: 9). Aliwacha nyuma chanzo cha utajiri wake; aliwacha mahali penye usalama na faraja na kuhusika katika kusafiri, shida, na hatimaye kuuawa; aliwacha maisha yake ya zamani na kukubali maisha mapya na Yesu.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Mathayo alikuwa nani katika Biblia?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries