settings icon
share icon
Swali

Nini maana ya damu ya Kristo?

Jibu


Maneno "damu ya Kristo" imetumiwa mara kadhaa katika Agano Jipya na ni maonyesho ya kifo cha dhabihu na kazi kamili ya Yesu ya kulipa kwa niaba yetu. Marejeleo ya damu ya Mwokozi ni pamoja na ukweli kwamba Yeye alimwaga damu kwa msalaba, lakini kwa kiasi kikubwa kwamba Alimwaga na kufa kwa ajili ya wenye dhambi. Damu ya Kristo ina uwezo wa kulipa kwa idadi isiyo na mwisho ya dhambi zilizofanywa na idadi isiyo na mwisho ya watu kwa miaka yote, na wote ambao imani yao hukaa katika damu hiyo wataokolewa.

Ukweli wa damu ya Kristo kama njia ya upatanisho wa dhambi ina asili yake katika Sheria ya Musa. Mara moja kwa mwaka, kuhani alikuwa akitoa sadaka ya damu ya wanyama kwa madhabahu ya hekalu kwa ajili ya dhambi za watu. "Na katika Torati karibu vitu vyote husafishwa kwa damu, na pasipo kumwaga damu hakuna ondoleo." (Waebrania 9:22). Lakini hii ilikuwa sadaka ya damu ambayo ilikuwa imepungua kwa ufanisi wake, ndiyo sababu ilitolewa tena na tena. Hii ilikuwa onyesho la "mara moja ya mwisho" dhabihu ambayo Yesu aliitoa juu ya msalaba (Waebrania 7:27). Mara tu dhabihu hiyo ilitolewa, hakukuwa na haja ya damu ya ng'ombe na mbuzi.

Damu ya Kristo ni msingi wa Agano Jipya. Usiku uliopita kabla ya kwenda msalabani, Yesu aliwapa wanafunzi wake kikombe cha divai na kusema, "kikombe hiki ni agano jipya katika damu yangu, iliyomwagika kwa ajili yenu" (Luka 22:20). Kumwawa kwa divai katika kikombe ilishiria damu ya Kristo ambayo ingemwawa kwa ajili ya wote ambao wangeweza kumwamini Yeye.Alipomwaga damu yake msalabani, Yesu aliondoa mahitaji ya Agano la Kale ya kuendelea kutoa sadaka ya wanyama. Damu yao haikutosha kufunika dhambi za watu, ila kwa misingi ya muda mfupi, kwa sababu dhambi dhidi ya Mungu mtakatifu na asiye na mwisho inahitaji dhabihu takatifu na isiyo na mwisho. "Lakini katika dhabihu hizo liko kumbukumbu la dhambi kila mwaka "(Waebrania 10: 3). Ili hali damu ya ng'ombe na mbuzi ilikuwa "kumbusho" la dhambi, "damu ya thamani ya Kristo, mwana-kondoo asiye na hatia au kasoro "(1 Petro 1: 19), ililipa kikamilifu deni la dhambi tunazo kwa Mungu, na hatuhitaji tena dhabihu kwa dhambi. Yesu alisema, "Imekwisha" alipokuwa akifa, na alikuwa akimaanisha -kazi yote ya ukombozi ilikamilishwa milele, "tumepata ukombozi wa milele" kwetu (Waebrania 9:12).

Sio tu damu ya Kristo kuwakomboa waumini kutoka kwa dhambi na adhabu ya milele, lakini "basi si zaidi damu yake Kristo, ambaye kwamba kwa Roho wa milele alijitoa nafsi yake kwa Mungu kuwa sadaka isiyo na mawaa. Itawasafisha dhamiri zenu na matendo mafu, mpate kumwabudu Mungu aliye hai" (Waebrania 9:14). Hii inamaanisha kwamba sio tu sisi tuko huru kutoka dhabihu ambazo "hazina maana" kupata wokovu, lakini tuko huru kutokana na kutegemea kazi zisizo na maana na zisizozalisha za mwili kufurahisha Mungu. Kwa sababu damu ya Kristo imetukomboa, sasa sisi ni uumbaji viumbe vibya katika Kristo (2 Wakorintho 5:17), na kwa damu yake sisi tuko huru kutokana na dhambi ili kumtumikia Mungu aliye hai, kumtukuza Yeye, na kumfurahia milele.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Nini maana ya damu ya Kristo?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries