settings icon
share icon
Swali

Je, ni makosa kumkasirikia Mungu?

Jibu


Kuwa na hasira kwa Mungu ni kitu ambacho watu wengi, wote waumini na wasioamini, wameshindana nalo kwa wakati wote. Wakati jambo la kusikitisha linatokea katika maisha yetu, tunamuuliza Mungu swali, "Kwa nini?" Kwa sababu ni jibu la kawaida. Tunachomuuliza kwa hakika, ingawa, sio mengi "Kwa nini, Mungu?" Kama "Kwa nini mimi, Mungu?" Jibu hili linaonyesha makosa mawili katika kufikiri kwetu. Kwanza, kama waumini tunafanya kazi chini ya hisia kwamba maisha lazima iwe rahisi, na kwamba Mungu lazima azue msiba kutukumba. Wakati hafanyi, tunamkasirikia. Pili, wakati hatujui kiwango cha uhuru wa Mungu, tunapoteza ujasiri katika uwezo Wake wa kudhibiti hali, watu wengine, na jinsi wanavyotuathiri sisi. Kisha tunakasiririka Mungu kwa sababu anaonekana kuwa amepoteza udhibiti wa ulimwengu na hasa udhibiti wa maisha yetu. Wakati tunapoteza imani katika uhuru wa Mungu, ni kwa sababu mwili wetu wenye udhaifu unakabiliana na kuchanganyikiwa kwetu na ukosefu wetu wa udhibiti juu ya matukio. Wakati mambo mazuri yatatokea, mara nyingi tunayahusisha na matarajio yetu na mafanikio yetu. Wakati mambo mabaya yanapotokea, hata hivyo, tuna haraka ya kumlaumu Mungu, na tunamkasirikia kwa sababu hakuzuia hayo, ambayo inaonyesha kosa la kwanza katika mawazo yetu-kwamba tunastahili kuepuka hali mbaya.

Maafa huleta nyumbani ukweli kwamba sisi hatuna wajibu. Sisi sote tunafikiria kwa wakati mmoja au mwingine kwamba tunaweza kudhibiti matokeo ya hali, lakini kwa kweli ni Mungu ambaye ndiye anayehusika na viumbe vyake vyote. Kila kitu kinachotokea husababishwa na au kuruhusiwa na Mungu. Si sruji huanguka chini wala nywele kutoka kichwa changu bila Mungu kujua kuhusu hilo (Mathayo 10: 29-31). Tunaweza kulalamika, kasirika, na kumulaamu Mungu kwa yale yanatokea. Lakini ikiwa tutamtumaini na kukuza machungu na maumivu Yatu kwake, tukikubali dhambi ya kiburi ya kujaribu kulazimisha mapenzi yetu juu ya Yake, anaweza kutupa utulivu na nguvu zake ili kutuwesesha kupitia hali yoyote ngumu (1 Wakorintho 10: 13). Waumini wengi katika Yesu Kristo wanaweza shuhudia ukweli huo. Tunaweza mkasirikia Mungu kwa sababu nyingi, hivyo sote tunapaswa kukubali kwa wakati fulani kwamba kuna vitu ambavyo hatuwezi kudhibiti au hata kuelewa na akili zetu za mwisho.

Uelewa wetu wa uhuru wa Mungu katika hali zote lazima uambatane na ufahamu wetu wa vigezo vyake vingine: upendo, huruma, unyenyekevu, wema, ukweli, haki, na utakatifu. Tunapoona shida zetu kwa njia ya ukweli wa Neno la Mungu-ambayo inatuambia kuwa Mungu wetu mwenye upendo na mtakatifu anafanya kazi pamoja kwa ajili yetu nzuri (Warumi 8:28), na kwamba ana mpango kamili na kusudi kwetu ambayo haiwezi kuharibiwa (Isaya 14:24, 46: 9-10) — tunaanza kuona matatizo yetu kwa nuru tofauti. Pia tunajua kutoka kwa Maandiko kwamba maisha haya haitakuwa kamwe ya raha na furaha kila siku. Badala yake, Ayubu hutukumbusha kwamba "Lakini mwanadamu huzaliwa ilia pate mashaka, kama cheche za moto zirukavyo juu." (Ayubu 5: 7), na kwamba maisha ni mafupi na "yamejaa shida" (Ayubu 14: 1). Kwa sababu tunakuja kwa Kristo kwa ajili ya wokovu kutoka kwa dhambi haimaanishi tumehakikishiwa maisha bila matatizo. Kwa kweli, Yesu alisema, "Katika ulimwengu huu utakuwa na taabu," bali kwamba "ameshinda ulimwengu" (Yohana 16:33), na kutuwezesha kuwa na amani ndani, licha ya mawimbi yanayotusunguka (Yohana 14:27).

Jambo moja la uhakika: hasira isiyofaa ni dhambi (Wagalatia 5:20; Waefeso 4: 26-27, 31; Wakolosai 3: 8). Hasira isiyo ya kimungu ni kushindwa kwa kibinafsi, inampa shetani kuwa na nguvu katika maisha yetu, na inaweza kuharibu furaha yetu na amani ikiwa tunatashikilia kwa hilo. Kushikilia hasira yetu itawawezesha uchungu na chuki kuongezeka ndani ya mioyo yetu. Tunapaswa kukiri kwa Bwana, na kisha katika msamaha Wake, tunaweza achilia hisia hizo kwake. Lazima tuende mbele ya Bwana kwa sala mara kwa mara katika huzuni, hasira, na maumivu yetu. Biblia inatuambia katika 2 Samweli 12: 15-23 kwamba Daudi alienda mbele ya kiti cha neema kwa niaba ya mtoto wake mgonjwa, kwa kufunga, kulia, na kumwombea aishi. Wakati mtoto alipokufa, Daudi akasimama na kumsujudia Bwana na kisha akawaambia watumishi wake kwamba alijua ambapo mtoto wake alikuwa na kwamba siku moja angekuwa pamoja naye mbele ya Mungu. Daudi alimlilia Mungu wakati wa ugonjwa wa mtoto, na baadaye akainama mbele yake katika ibada. Huo ni ushuhuda wa ajabu. Mungu anajua nyoyo zetu, na hauna maana kujificha jinsi tunavyohisi, kwa hivyo kuzungumza naye juu yake ni mojawapo ya njia bora za kushughulikia huzuni zetu. Ikiwa tutafanya hivyo kwa unyenyekevu, tukamwagilia mioyo yetu kwake, Yeye atafanya kazi kupitia kwetu, na katika mchakato huo, atatufanya zaidi kama Yeye.

Chini ya msingi ni tunaweza kumwamini Mungu kwa kila kitu, maisha yetu na maisha ya wapendwa wetu? Bila shaka tunaweza! Mungu wetu ni mwenye huruma, amejaa neema na upendo, na kama wanafunzi wa Kristo tunaweza kumwamini Yeye kwa vitu vyote. Wakati msiba unatukumba, tunajua Mungu anaweza kuutumia kutuleta karibu naye na kusidisha Imani yetu, kutuleta kwa ukomavu na ukamilivu (Zaburi 34:18; Yakobo 1:2-4). Kisha, tunaweza kuwa ushuhuda wa utulivu kwa wengine (2 Wakotintho 1: 3-5). Kwamba ni rahisi kusema kuliko kutenda, ata hivyo. Inaiaji kujitolea kwetu wa kila siku kwa uwezo wetu kwake,usomaji wa Imani wa vigezo vyake vile tunona katika neon la Bwana, maombi mengi, na kisha kuyatekeleza yale tunayosoma katika hali zetu. Kwa kufanya hivyo, Imani yetu itakua na kukomaa, kufanya rahisi kuamini kwake ili atuweseshe kuepuka msiba unaofuata ambao ungetendeka.

Kwa hivyo, kujibu swali moja kwa moja, ndio, ni mbaya kumkasirikia Mungu. Hasira kwa Mungu ni kwa sababu kukosa uwezo wa kumwamini ata wakati hatuelewi chenye anafanya. Hasira kwa Mungu mwanzoni umwambia Mungu kwamba amefanya mbaya, chenye hajaawai. Je, Mungu anaelewa wakati tumekasirika au kuchanganyikiwa nay eye? Ndio, anajua nyoyo zetu na anajua vile maisha ni ngumu na yenye machungu katika duniani. Je, hilo litaifanya kweli kumkaasirikia Mungu? Kwa hakika hapana. Badaala ya kumkasirikia Mungu tunasitahili kuachilia mioyo yetu kwake kwa maombi kisha kumwamini kuwa atadhibiti na ako na mpango kamili.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je, ni makosa kumkasirikia Mungu?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries