settings icon
share icon
Swali

Injili za Kiroho ni gani?

Jibu


Injili za kiroho ni maandishi ya awali ya "Kikristo". Baada ya karne ya kwanza ya Ukristo, migawanyiko miwili ya msingi ilianzishwa-Wakristo wa kidini na Wakiroho. Wakristo wa kidini walishikilia vitabu ambavyo sasa tunavyo katika Biblia na kile ambacho leo kinachukuliwa kuwa theolojia ya kidini. Wakristo wa kiroho, kama wanaweza kwa kweli kuelezwa kama Wakristo, wanao mtazamo tofauti wa Biblia, wa Yesu Kristo, wa wokovu, na karibu na mafundisho mengine yote ya Kikristo. Hata hivyo, hawakuwa na maandishi yoyote ya mitume ili kutoa uhalali wa imani zao.

Ndiyo sababu na jinsi injili za kiroho zilivyoundwa. Wanaroho walidanganya kwa kuandika majina ya Wakristo maarufu kwa maandishi yao, kama Injili ya Tomasi, Injili ya Filipo, Injili ya Maria, n.k. Ugunduzi wa maktaba ya Nag Hammadi kusini mwa Misri mwaka wa 1945 ulikuwa ni ugunduzi mkubwa wa Injili za kiroho. Vitabu hivi vya kiroho mara nyingi vinatajwa kama vile "vitabu vilivyopotea vya Biblia."

Tunapaswa kujibuje kwa Injili za kiroho? Lazima wengine wao au wote wawe katika Biblia? La, hawapaswi. Kwanza, kama ilivyoelezwa hapo juu, Injili za kiroho ni udanganyifu, udanganyifu ulioandikwa kwa majina ya mitume ili kuwapa uhalali kanisa la kwanza. Kwa kushangaza, baba za kanisa la kwanza walikuwa karibu kwa kutambua Injili za kiroho zilipendekeza mafundisho ya uongo. Kuna tofauti nyingi sana kati ya Injili za kiroho na Injili za kweli za Mathayo, Marko, Luka, na Yohana. Injili za Gnostic zinaweza kuwa chanzo kizuri cha kujifunza mafundisho ya Kikristo ya mapema, lakini inapaswa kukataliwa kabisa kama sio ndani ya Biblia na sio kuwakilisha imani halisi ya Kikristo.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Injili za Kiroho ni gani?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries