settings icon
share icon
Swali

Biblia inasema nini kuhusu kuzeeka/kukua mzee?

Jibu


Biblia inaonyesha kukua mzee kama sehemu ya kawaida, asili ya maisha katika ulimwengu huu. Kuna heshima inayohusika katika mchakato wa kuzeeka kwa sababu kukua mzee kwa kawaida huambatana na hekima na uzoefu. "Kichwa chenye mvi ni taji ya utukufu, kama kikionekana katika njia ya haki"(Mithali 16:31; tazama pia Mithali 20:29). Mungu anataka sisi kukumbuka kwamba maisha ni mafupi (Yakobo 4:14) na kwamba uzuri wa ujana utakwenda hivi karibuni (Mithali 31:30, 1 Petro 1:24).

Hatimaye, swali la kukua mzee haliwezi kutenganishwa na swali la maana ya maisha na dhana ya urithi tutakaoacha. Katika kitabu cha Mhubiri, Sulemani hutoa uangalifu wa busara juu ya kuzeeka na masuala yanayohusiana nayo.

Tunazaliwa na mwelekeo wa asili wa kuishi kwa muda mfupi, lakini ubatili wa mwisho wa njia hiyo ni mada ya Mhubiri 1-7. Wakati watu wanapokua wazee na kuanza kuhisi kuongezeka kwa athari ya mauti yao, wanajaribu kwa kufanana hasa kuwekeza rasilimali zao zinazofifia katika miradi ambazo kwao zinaonekana kuwa na ahadi zaidi ya maana ya kudumu katika maisha, hasa matumaini ya kuendeleza "jina" lao katika urithi wa kudumu (Mhubiri 2). Kwa bahati mbaya, hakuna mtu anayeweza kutabiri ni miradi gani ambayo itakuwa na thamani na umuhimu wa kudumu (Mhubiri 3:1-15), na kwa kawaida hii inasababisha viwango tofauti vya kuishiwa na imani na hata kukata tamaa juu ya ufupi wa maisha na udhalimu dhahiri "chini ya jua" (maneno Sulemani hutumia kuzungumza juu ya maisha hapa duniani (Mhubiri 3:16, 7:29).

Na utambuzi unaokua kwamba kuridhika katika shughuli kama hizo kila wakati ni za muda mfupi tu, tumaini la Sulemani ni kwamba watu watakua kwa hekima katika matumizi ya "sehemu" yao waliopewa na Mungu au mgao wao kabla ya kufa (Mhubiri 8-12; tazama pia Zaburi 90:12). Hekima hii inakua kuhusiana na ufahamu wetu wa "wakati na hukumu" — tunahitaji mtazamo wa Mungu katika uso wa ufupi wa maisha na udhalimu dhahiri (Mhubiri 3:15c-17; 8:5b-8, 12b-15; 9:11-12; 11:9; 12:14). Wazo la Kiebrania la muda katika vifungu hivi linachanganya dhana ya fursa (wakati mzuri wa kutenda kwa ufanisi wakati tukio linatokea) na maisha chache (muda mwingi tu sana kabla ya fursa zote kuenda). Wazo la kiebrania la hukumu katika maandiko haya inamaanisha uhuru kamili katika matumizi ya "sehemu" yetu tuliyopewa na Mungu katika maisha vile tamaa zetu zinatuongoza, bado na kuambatana na uwajibikaji kwa Mmoja ambaye alisambaza sehemu ya mgao wetu zilizotolewa. Agano Jipya inafanana kwa dhana hizi zinaweza kupatikana zimeonyeshwa waziwazi katika mafumbo ya Yesu ya wasichana kumi na talanta (Mathayo 25), wana wawili (Mathayo 21:28-32), na mtumishi asiye na haki (Luka 16:1- 13).

Mwandishi wa Mhubiri anakiri matatizo na changamoto za kukua mzee, ikiwa ni pamoja na upungufu wa kimwili na akili. Mhubiri anazungumzia matatizo haya kwa mtazamo wa kibinadamu (Mhubiri 7:15-18; 8:14; 9:3) bado hutoa hekima kutusaidia kukabiliana na kuzeeka kwa mtazamo wa Mungu, na kuhitaji wazo la "wakati na hukumu". Na uishaji wetu usioepukika wa imani juu ya hali ya kibinadamu — upotovu wetu wote, kutokuwa na uhakika, na mauti- ni busara kukumbuka kuwa "kwa kuwa liko tumaini kwa yule aliyeambatana na wote walio hai; (maana ni afadhali mbwa aliye hai kuliko simba aliyekufa); kwa sababu walio hai wanajua ya kwamba watakufa; lakini wafu hawajui neno lolote, wala hawana ijara tena; maana kumbukumbu lao limesahauliwa. Mapenzi yao na machukio yao, na husuda yao, imepotea yote pamoja; wala hawana sehemu tena katika jambo lolote lililofanyika chini ya jua"(Mhubiri 9:4-6). Wanajua kwamba wanajibika kwa "sehemu" yao iliyotolewa na Mungu, watu wanapaswa kuchukua fursa ya furaha ya vipawa vyao vyote, talanta, hekima, na nafasi katika maisha mapema badala ya baadaye — kabla ya nafasi yote ya kufanya hivyo imekoma (9:7- 10; 11:9-12:7).

Msukumo wa tafakari hili kutoka Mhubiri juu ya kukua mzee ni kwamba maana katika maisha inatimizwa katika kusudi la Mungu ambalo ametupa, na kusudi letu linatimizwa tu wakati tunapochukua fursa sehemu yetu aliyotupa Mungu katika Kristo, Mwokozi aliyeahidiwa na Mungu. Ingawa sehemu hii inaweza kuonekana kuwa isiyo ya haki kwa wengine kuliko ya wengine, maana ya maisha itakamilika tu wakati wa hukumu ya mwisho tunapopokea urithi wetu (Mhubiri 7:11) kwa njia tunayowekeza sehemu yetu, iwe ni mema au mbaya (Mhubiri 12:14; linganisha 2 Wakorintho 5:10). Siku hiyo, tutamwona Mungu kama tukufu katika tuzo Zake, bila kujali jinsi si haki au si sawa kusambazwa sehemu yetu inaweza kuonekana katika maisha ya sasa.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Biblia inasema nini kuhusu kuzeeka/kukua mzee?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries