settings icon
share icon
Swali

Je! Ni kanisa gani ambalo ni la kweli?

Jibu


Je! Ni kanisa gani — yaani, ni dhehebu gani la Ukristo — ambalo ni "kanisa la kweli"? Je! Ni kanisa gani ambalo Mungu anapenda na kuliehensi ambalo alilikufia? Je! Ni kanisa ambalo ni bi-arusi wa Mungu? Jibu ni kwamba hakuna kanisa linaloonekana au dhehebu ambalo ni kanisa la kweli, kwa sababu bi-arusi wa Kristo sio taasisi, lakini badala yake ni shirika la kiroho linaloundwa na wale ambao kwa neema na imani wameletwa katika uhusiano wa karibu, wa dhati na Bwana Yesu Kristo (Waefeso 2: 8-9). Watu hao, haijalishi ni jengo gani, dhehebu, au nchi gani, wanaweza kuwa, wao wanaunda kanisa la kweli.

Katika Biblia, tunaona kwamba kanisa la mtaa (au linaloonekana) sio zaidi ya mkusanyiko wa wanaokiri imani hiyo. Katika barua za Paulo, neno kanisa linatumika kwa njia mbili tofauti. Kunayo mifano mingi ya neno kanisa inayotumiwa kurejelea kundi la wanaojiita waumini ambao hukutana pamoja kila mara (1 Wakorintho 16: 9; 2 Wakorintho 8: 1; 11:28). Tunaona sikitiko la Paulo, katika barua zake, kwa makanisa binafsi katika miji anuwai katika safari yake ya umishonari. Lakini pia anataja kanisa lisiloonekana — chombo cha kiroho ambacho kina ushirika wa karibu na Kristo, karibu sana kama bi-arusi kwa mumewe (Waefeso 5:25, 32), na ambaye Yeye ndiye kichwa cha kiroho (Wakolosai 1: 18; Waefeso 3:21). Kanisa hili linajumuisha kikundi cha watu wasiotajika, na wasiojulikana (Wafilipi 3: 6; 1 Timotheo 3: 5) ambao wote wampata Kristo.

Neno kanisa ni tafsiri ya neno la Kiyunani eklesia, linalomaanisha "kusanyiko lililoitwa." Neno hilo linaelezea kikundi cha watu ambao wameitwa kutoka ulimwenguni na kutengwa kwa ajili ya Bwana, na hutumiwa kila wakati, katika hali yake ya umoja kuelezea kikundi cha watu wote wanaomjua Kristo. Neno eklesia, wakati linawekwa katika hali wingi, linatumika kuelezea vikundi vya waumini wanavyokusanyika pamoja. Cha kufurahisha ni kwamba, neno kanisa halitumiwi kamwe katika Biblia kuelezea jengo au shirika.

Ni rahisi kunaswa na dhana kwamba dhehebu fulani katika Ukristo ndio "kanisa ya kweli," lakini mtazamo huu kuyaelewa Maandiko vipya. Wakati unachagua kanisa la kuhudhuria, ni muhimu kukumbuka kuwa mkusanyiko wa waumini unapaswa kuwa mahali ambapo wale walio wa kanisa la kweli (taasisi ya kiroho) wanahisi wako mahali salama. Hiyo ni kusema, kanisa zuri la mtaa linasingatia Neno la Mungu, likiliheshimu na kulihubiri kwa uaminifu, kuitangaza injili kwa uthabiti, na kuwalisha kondoo na kuwachunga. Kanisa linalofundisha uzushi au kujiingiza katika dhambi hatimaye litakuwa chini sana (au kuanguka kabisa) wale watu ambao ni wa kanisa la kweli – ni wale kondoo wanaoisikia sauti ya Mchungaji na kumfuata (Yohana 10:27).

Washirika wa kanisa mara nyingi wao hufurahia kukubaliana na ushirika kando mwa Yesu Kristo, jinsi vile amefunuliwa katika Neno Lake. Hii ndio inaitwa umoja wa Kikristo. Makosa mengine ya kawaida ni kuamini kuwa umoja wa Kikristo ni jambo la kukubaliana na kila mmoja. Makubaliano ya urahisi kwa sababu ya makubaliano hayasemi ukweli kwa upendo au kutia moyo kila moja kufikia umoja katika Kristo; badala yake, inahimiza waumini kujiepusha na kusema ukweli mchungu. Huwa inaondoa uelewo wa kweli wa Mungu kwa kupendelea umoja wa uwongo unaotegemea upendo usiofaa ambao sio kitu kingine ila ni ubinafsi wa kuruihurusu dhambi ndani ya mtu na kwa wengine.

Kanisa la kweli ndio bi-harusi wa Kristo (Ufunuo 21:2, 9; 22:17) na ndio mwili wa Kristo (Waefeso 4:12; 1 Wakorintho 12:27). Kanisa hilo haliwezi wekeka, elezeka vyema, au kufafanuliwa na kitu chochote mbali na upendo wake kwa Kristo na kujitolea kwake kwa Kristo.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je! Ni kanisa gani ambalo ni la kweli?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries