settings icon
share icon
Swali

Ninawezaje kupata dhamiri safi?

Jibu


Dhamiri inaweza kufafanuliwa kama "hisia ya ndani ambayo hufanya kama mwongozo wa haki au uovu wa tabia ya mtu." Kwa wale wenye mtazamo wa kibiblia, dhamiri ni sehemu ya nafsi ya binadamu ambayo ni kama Mungu (Mwanzo 3:22). Wale ambao hawamwamini Mungu wana wakati mgumu kuelezea kuwepo kwa dhamiri ya kibinadamu. Mageuzi hayawezi kueleza kipengele hiki cha roho ya binadamu, ambayo haiwezi kuelezewa na fikira ya "kujaribu kuishi".

Dhamiri ya mwanadamu iliamka wakati Adamu na Hawa walikosa kutii amri ya Mungu na kula kutoka mti wa ujuzi wa mema na mabaya (Mwanzo 3:6). Kabla ya hapo, walikuwa wamejua tu mema. Neno la kujua katika Mwanzo 3:5 ni neno lile lile lililotumika mahali pengine kuelezea urafiki wa kijinsia (Mwanzo 4:17; 1 Samweli 1:19). Tunapochagua "kujua" uovu kwa uzoefu wa ndani, dhamiri zetu zinakiukwa na usumbufu wa kihisia huchukua hatamu. Ikiwa tunakubali Mungu au la, tuliumbwa kuwa na ushirika na Muumba wetu. Tunapofanya makosa, tunaona kwamba sisi tuko kinyume na madhumuni yetu yaliyotengenezwa, na hisia hiyo inafadhaika kwa undani.

Alikuwa Mungu ambaye Adamu na Hawa walikuwa wamekosea; bado Mungu Mwenyewe alitoa suluhisho la dhamiri zao zilizokiukwa. Alichinja mnyama asiye na hatia ili kufunika uchi wao (Mwanzo 3:21). Hii ilikuwa kutabiri kusudi la mpango wa Mungu wa kufunika dhambi ya watu wote.

Wanadamu wamejaribu vitu mbalimbali kufuta dhamiri zao, kutoka kwa kazi za fadhila hadi kujihasiri. Historia imejaa mifano ya jitihada za wanadamu za kuridhisha dhamiri yake, lakini hakuna yenye inafanya kazi. Hivyo mara nyingi anarudi kwa njia zingine za kuzama nje sauti hiyo ya ndani ambayo humtangaza kuwa na hatia. Kuzoea tabia mbaya, uasherati, unyanyasaji, na uroho mara nyingi ina mizizi imara katika udongo wenye rutuba wa dhamiri ya hatia.

Hata hivyo, kwa kuwa dhambi zote hatimaye ni dhambi dhidi ya Mungu, Mungu pekee anaweza kukomboa dhamiri iliyokiukwa. Kama vile alivyofanya katika Bustani ya Edeni, Mungu hutupa kifuniko kwa njia ya dhabihu ya kitu kamilifu na kisicho na hatia (Kutoka 12:5; Mambo ya Walawi 9:3; 1 Petro 1:18-19). Mungu alimtuma Mwanawe mwenyewe, Yesu, ulimwenguni kwa kusudi la kuwa dhabihu la mwisho, kamilifu kwa ajili ya dhambi za ulimwengu wote (Yohana 3:16, 1 Yohana 2:2). Wakati Yesu alienda msalabani, alijichukua juu yake Mwenye kila dhambi tutaweza kufanya. Kila dhamiri iliyokiukwa, mawazo yote ya dhambi, na kila tendo ovu liliwekwa juu yake (1 Petro 2:24). Ghadhabu yote ya haki ambayo Mungu anayo kwa ajili ya dhambi zetu ilimwagwa juu ya Mwanawe mwenyewe (Isaya 53:6; Yohana 3:36). Kama vile mnyama asiye na hatia alitolewa dhabihu ili kufunika dhambi ya Adamu, hivyo Mwana mkamilifu alitolewa kwa ajili ya kufunika zetu. Mungu Mwenyewe huchagua kutufanya tuwe wa haki na Yeye na kututangaza kusamehewa.

Tunaweza kuwa na dhamiri zetu kutakaswa wakati tunaleta dhambi zetu, kushindwa kwetu, na majaribio yetu ya kusikitisha ya kuridhisha Mungu kwa mguu wa msalaba. Upatanisho wa Kristo unasamehe dhambi zetu na hutakasa dhamiri yetu (Waebrania 10:22). Tunakubali kutokuwa na uwezo wa kutakasa mioyo yetu wenyewe na kumwomba Yeye atufanyie. Tunaamini kwamba kifo cha Yesu na ufufuo wake ni wa kutosha kulipa bei tunayodaiwa na Mungu. Tunapokubali malipo ya Yesu kwa ajili ya dhambi yetu binafsi, Mungu anaahidi kutupa dhambi zetu mbali na sisi "kama mashariki ilivyo mbali na magharibi" (Zaburi 103:12, tazama Waebrania 8:12).

Katika Kristo, tumeachiliwa kutoka kwenye msongo wa dhambi. Tumewekwa huru kufuatilia haki na usafi na kuwa wanaume na wanawake Mungu aliumba sisi kuwa (Warumi 6:18). Kama wafuasi wa Kristo, tutaendelea kufanya dhambi ya mara kwa mara. Lakini, hata hivyo, Mungu hututolea njia ili kuwa na dhamiri zetu kufanywa safi. 1 Yohana 1:9 inasema kwamba, "tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote." Mara nyingi, kwa ungamo hilo kunakuja ujuzi kwamba tunapaswa kufanya mambo sawa na wale tumekosea. Tunaweza kuchukua hatua hiyo na watu ambao tumewaumiza, kujua kwamba Mungu tayari ametusamehe.

Dhamiri zetu zinaweza kubaki safi vile tunaungama dhambi zetu daima kwa Mungu na kuaamini kwamba damu ya Yesu inatosha kutufanya tuwe wa haki na Yeye. Tunaendelea "kutafuta kwanza ufalme wa Mungu na haki yake" (Mathayo 6:33). Tunatumaini kwamba, licha ya kutokamilika kwetu, Mungu anatufurahia sisi na katika kazi yake ya kubadilisha katika maisha yetu (Wafilipi 2:13; Warumi 8:29). Yesu alisema, "Basi Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kweli" (Yohana 8:36). Tunaishi na dhamiri safi kwa kukataa kugaagaa katika kushindwa ambazo Mungu amesamehe. Tunasimama hakika katika ahadi yake kwamba, "Mungu akiwapo upande wetu, ni nani aliye juu yetu?" (Warumi 8:31).

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Ninawezaje kupata dhamiri safi?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries