settings icon
share icon
Swali

Biblia inasema nini juu ya uvumilivu?

Jibu


Biblia ina mengi ya kusema juu ya uvumilivu katika mazingira mbalimbali. Kwa wazi, Maandiko yanafundisha kwamba wale ambao "wanashinda" na kuhimili katika imani watapata uzima wa milele (Ufunuo 2: 7). Ukweli huu vile vile umeelezwa katika Wakolosai 1:23 ambapo tunaona kwamba watu watakuwa watakatifu, wasio na hatia na bila aibu "mkidumu tu katika ile imani, hali mmewekwa juu ya msingi, mkawa imara; msipogeuzwa na kuliacha tumaini la Injili mliyosikia habari zake." Kwa hivyo Wakristo wote wanapaswa kukubaliana kwamba wale ambao hatimaye wataokolewa ni wale ambao wanaendelea kuvumilia na kuendelea kuiamini injili.

Kuna maoni mawili tofauti juu ya suala la uvumilivu wa watakatifu kati ya Wakristo. Jambo la kwanza ni mtazamo wa Arminian kwamba inawezekana kwa Wakristo wa kweli kugeuka mbali na Mungu na wasivumilie. Hii ni sawa na dhana ya wokovu ambayo ina "uhuru wa mtu" katikati yake. Ni mantiki thabiti kwamba, kama "uhuru wa kuchagua" wa mtu ni sababu ya kuamua wokovu wake, basi pia inawezekana kwa mtu huyo baadaye kuchagua kumkataa Mungu na hivyo kupoteza wokovu wake.

Hata hivyo, Biblia inafundisha waziwazi kwamba "tumezaliwa mara ya pili" na Roho Mtakatifu, ambayo husababisha kuja kwetu kwa imani katika Kristo. Wote ambao "wamezaliwa tena" wana usalama wa milele na wataendelea. Mafundisho ya uvumilivu wa watakatifu imeanzishwa katika ahadi ya kwamba "yeye aliyeanza kazi njema mioyoni mwenu ataimaliza hata siku ya Kristo Yesu" (Wafilipi 1: 6) na tamko la Yesu kuwa "ye yote ajaye kwangu sitamtupa nje kamwe "na" katika wote alionipa nisimpoteze hata mmoja" (Yohana 6:37, 39).

Zaidi ya dhana ya uvumilivu kwa mjibu wa wokovu, kuna maagizo ya kibiblia ya kuhimili katika maisha ya Kikristo. Katika barua zake za uchungaji kwa Timotheo, mtume Paulo anakumbusha mchungaji mdogo "Jitunze nafsi yako, na mafundisho yako. Dumu katika mambo hayo; maana kwa kufanya hivyo utajiokoa nafsi yako na wale wakusikiao pia"(1 Timotheo 4:16). Tabia ya Timotheo ilikuwa ni ya mtu mwenye kumcha Mungu, na mafundisho yake yalikuwa mazuri na ya maandiko. Paulo alimwomba awaangalie kwa karibu na kuyahimili kwa sababu-na hii ni onyo kwa Wakristo wote-uvumilivu katika maisha ya kiungu na kuamini ukweli daima huongoza kwa uongofu wa kweli (Yohana 8:31; Warumi 2: 7).

Himizo zaidi la kuhimili katika maisha ya Kikristo linatoka kwa Yakobo, ambaye anatuonya kuwa " Lakini iweni watendaji wa neno, wala si wasikiaji tu, hali mkijidanganya nafsi zenu. Kwa sababu mtu akiwa ni msikiaji wa neno tu, wala si mtendaji, mtu huyo ni kama mtu anayejiangalia uso wake katika kioo. Maana hujiangalia, kisha huenda zake, mara akasahau jinsi alivyo" (Yakobo 1: 22-24). Hisia hapa ni kwamba Mkristo ambaye huendeleza katika utauwa na taaluma za kiroho atabarikiwa katika tendo la kuvumilia. Tunapovumilia Zaidi katika maisha ya Kikristo, Mungu atatoa baraka zake kwetu, na hivyo kutuwezesha kuendelea kuhimili. Mtunga-zaburi hutukumbusha kwamba kuna mshahara mkubwa katika kuvumilia katika maisha ya Kikristo. Kwa kuzingatia amri za Mungu, kuna "malipo makubwa" kwa roho zetu (Zaburi 19:11), amani ya akili, dhamiri safi, na kushuhuda ulimwengu kwa ufasaha zaidi kuliko maneno mengi.

Yakobo pia anatuhimiza kuvulia "katika majaribu" kwa sababu wale wanaofanya hivyo watabarikiwa na watapata "taji ya uzima" ambayo Mungu ameahidi (Yakobo 1:12). Kama vile muumini wa kweli atahakikishiwa usalama kabisa katika wokovu wake, imani yake pia itahimili mateso, magonjwa, mateso, na majaribu mengine ya maisha yanayowapata waumini wote. Ikiwa tunataka kuishi maisha ya kiungu katika Kristo, tutateseka (2 Timotheo 3:12), lakini waaminifu watahimili, wakiwa na nguvu za Roho Mtakatifu ambaye ni dhamana ya wokovu wetu na atutupa "nguvu" hadi mwisho, "ambaye atawathibitisha hata mwisho, ili msilaumiwe siku ile ya Bwana wetu Yesu Kristo" (1 Wakorintho 1: 8).

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Biblia inasema nini juu ya uvumilivu?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries