settings icon
share icon
Swali

Je, kuna hatari gani / matokeo yapi ya dhambi isiyokiriwa?

Jibu


Kwanza Yohana 1: 9 inasema, "Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote." Aya hii imeandikwa kwa Wakristo na msingi wake ni kwa neno ikiwa. Mungu hutoa msamaha kamili kwa kila dhambi watoto wake wanafanya ikiwa tunazikiri kwake. Neno kukiri linamaanisha kukubaliana na Mungu kuhusu jinsi dhambi zetu zilivyo mbaya. Kutubu, au kuokoka, ni sehemu ya kukiri. Kwa wale ambao hawajawahi kusamehewa na damu ya Yesu, dhambi zote hazijakiriwa na hazijasamehewa. Adhabu ya milele inawasubiri wale wanaokataa kutubu dhambi zao na kukubali sadaka ya Yesu kwa ajili yazo (2 Wathesalonike 1: 8-9; Yohana 3: 15-18). Walakini nini kuhusu Mkristo mwenye dhambi isiyokiriwa?

Kwa mujibu wa Maandiko, dhambi zetu zote zililipwa wakati tulikubali dhabihu ya Yesu kwa niaba yetu. Wakorintho wa pili 5:21 inasema, "Yeye asiyejua dhambi alimfanya kuwa dhambi kwa ajili yetu, ili sisi tupate kuwa haki ya Mungu katika Yeye." Tunapofanya kubadilishana kwa Mungu msalabani, Mungu huchagua kutuona kama wenye haki. Sio haki yetu bali ni haki ya Kristo ambayo Mungu anaona (Tito 3: 5). Anabadili mtazamo na sisi: rekodi yetu iliyoharibiwa ya rekodi yake kamili. Tuna idhini kamili na kukubalika kwa Mungu tangia wakati huo kuendelea.

Lakini nini kinatokea tunapofanya dhambi baada ya kupokea rekodi hiyo kamili? Fikiria kusimama karibu na dirisha la kusini kwenye siku ya baridi msimu wa baridi. Hewa ni baridi, lakini jua linaangaza kupitia dirisha. Linaanza kukupasha joto, nawe hutazama katika mwanga wake. Kisha utavuta pasia kuifunga. Mara moja, joto linaisha. Je, ni kwa sababu jua limeacha kuangaza? La, ni kwa sababu kuna kitu kilikuja kati yako na jua. Wakati unafungua pasia, jua linaweza kukupasha joto tena. Lakini ni juu yako. Kikwazo ki ndani ya nyumba, wala sio nje.

Dhambi isiyokiriwa inafanya kazi kama vile pasia. Mungu hufurahia watoto Wake (Zaburi 37:23; Warumi 8: 38-39). Anatazamia kutubariki, kushiriki na sisi, na kutunyeshea idhini yake juu yetu (Zaburi 84:11, 115: 13; 1 Samweli 2:30). Anataka tutazamie katika joto la tabasamu Yake. Lakini tunapochagua dhambi, tunajenga kizuizi kati yetu na Baba yetu Mtakatifu. Tunaivuta pasia ya ushirika na Yeye na kuanza kuhisi kibaridi cha upweke wa kiroho. Mara nyingi, kwa hasira tunamlaumu Mungu kwa kutuacha, wakati kwa kweli sisi ndio tumemwacha. Tunapofanya kukataa kutubu, tutaadhibiwa na Baba yetu mwenye upendo (Waebrania 12: 7-11). Adabu ya Bwana inaweza kuwa kali, hata kusababisha kifo wakati moyo umekuwa mgumu kiasi cha kutobadilika (1 Wakorintho 11:30, 1 Yohana 5:16). Mungu anatamani ushirika wa kurejeshwa hata zaidi kuliko sisi (Isaya 65: 2, 66:13; Mathayo 23:37; Yoeli 2: 12-13). Anatufuata, hutuadhibu, na anatupenda hata katika dhambi zetu (Warumi 5: 8). LakiniYeye huacha mapenzi yetu imara. Lazima tufungue pasia kwa kukiri na kutubu.

Ikiwa, kama watoto wa Mungu, tunachagua kubaki katika dhambi zetu, basi tunachagua matokeo ambayo huenda na uchaguzi huo. Ushirika uliovunjika na kukosa kukua kiroho kunatokea. Hata hivyo, wale wanaoendelea katika dhambi wanahitaji kuchunguza tena uhusiano wao wa kweli na Mungu (2 Wakorintho 13: 5). Maandiko ni dhahiri kwamba wale wanaomjua Mungu hawaendelei na maisha ya dhambi zisizokiriwa (1 Yohana 2: 3-6; 3: 7-10). Tamaa ya utakatifu ni ishara ya wale wanaomjua Mungu. Kumjua Mungu ni kumpenda (Mathayo 22: 37-38). Kumpenda ni kutamani kumpendeza (Yohana 14:15). Dhambi zisizokiriwa zinapata njia ya kumpendeza, hivyo mwana wa kweli wa Mungu anataka kuzikiri, kuzibadilisha, na kurejesha ushirika na Mungu.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je, kuna hatari gani / matokeo yapi ya dhambi isiyokiriwa?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries