settings icon
share icon
Swali

Kuhusu msamaha, je kuna tofauti kati ya dhambi ya kukusudia na dhambi ya kutojua?

Jibu


Ingawa Mungu huweka tofauti kati ya wale wanaofanya dhambi kwa kutojua na wale wanaofanya dhambi kwa hiari (Hesabu 15: 27-31), toba ni lazima kila mara kupokea msamaha (Marko 1:15; Matendo 2:38; Matendo 26:18). Toba hasa ni kubadili mtazamo wa mtu kuhusu Mungu na inaambatana na kuwa na imani katika Kristo (Matendo 3:19; 20:21; 26:20). Bila toba hakutakuwa na msamaha. Yesu akasema, "La, nawaambia; msipotubu, ninyi nyote mtaangamia "(Luka 13: 3, tazama 17: 3-4; 2 Petro 3: 9).

Kutenda dhambi kwa hiari ni kuwa na kiburi na kujigamba katika kumhasi Mungu (Zaburi 19:13; Waebrania 10:26). dhambi za kukusudia huleta hukumu ya Mungu, mapema au baadaye, bali pia dhambi za kutojua hazijaachwa kuhukumiwa: "Kwa hiyvo nawaambieni haya, na kuyasisitiza kwa Bwana, kwamba msipate kuishi kama watu wa mataifa mengine, kwa ubatili wa mawazo yao. Wako gizani katika ufahamu wao na kutengwa na maisha ya Mungu kwa sababu ya kutojua kulio ndani yao kutokana na kuifanya mioyo yao ngumu. Kwa kuwa walipoteza uelewa wote, wamejitoa wenyewe juu ya utamaduni ili waweze kujiingiza katika kila aina ya uchafu, na wamejawa na tamaa "(Waefeso 4: 17-19; tazama pia Matendo 3: 17-19; Matendo 17:30 -31). Msamaha hupo kwa wote, lakini tunaiacha kwa neema ya Mwenyezi Mungu ili kumfanya mkosaji kutubu kwa kweli ili apate kusamehewa (Waefeso 2: 4).

Wale wanaomkataa Yesu na Injili yake kwa kutojua lazima wamkubali Yeye kwa toba ili wapate msamaha wa dhambi zao. Yesu alifanya wazi wazi hivi: "Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima. Hakuna mtu anakuja kwa Baba isipokuwa kwa njia yangu "(Yohana 14: 6). Haijalishi kama mtu anakosa njia kwa sababu ya kutojua au kwa sababu ya uasi wa makusudi-bado amekosa njia.

Watu sio kuwa hawajui kama wanavyoweza kudai, hata hivyo. Hakuna mtu anayeweza kuwa hamjui Mungu kabisa, na hakuna mtu mwenye udhuru wa kuishi katika kutotii. Mtume Paulo alisema, " Kwa maana ghadhabu ya Mungu imedhihirishwa kutoka mbinguni juu ya uasi wote na uovu wa wanadamu waipingao kweli kwa uovu.

Kwa kuwa mambo ya Mungu yanayojulikana yamekuwa dhahiri ndani yao, kwa maana Mungu aliwadhihirishia.

Kwa sababu mambo yake yasiyoonekana tangu kuumbwa ulimwengu yanaonekana, na kufahamika kwa kazi zake; yaani, uweza wake wa milele na Uungu wake; hata wasiwe na udhuru;

"(Warumi 1: 18-20).

Ingawa tunaweza kutenda dhambi wakati mwingine kwa kutojua, tunaweza kuwa na uhakika wa msamaha wa Mungu daima. Mtume Paulo ni mfano wa kweli wa ukweli huu: " ingawa hapo kwanza nalikuwa mtukanaji, mwenye kuudhi watu, mwenye jeuri, lakini nalipata rehema kwa kuwa nalitenda hivyo kwa ujinga, na kwa kutokuwa na imani." (1 Timotheo 1:13). Kwa maana wale waliokwisha kuyakimbia machafu ya dunia kwa kumjua Bwana na Mwokozi Yesu Kristo, kama wakinaswa tena na kushindwa, hali yao ya mwisho imekuwa mbaya kuliko ile ya kwanza. Maana ingekuwa heri kwao kama wasingaliijua njia ya haki, kuliko kuijua, kisha kuiacha ile amri takatifu waliyopewa.

"(2 Petro 2: 20-21).

Yohana anatueleza wazi juu ya suala la msamaha: " Tukisema kwamba hatuna dhambi, twajidanganya wenyewe, wala kweli haimo mwetu. Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote.

"(1 Yohana 1: 8-9).

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Kuhusu msamaha, je kuna tofauti kati ya dhambi ya kukusudia na dhambi ya kutojua?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries