settings icon
share icon
Swali

Je, Biblia inasema nini kuhusu mafadhaiko?

Jibu


Kamusi inafafanua mafadhaiko kama "majaribu ya kimwili, ya akili, au ya kihisia au mvutano." Mafadhaiko fulani ni muhimu na hata nzuri-kama vile majaribu ya kimwili tunayoweka kwa misuli yetu ili kuifanya kuwa na nguvu. Lakini tunapozungumzia "mafadhaiko," mara nyingi tunataja matatizo au machafuko kupita kiasi au kinyume ya akili au ya kihisia. Wakati "mafadhaiko" hayajatajwa hasa katika Biblia, Maandiko hayazungumzii mambo kama vile dukuduku, wasiwasi, na shida-mambo ambayo mara nyingi tunashirikisha na mafadhaiko-na hutupa majibu wazi juu ya jinsi tunapaswa kushughulika nayo.

Kila mtu anaumia kutokana na mafadhaiko wakati mmoja au mwingine. Jinsi tunavyoishughulikia kwa kawaida hutegemea kwa kiasi kikubwa juu ya sisi ni nani. Kwa baadhi, matatizo ya kihisia husababisha ugonjwa wa kimwili. Wengine wanaweza kuwa wa kuzalisha zaidi. Kwa upande mwingine, watu wengine wanaofadhaika wamefungwa kiakili na kihisia. Na, bila shaka, kuna aina mbalimbali ya majibu. Mafadhaiko ni uzoefu wa kawaida wa kibinadamu, hasa katika ulimwengu ambako mahitaji ya wakati wetu na mazingatio huonekana kuwa ya kudumu. Kazi zetu, afya, familia, marafiki, na hata shughuli za huduma zinaweza kutushinda. Suluhisho la mwisho kwa mafadhaiko ni kujitolea maisha yetu kwa Mungu na kutafuta hekima Yake juu ya vipaumbele pamoja na kuwezesha Kwake kufanya mambo ambayo anatuitia Yeye. Daima hutupa ya kutosha, hivyo hatuhitaji kushindwa na mafadhaiko.

Sababu moja ya kawaida ya mafadhaiko ni ya kifedha. Tunafadhaika juu ya pesa kwa sababu hatuonekani kuhisi kamwe kuwa na za kutosha. Tuna wasiwasi juu ya kuwa na uwezo wa kulipia bili zetu zote, wengi huishi hukopa ili kulipa madeni. Au tunaangamizwa na vitu vya kimwili, na hivyo, tunafadhaika juu ya kudumisha mtindo wa maisha yetu. Baadhi wanafadhaika juu ya fedha kwa sababu hawaamini Mungu kutoa mahitaji ya msingi ya maisha. Lakini Yesu akasema, "Kwa sababu hiyo nawaambieni, Msisumbukie maisha yenu, mle nini au mnywe nini; wala miili yenu, mvae nini. Maisha je! Si Zaidi ya chakula, na mwili Zaidi ya mavazi? ...Ni yupi kwenu ambaye akijisumbua aweza kujiongeza kimo chake hata mkono mmoja?" (Mathayo 6:25, 27). Ni kweli kwamba tunatakiwa kuwa wasimamizi wazuri wa fedha na kukimu familia zetu (1 Timotheo 5:8), lakini hatupaswi kamwe kusahau kuwa Mungu ndiye Mtoaji wetu wa mwisho. Ikiwa sisi ni Wake, hatuhitaji kuogopa kwamba atatuacha. Kwa upande mwingine, kuna wale ambao mafadhaiko yao ya kifedha husababishwa zaidi na tamaa ya kimwili kuliko ilivyo kwa mahitaji ya kweli. Tamaa za kimwili huongoza kwa mafadhaiko yasioepukika kwa sababu, tunapotafuta vitu vya dunia, tumeanguka kwa "udanganyifu wa utajiri" (Marko 4:19), uongo kwamba vitu hivyo huondoa mafadhaiko na kusababisha furaha, kuridhika, na raha. Hazifanyi.

Tunaweza pia kujipata wenyewe tunafadhaika wakati tunapokabiliwa shida au majaribio. Yakobo 1:2-4 ushauri, "Ndugu zangu, hesabuni ya kuwa ni furaha tupu, mkiangukia katika majaribu mbalimbali; mkifahamu ya kuwa kujaribiwa kwa Imani yenu huleta saburi. Saburi na iwe na kazi kamilifu, mpate kuwa wakamilifu na watimilifu bila kupungukiwa na neno." Tunakabiliwa na shida, tunaweza shindwa na mafadhaiko, au tunaweza kuitazama kama njia ambayo Mungu anaweza kuimarisha imani yetu na kuunda tabia yetu (Warumi 5:3-5; 8:28-29). Tunapoelekeza mtazamo wetu juu ya Mungu, tunapata faraja katika huzuni zetu na nguvu ya kuvumilia (2 Wakorintho 1:3-4; 12:9-10).

Haijalishi aina ya mafadhaiko katika maisha yetu, hatua ya mwanzo ya kukabiliana nayo ni Yesu Kristo. Yesu anatutia moyo mkubwa katika Yohana 14:1: "Msifadhaike mioyoni mwenu; mwamini Mungu, amini pia ndani yangu." Tunamhitaji sana katika maisha yetu. Tunamhitaji Yeye kwa sababu Yeye ndiye pekee ambaye anaweza kutupa nguvu ya kuvumiliana na shida katika maisha yetu. Kumwamini haimaanishi kwamba tutakuwa na maisha yasio na shida au kwamba hatuwezi kuhisi kushindwa na mafadhaiko katika maisha yetu. Ina maana tu kuwa maisha bila Yesu Kristo hufanya kuvumiliana na mafadhaiko kazi isiyowezekana na ya kudhoofisha mara nyingi.

Kuamini kunasababisha kuamini. Mithali 3:5-6 inatuambia "Mtumaini BWANA kwa moyo wako wote, wala usizitegemee akili zako mwenyewe; katika njia zako zote mkiri yeye, naye atayanyosha mapito yako." Kutegemea "akili zetu" mara nyingi inamaanisha kuchukua njia za dunia za kupunguza mafadhaiko-vitu kama vile pombe au madawa ya kulevya au burudani bila akili. Badala yake, tunapaswa kuamini Neno Lake kama mwongozo wetu wa mwisho kwa maisha yenye upungufu wa mafadhaiko. Daudi anasema, "Nalimtafuta BWANA akanijibu, akaniponya na hofu zangu zote" (Zaburi 34:4). Daudi alijua kwamba kwa kumtafuta Bwana na kushiriki matatizo yake na Yeye kwamba labda angepata kibali na Yeye. Bwana pia akamjibu na kumtuliza.

Labda hakuna kifungu katika Maandiko bora kinachoonyesha jinsi ya kushughulikia mafadhaiko kuliko Wafilipi 4:6-7: "Msijisumbue kwa neno lolote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu. Na Amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu." Bwana anatuambia tusiwe na wasiwasi juu ya kitu cho chote, lakini badala yake tugeuze kila kitu kwake Yeye kwa sala. Kuleta mizigo na shida zetu kwa Mungu mtakatifu na mwenye haki kila siku itapunguza au kuondoa mafadhaiko katika maisha yetu. Zaburi 55:22 inatuambia tumtwike mizigo yetu yote kwa sababu Yeye atatuhimili na kamwe hatatuacha (tazama pia 1 Petro 5:6-7). Yesu Kristo hutoa amani ikiwa tutakuja Kwake na wahaka na wasiwasi wetu. "Amani nawaachieni; amani yangu nawapa; niwapavyo mimi sivyo kama ulimwengu utoavyo. Msifadhaike mioyoni mwenu, wala msiwe na woga" (Yohana 14:27).

Mafadhaiko ya kila aina ni sehemu ya asili ya maisha (Ayubu 5:7, 14:1, 1 Petro 4:12, 1 Wakorintho 10:13). Lakini jinsi tunavyoishughulikia ni juu yetu. Ikiwa tunachagua kujaribu kufanya hivyo peke yetu, hatuwezi kupata tulizo la kudumu. Njia pekee ambayo tunaweza kukabiliana na mafadhaiko mara kwa mara na kwa ufanisi ni pamoja na Yesu Kristo. Kwanza, lazima tuamini Kwake. Pili, tunahitaji kumtumaini na kumtii Yeye. Tunapaswa kumwamini Yeye kufanya yaliyo sawa kwa sababu njia zake ni bora kwetu daima. Uasi na dhambi zinaweza kuleta mafadhaiko na kutukata mbali na njia pekee ya amani na furaha. Kwa kutii amri Zake tunavuna baraka za kuridhisha kweli kutoka kwa Mungu mwenye upendo. Hatimaye, tunahitaji kutafuta amani Yake kila siku kwa kujaza mawazo yetu na Neno Lake, kuinua vitu vyote Kwake katika sala, na kukaa kwa miguu Yake kwa kustahi sana na unyenyekevu. Ni kwa neema Yake tu, huruma na upendo kwamba mafadhaiko katika maisha yetu yanaweza kuthibitiwa.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je, Biblia inasema nini kuhusu mafadhaiko?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries