settings icon
share icon
Swali

Ni kwa nini damu na maji yalitoka kwa mwili wa Yesu wakati alidungwa mkuki?

Jibu


Kichapo cha Warumi ambacho Yesu alikivumilia kabla ya kusulubiwa kilikuwa cha fimbo 39, labda kulikuwa na zingine nyingi (Marko 15:15; Yohana 19:1). Mjeledi ambao ulitumika ulioitwa fulagumi ulikuwa na nyusi za ngozi ilisongwa pamoja na chuma za mviringo na vyuma kali kali vikiwa ndani mwa nyusi. Hivyo vyuma vya mviringo vilikuwa viongeze uzito kwa mjeledi, ndio uweze kusababisha ukali kwa mwadhiriwa alipopigwa. Vipande vya mifupa vilitumika kukata mwili. Kichapo kilipoendelea ndivyo kukatwa kuliendelea hadi sehemu ya ndani ya mwadhiriwa ikawa nje. Kuchapwa huku kulikuwa kubaya kwamba wakati mwingine mwadhiriwa hangeuistahimili na kungoja kusulubiwa.

Wale ambao walichapwa mara nyingi walipatwa na mshutuko wa moyo, msemo uliotumika kwa kuwa na kiwango cha chini cha damu mwilini. Kwa njia nyingine, mtu angepoteza damu nyingi sana angepatwa na mshutuko. Na matokeo ya haya ni:
1) Moyo ungekazana na kusambaza damu ambayo haikuwemo.
2) Mwadhiriwa angezimia au kusirai kwa kuwa na kiwango cha chini cha damu.
3) Figo zingekwama na hivyo hazingeweza kuweka maji ya mwili.
4) Mtu angekuwa na kiu kubwa sana kwa vile mwili ulihitaji maji yaliyopotea.

Kunao Ushahidi wa kutoka Maandiko kuwa Yesu alipatwa na mshutuko kwa sababu ya kupigwa. Yesu alipokuwa akiubeba msalaba wake kwenda Golgotha (Yohana 19:17), alisirai na mtu aitwaye Simioni alilazimishwa iadha kuubeba au kumsaidia kubeba katika kipindi cha safari kilichobaki hadi mlimani (Mathayo 27:32-33; Marko 15:21-22; Luka 23:36). Kusirai huku kunaonyesha kuwa Yesu alikuwa na nyusi choto ya chini. Ashirio linginge ni kuwa Yesu aliadhirika tokana na mshutuko ni kuwa alisema kuwa alikuwa na kiu akiwa ameangikiwa mtini (Yohana 19:28), ikidhihirisha kuwa mwili wake uliitaji maji.

Kabla ya kifo chaek, mpigo wa moyo wa haraka uliosabishwa na mshutuko pia ulisababisha maji ya mwili kujikusanya karibu na moyo na pavu. Mkusanyiko huu wa maji karibu na utando unaozunguka moyo huitwa mshutuko unaotokana na umwagikaji wa maji, na maji yanajikusanya kando ya pavu huitwa mshutuko wa pavu. In inaelezea ni kwa nini, baada ya Yesu kufa askari wa Kirumi alimdunga mkuki upavuni mwake, huku akidunga pavu zote mbili na moyo, damu na maji yalitoka upavuni mwake vile Yohana ameandika katika Injili yake (Yohana 19:34).

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Ni kwa nini damu na maji yalitoka kwa mwili wa Yesu wakati alidungwa mkuki?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries