settings icon
share icon
Swali

Luka alikuwa nani katika Biblia?

Jibu


Machache tu yanajulikana kuhusu Luka, mwandishi wa kitabu cha Luka na Matendo ya mitume katika Biblia. Tunajua kwamba alikuwa tabibu na Mtaifa pekee aliyeandika baadhi ya vitabu vya Agano Jipya. Barua ya Paulo kwa Wakolosai inaonyesha tofauti kati ya Luka na wenzake "watu wa tohara," maanake Wayahudi (Wakolosai 4:11). Luka ndiye mwandishi pekee wa Agano Jipya anayejulikana wazi kama asiye Myahudi.

Luka alikuwa mwandishi wa kitabu cha injili cha Luka na kitabu cha Matendo ya mitume. Luka hajajitaja katika vitabu vyake, lakini Paulo anataja jina lake katika barua tatu. Vitabu vya Luka na Matendo ya mitume vimeelekezwa kwa mtu mmoja, Theofilo (Luka 1: 3; Matendo 1: 1). Hakuna mtu anayejua hasa Theofilo alikuwa nani, lakini tunajua kwamba kusudi la Luka katika kuandika vitabu hivi viwili lilikuwa kwamba Theofilo angejua Yesu kwa hakika na kazi ya Yesu Kristo (Luka 1: 4). Labda Theofilo alikuwa tayari amepokea mafundisho ya misingi ya Kikristo lakini bado hakuwa na msingi imara kabisa katika mafundisho hayo.

Luka alikuwa rafiki wa karibu wa Paulo, ambaye alimtaja kuwa "tabibu mpendwa" (Wakolosai 4:14). Pengine kuvutiwa kwa Luka katika utabibu ndiyo sababu injili ya Luka inatoa maelezo mazuri sana ya matendo ya Yesu ya uponyaji.

Paulo pia anamtaja Luka kama "mfanyakazi mwenzangu" (Filemoni 1:24). Luka alijiunga na Paulo huko Troa huko Asia Ndogo wakati wa safari ya pili ya umisionari wa Paulo (Matendo 16: 6-11). Wasomi wengine wanasema kwamba Luka alikuwa "mtu wa Makedonia" ambaye Paulo alimwona katika ndoto yake (Matendo 16: 9). Luka alisalia Filipi wakati wa safari ya pili ya umishonari (Matendo 17: 1) na kisha kusafiri pamoja na Paulo katika safari ya tatu (Matendo 20: 5). Luka alisafiri pamoja na Paulo kwenye safari yake kwenda Yerusalemu na Roma na alikuwa pamoja naye wakati wa kifungo chake huko (2 Timotheo 4:11). Maelezo wazi ya safari ya Luka na Paulo katika Matendo 27 yanaonyesha kuwa alisafiri sana na alikuwa mwenye ujuzi katika usafiri.

Wasomi wamebainisha kwamba Luka alikuwa na ufahamu bora wa lugha ya Kigiriki. Msamiati wake ni bora zaidi , na mtindo wake mara kwa mara unakaribia ule wa Kigiriki rasmi, kama ilivyoandikwa katika injili yake (Luka 1: 1-4), wakati mwingine inaonekana kuwa Kisemiti (Luka 1: 5-2: 52). Alikuwa na ufahamu wa meli na alipenda sana kurekodi maelezo ya kijiografia. Yote haya yanaonyesha kwamba Luka alikuwa mwenye elimu, mwangalifu, na mwandishi mwangalifu.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Luka alikuwa nani katika Biblia?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries