settings icon
share icon
Swali

Kafiri ni nini? Je, ukairi ni nini?

Jibu


Kutoka kwa mtazamo wa Kikristo, makafiri kwa ujumla hujulikana kama wale ambao hupatikana katika sherehe yoyote ya dini, kitendo, au mazoezi ambayo sio ya Kikristo halisi. Vivyo hivyo, Wayahudi na Waislamu pia hutumia maneno ya makafiri kuelezea wale walio nje ya dini yao. Wengine hufafanua neno ukafiri kama dini yoyote nje ya ubuddhi, Uhindu, Uyahudi, na Ukristo; ambapo wengine wanasema kwamba kafiri ni mtu yeyote asiye na dini kabisa.

Ukafiri unaweza kurejelea ushirikina au ibada ya zaidi ya mungu mmoja, kama vile Roma ya kale. kairi pia anafikiriwa kuwa ni mmoja ambaye, kwa sehemu kubwa, hana dini na ujihusisha katika radhi za kidunia na vitu vya kimwili; mtu ambaye anajitokeza katika raha ya kimwili; mwenye ni muhedonisiti au mwenye kujitegemea. Mwingine, neno la kisasa zaidi ni kuiga ukafiri, ambalo linamaanisha baadhi ya aina za kisasa za kikafiri kama vile Wicca, Druidry, na Gwyddon.

Hivi vitendo vya kisasa vya "ukafiri" ni kweli sawa na wenzao wa zamani kwa kuwa wanategemea sana uhamasishaji wa hisia- kujifurahisha kimwili na kufuata furaha na starehe kwa kuepuka kila kitu kingine. Katika nyakati za kale, sherehe za ngono zilikuwa sehemu kubwa ya dini za kikafiri. Agano la Kale inarejelea hizi dini zilizopotoshwa katika vifungu kama vile Kumbukumbu la Torati 23:17, Amosi 2: 7-8, na Isaya 57: 7-8.

Ingawa wao ni wengi na tofauti katika vitendo na imani zao, makafiri wanashikilia kwenye imani sawa. Kwa mfano:
• Dunia ya kimwili ni mahali pazuri, ambayo inapaswa kupendezwa na kila mtu.
• Kila mtu anahesabiwa kuwa sehemu ya Dunia hii ya kiasili.
• Uungu unajionyesha katika kila nyanja ya ulimwengu.
• Kila kilicho hai, mwanadamu na mnyama, ni kwa mnajiri wa Uungu. Kwa hivyo, wote ni miungu ya kiume na ya kike.
• Dini nyingi za kikafiri hazina magwiji au messia.
• Mafundisho yanasimamiwa na jukumu la mtu mwenyewe.
• Mzunguko wa jua na mwanga ni muhimu katika ibada ya kikafiri.

Aina yoyote ya ukafiri ni mafundisho ya uongo. Paulo alielezea uongo huu wa kweli katika barua yake kwa waumini huko Roma (Warumi 1: 22-27). Watu ambao Paulo aliwaelezea walikuwa wa kidunia na wapenda vitu vya kimwili, kuabudu viumbe vingine badala ya Muumba. Waliabudu miti, wanyama, na miamba, kwenda hadi sasa kwa kutumia vibaya miili yao katika vitendo vya kijinsia vibaya ili kuvutia katika tamaa zao. Paulo kisha anaendelea kutuambia kwa nini walifanya hivyo na matokeo ya mwisho:

"Zaidi ya hayo, kwa kuwa hawakufikiri kuwa ni jambo la thamani la kuhifdhi ujuzi wa Mungu, aliwapeana kwa akili iliyopotoka, kufanya mambo ambayo haifai kufanyika" (Warumi 1:28).

Licha ya mawazo ya kawaida, waabudu wengi wa kikafiri wanasema hawamwamini Shetani. Hata hivyo, hakuna swali kwamba Shetani ni chanzo kikuu cha ushawishi na udhibiti wao. Ingawa watakataa, wanamdharau katika vitendo vya kidunia na vya kimwili. Paulo anatuambia waziwazi jinsi Shetani anavyofanya kazi katika maisha ya watu wasio na Mungu, kwa nguvu zake, ishara zake, udanganyifu wake, na uongo wake:

"Kuja kwa mtu asiye na sheria kutakuwa sawa na kazi ya Shetani iliyoonyeshwa kwa kila aina ya miujiza ya ishara, ishara na maajabu, na katika aina yoyote ya uovu inayowadanganya wanaoangamia. Wanaangamia kwa sababu walikataa kupenda ukweli na hivyo kuokolewa. Kwa sababu hii Mungu anawapelekea udanganyifu wenye nguvu ili waweze kuamini uongo na hivyo wote watahukumiwa ambao hawakuamini ukweli bali wamefurahia uovu "(2 Wathesalonike 2: 9-12).

Kwamba Shetani yu hai na vizuri anaonyeshwa nguvu zake katika vitendo hivi vya kikafiri. Hii haikuwa wazi tu katika nyakati za kanisa la karne ya kwanza, lakini pia katika ulimwengu wa kisasa. Kwa waumini waaminifu wanaomjua Bwana, ibada ya kikafiri inaonekana kuwa ni nguvu na udanganyifu wa mkuu wa ulimwengu huu, ambaye ni Shetani (1 Yohana 5:19), ambaye "huzunguka kama simba anayenguruma akitafuta mtu kula "(1 Petro 5: 8). Kwa hivyo, ukafiri unapaswa kuepukwa.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Kafiri ni nini? Je, ukairi ni nini?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries