settings icon
share icon
Swali

Biblia inasemaje kuhusu matatizo ya familia?

Jibu


Matatizo ya familia sio jambo jipya. Katika ulimwengu ulioanguka, wale ambao tunapaswa kupenda zaidi-familia zetu-mara nyingi huwa ndio tunapigana nao. Biblia haisifu dhambi, na inarekodi matatizo kadhaa ya familia, kwa kuanzia na kulaumiana kwa Adamu, na mkewe kama lengo (Mwanzo 3:12). Ushindani wa ndugu unajitokeza katika hadithi za Kaini na Abeli, Yakobo na Esau, na Yusufu na ndugu zake. Wivu kati ya wake-moja ya matokeo mabaya ya mitara-inapatikana katika hadithi za Hana, na Leah na Raeli. Eli na Samweli walishughulika na watoto waliokuwa wamepotoka. Yonathani alikuwa karibu kuuawa na baba yake, Sauli. Daudi alikuwa amevunjika moyo kwa sababu ya uasi wa mwanawe Absalomu. Hosea alipata matatizo ya ndoa. Katika kesi hizi, mahusiano yaliharibiwa na dhambi.

Biblia ina mengi ya kusema juu ya mahusiano, ikiwa ni pamoja na mienendo ya familia. Taasisi ya kwanza ambayo Mungu aliyoundwa ili kuingiliana na mwanadamu ilikuwa familia (Mwanzo 2: 22-24). Aliumba mke kwa Adamu na akajiunga nao katika ndoa. Akirejelea tukio hili, baadaye Yesu alisema, "Basi aliowaunganisha Mungu, mwanadamu asiwatenganishe" (Mathayo 19: 6). Mpango wa Mungu ulikuwa kwamba mwanaume mmoja na mwanamke mmoja kubaki katika ndoa mpaka mmoja wao atakapofariki. Anataka kubariki muungano huo na watoto watakapolelewa "katika adabu na maonyo ya Bwana." (Waefeso 6: 4; tazama pia Zaburi 127: 3). Shida nyingi za familia zinajitokeza tunapopinga uumbaji na mpango wa Mungu, kwa mfano mitara, uzinzi, na talaka husababisha matatizo yote kwa sababu hukiuka mpango wa awali wa Mungu.

Biblia inatoa maagizo ya wazi juu ya jinsi wanafamilia wanapaswa kutimiana. Mpango wa Mungu ni kwamba waume wawapende wake zao kwa namna ile ile ambayo Kristo anapenda kanisa lake (Waefeso 5:25, 33). Wanawake wanapaswa kuwaheshimu waume zao na kutii uongozi wao (Waefeso 5: 22-24, 33, 1 Petro 3: 1). Watoto wanapaswa kutii wazazi wao (Waefeso 6: 1-4; Kutoka 20:12). Ni matatizo magani mengi ya familia ambayo yataweza kutatuliwa ikiwa waume, wake, na watoto watafuata sheria hizo za msingi?

Timotheo wa kwanza 5: 8 inasema kwamba familia yapaswa kutunza jamaa zao. Yesu alikuwa na maneno makali kwa wale walisusia wajibu wao wa kifedha kwa wazazi wao wazee kwa kudai walipa fedha zao hekaluni (Mathayo 15: 5-6).

The key to harmony in families is not one we naturally want to apply. Ephesians 5:21 says to "submit to one another out of reverence for Christ." Submission is in direct opposition to our flesh's desire to rule and have its way. We defend our rights, champion our causes, defend our opinions, and assert our own agendas whenever possible. God's way is to crucify our flesh (Galatians 5:24; Romans 6:11) and submit to the needs and wishes of others whenever we can. Jesus is our model for that kind of submission to God's will. First Peter 2:23 says, "When they hurled their insults at him, he did not retaliate; when he suffered, he made no threats. Instead, he entrusted himself to him who judges justly."

Cha msingi katika maelewano katika familia sio jambo ambaayo tunataka kutekeleza. Waefeso 5:21 inasema "hali mnanyenyekeana katika kicho cha Kristo."Unyenyekevu unapinga tamaa za mwili wetu na nia yake kujitawala. Tunatetea haki zetu, tunatetea matendo yetu, hutetea maoni yetu, na tunatetea ajenda zetu wakati wowote iwezekanavyo. Njia ya Mungu ni kusulubisha mwili wetu (Wagalatia 5:24; Warumi 6:11) na kutimiza mahitaji na matakwa ya wengine wakati wowote tunapoweza. Yesu ni mfano wetu kwa aina hiyo ya utii kwa mapenzi ya Mungu.Petro wa kwanza 2:23 inasema, "Yeye alipotukanwa, hakurudisha matukano; alipoteswa, hakuogofya; bali alijikabidhi kwake yeye ahukumuye kwa haki."

Matatizo mengi ya familia yanaweza kupunguzwa kama sisi wote tulifuata maelekezo yaliyopatikana katika Wafilipi 2: 3-4: "Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake. Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine.

Usifanye chochote kutokana na tamaa ya ubinafsi au kujifurahisha. Badala yake, kwa unyenyekevu unathamini wengine juu yenu wenyewe, wala msijiangalie maslahi yenu wenyewe bali kila mmoja wenu kwa maslahi ya wengine." Tunapopata roho ya unyenyekevu na kuwatendea wengine kama Yesu anavyowatendea, tutaweza kutatua matatizo mengi ya uhusiano katika familia zetu.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Biblia inasemaje kuhusu matatizo ya familia?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries