settings icon
share icon
Swali

Hadithi ya Biblia ya Uumbaji ipi?

Jibu


Hadithi ya msingi ya uumbaji inapatikana katika Mwanzo 1 na 2, na akaunti ya bustani ya Edeni katika sura ya 3. Mwanzo 1 huanza kabla ya kuwepo kwa chochote ila Mungu mwenyewe. Kwa kuwa hii ndio kesi, hakuna kitu kama wakati kabra ya "muda wa kihistoria". Ufunuo wa Mungu mwenyewe na mapenzi yake kwa wanadamu ni mwanzo. Katika mwanzo huu, Mungu aliumba kila kitu katika ulimwengu katika siku sita halisi za saa 24. Hii inajumuisha miili yote ya mbinguni (ikiwa ni pamoja na nyota na sayari), pamoja na kila kitu duniani. Huku hali ya utatu wa Mungu sio wazi katika akaunti ya Mwanzo, Mungu hufunua "sisi" ndani ya Uungu (Mwanzo 1:26). Roho anahusika katika uumbaji (Mwanzo 1: 2) kama vile Kristo (Yohana 1: 1-3; Wakolosai 1: 15-17).

Katika siku sita za Uumbaji, Mungu aliumba ulimwengu na dunia (siku ya 1), wingu na anga (siku 2), ardhi kavu na maisha yote ya mimea (siku 3), nyota na miili ya mbinguni ikiwa ni pamoja na jua na mwezi (siku 4), ndege na viumbe vya maji (siku ya 5), na wanyama wote na mtu (siku 6). Mwanadamu ni maalum zaidi ya viumbe wengine wote kwa sababu yeye huzaa mfano wa Mungu na ana jukumu la kusimamia na kuijaza na dunia. Uumbaji wote ulikamilishwa kwa siku sita katika safu yake yote na uzuri wa ajabu. Siku halisi ya sita, saa 24 hazina muda wa kutenganisha siku. Mungu alitangaza kwamba uumbaji wake ulikuwa mzuri sana. Mwanzo 2 huona ukamilishaji kwa kazi ya Mungu na kutoa maelezo ya kina kuhusu uumbaji wa mwanadamu.

Siku ya saba imewekwa na Mungu kupumzika. Hii si kwa sababu Mungu alikuwa amechoka, lakini aliacha kazi yake ya uumbaji. Hii inaweka mfano wa kuchukua siku moja kwa saba kwa mapumziko na kuhesabu idadi ya siku katika wiki bado inatumiwa hii leo. Kuweka Sabato itakuwa alama ya kutofautisha watu waliochaguliwa na Mungu (Kutoka 20: 8-11.)

Baada ya hayo Mwanzo inachunguza uumbaji wa mwanadamu. Kifungu hiki sio tukio la pili ya uumbaji, wala siyo kinyume na Mwanzo 1. Taarifa hiyo inachukua hatua mbali na ripoti ya mwelekeo mmoja kumwelekeza msomaji kwa kazi ya Mungu kuhusu mwanadamu. Mungu aliumba mwanadamu kutoka kwa udongo wa dunia alikua imekwisha umbwa hapo awali. Baada ya kumuumba mwanadamu, Mungu alipumua uhai ndani yake. Ukweli kwamba Mungu alichagua kuumba mwanadamu kwa njia hii inaonyesha utunzaji wake mkubwa katika mchakato huu. Mungu baadaye aliweka mwanadamu wa kwanza, Adamu, mahali maalum, bustani ya Edeni. Edeni ilikuwa nzuri na yenye manufaa. Adamu alikuwa karibu na kila kitu alichohitaji ikiwa ni pamoja na chakula na kazi ya uzalishaji. Hata hivyo, Mungu hakuwa amaemalizana na mwanadamu.

Mungu alimsaidia Adamu kuona umuhimu wake wa mwenzi kwa kumruhusu kuviangalia upya viumbe wengine wote na kuwapa majina. Adamu alielewa kwamba alihitaji mwenzi. Mungu alimfanya Adamu kulala na kisha akamfanya Hawa kwa umakini kama vile alivyomuumba Adamu. Hawa aliumbwa kutoka kwa ubavu wa Adamu. Adamu alipomwona, alielewa kwamba alikuwa pekee. Alikuwa mwenzake, msaidizi wake, na mwili wa mwili wake. Mungu aliwaumba Adamu na Hawa katika smfano wake (Mwanzo 1:27). Kifungu hiki kinaiweka familia kuwa chanzo cha msingi cha jamii (Mwanzo 1:24; Mathayo 19: 5-6.) Kama taasisi iliyowekwa na Mungu, ndoa inapaswa iwe kati ya mme mmoja na mwanamke mmoja. Adamu na Hawa waliumbwa katika hali ya kutojua hatia (Mwanzo 1:25) na hawakuwa wamefanya dhambi yoyote. Walifurahia ushirika wao na Mungu huko Edeni. Sehemu ya uhusiano ilikuwa kuingizwa kwa utawala mmoja rahisi. Adamu na Hawa walikatazwa kula kutoka kwa mti mmoja na ni mti mmoja tu katika bustani nzima (Mwanzo 1:17).

Wakati fulani Hawa alijaribiwa na yule nyoka kula kwenye mti huu mmoja, kitu ambacho alifanya. Adamu pia alikula kutokana na mti uliopigwa marufuku. Adamu na Hawa walifanya dhambi dhidi ya Mungu na walipoteza haki yao (Mwanzo 2: 8-12). Dhambi ilileta matokeo. Mungu alilaani nyoka kutambaa milele juu ya ardhi na kuchukiwa na wanadamu. Mungu alimlaani Hawa kwa maumivu wakati wa kujifungua na kupigana na mumewe, na alimlaani Adamu kwa shida na shida katika kazi zake (Mwanzo 3: 14-19). Sehemu ya matokeo ya dhambi yao ni pamoja na Adamu na Hawa kufukuzwa kutoka bustani (Mwanzo 3: 22-24.) Lakini pia katika matokeo hayo kuna ujumbe wa matumaini. Kutajwa kwa kwanza kwa ujio wa Masihi kunapatikana katika Mwanzo 3:15. Anakuja kuponda nyoka (Shetani), lakini si kabla ya Shetani kumchuzunisha msalabani. Hata katikati ya dhambi na matokeo yake mazuri, Mungu anajionyesha Mwenyewe kuwa Mungu wa neema na huruma na upendo.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Hadithi ya Biblia ya Uumbaji ipi?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries