settings icon
share icon
Swali

Biblia inasema nini kuhusu uadilifu?

Jibu


Katika Agano la Kale, neno la Kiebrania linalotafsiriwa "uadilifu" linamaanisha "hali ya kukosa uovu, kuwa na ukamilifu, uaminifu, uadilifu, ukamilifu." Uaminifu katika Agano Jipya ina maana "uaminifu na kuzingatia mfano wa kazi nzuri. "

Yesu ni mfano kamili wa mtu wa uadilifu. Baada ya kubatizwa, alikwenda jangwani na kufunga kwa siku arobaini (mchana na usiku) wakati ambapo Shetani alikuja kwake kwa udhaifu wake kujaribu na kuvunja uadilifu wake na kumdhuru. Yesu alikuwa mwanadamu kabisa na Mungu kabisa wakati huo huo, naye akajaribiwa kila njia, lakini hakufanya dhambi (Waebrania 4:15); hiyo ndiyo ufafanuzi wa uadilifu. Yesu peke yake hakuwa na hatia, alikuwa kamilifu, kweli kabisa, na daima anaonyesha mfano wa matendo mema.

Wakristo wanashauriwa kuwa kama Yesu. Katika Kristo, sisi ni viumbe vipya tunaweza kuzingatiwa kuwa wasio na hatia mbele za Mungu (2 Wakorintho 5:17, 21; Waefeso 1: 4-8). Katika Kristo, sisi pia tuna Roho Mtakatifu aliyekaa ndani yetu, kututakasa na kutufanya zaidi kama Yesu (Warumi 8:29, 2 Wakorintho 3:18). Tunajitahidi pia "utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka. Kwa maana ndiye Mungu atendaye kazi ndani yenu, kutaka kwenu na kutenda kwenu, kwa kulitimiza kusudi lake jema." (Wafilipi 2: 12-13). Ni kwa uwezo wa Mungu kwamba tunazidi kuwa watu wa uadilifu. Tunahimizwa kumtii Mungu na, kwa kufanya hivyo, kuwa watu wa maadili na uaminifu usioingilika. Wakristo wanapaswa kufuata ukweli na wanaofanya kazi njema.

"Uadilifu" katika ulimwengu wetu leo unamaanisha kuwa na maadili yasiyotingizika. Wakristo wanapaswa kuwa wale ambao hawawezi kufungwa au kuathiriwa kwa sababu tunamtumikia Mungu badala ya wanadamu (Wakolosai 3:17, 23; Matendo 5:29). Tunapaswa kuwa watu ambao tunatenda tunachosema. (Mathayo 5:27; Yakobo 5:12). Tunapaswa kuwawapenda wale walio karibu nasi kwa maneno na matendo (1 Yohana 3: 17-18; Yakobo 2: 17-18; Waefeso 4:29). Tunastahili kumwamini Mungu na kwa hivyo kumfuata kwa njia zetu zote (Yohana 6:19; 15: 1-17). Maisha yetu yanapaswa kuzingatia imani yetu kwa Mungu na kuamini kuwa njia zake ni bora (Mithali 3: 5-6).

Kuishi kwa uadilifu katika ulimwengu ambako wafisadi wanaonekana kuwa na kibali, bila kutaja vita yetu na asili yetu ya dhambi, ni changamoto. Kwanza Petro 3: 13-18 inatoa faraja hii: "Naye ni nani atakayewadhuru, mkiwa wenye juhudi katika mema? Lakini mjapoteswa kwa sababu ya haki mna heri. Msiogope kutisha kwao, wala msifadhaike; bali mtakaseni Kristo Bwana mioyoni mwenu. Mwe tayari siku zote kumjibu kila mtu awaulizaye habari za tumaini lililo ndani yenu; lakini kwa upole na kwa hofu. Nanyi mwe na dhamiri njema, ili katika neno lile mnalosingiziwa, watahayarishwe wale wautukanao mwenendo wenu mwema katika Kristo. Maana ni afadhali kuteswa kwa kutenda mema, ikiwa ndiyo mapenzi ya Mungu, kuliko kwa kutenda mabaya. Kwa maana Kristo naye aliteswa mara moja kwa ajili ya dhambi, mwenye haki kwa ajili yao wasio haki,ili atulete kwa Mungu; mwili wake akauawa, bali roho yake akahuishwa." Kuishi kwa uadilifu ni kufuata mfano wa Kristo. Na tunaweza tu kuishi na uadilifu wa kweli kwa nguvu zake, ambazo Yeye huwapa kwa hiari na kwa uhuru kwa wote ambao ni wake (Yohana 16:33, Wafilipi 1: 6; Waefeso 1: 13-14).

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Biblia inasema nini kuhusu uadilifu?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries