settings icon
share icon
Swali

Je! Bibli ina miaka mingapi?

Jibu


Tangu Biblia iandikwe takribani na watu 40 tofauti katika kipindi cha miaka 1,500, swali ni, "Je! Biblia ina miaka mingapi?" haliwezi jibiwa katika idadi moja. Kitabu cha kwanza cha Biblia kuandikwa, pengine Mwanzo au Ayubu, kilikamilika karibu mwaka wa 1400 BC. Kitabu cha mwisho cha Biblia kuandikwa, labda ni Ufunuo, kulichokamilishwa mnamo mwa wa AD 90. Kwa hivyo, ikiwa unasingatia ni lini Biblia ilianza kuandikwa, Biblia ina umri wa zaidi ya miaka 3,400. Lakini, ikiwa unaiangalia kutoka wakati Biblia ilikamilika, Biblia ina zaidi ya umri wa miaka 1,900

Wasomi wa kihafidhina wa Biblia wanaamini kuwa labda Kitabu cha Mwanzo au Kitabu cha Ayubu kilikuwa kitabu cha kwanza cha Biblia kuandikwa, kuna uwezekano labda Musa, na pengine miaka 40 jangwani wakizunguka kati mwa kutoka Misri na kifo cha Musa. Hii itaiweka tarehe ya uhandishi popote kati ya 1450 Kabla ya Kristo (KK) na 1400 KK

Pia, wasomi wengi wahafidhina wa Biblia wanaamini Kitabu cha Ufunuo ndio kilikuwa cha mwisho cha Biblia kuandikwa na mtume Yohana kati ya mwaka wa AD 90 na 95, wakati wa uhamisho wa Yohana kwenye kisiwa cha Patmo. Kuna uwezekano kwamba Yohana aliandika 1, 2, au 3 Yohana ua hata Injili ya Yohana, baada ya Kitabu cha Ufunuo. Lakini kubaliano ni kuwa Kitabu cha Ufunuo kilikuwa cha mwisho cha uandishi wa Yohana.

Hakika Biblia ni kitabu cha ajabu. Biblia ina umri kati ya miaka 3,400 na 1,900 na kime na kimeshawishi watu wengi na tamaduni duniani kote. Hata uandishi wake unapoenda nyuma kwa historia ya zamani, ujumbe wa Biblia ni wa kweli kabisa na unatumika hii leo. Ni kwa njia ya uvuvio wa kiungu Biblia ingeweza kuandikwa kitambo sana, na katika kipindi hicho kirefu cha wakati, na bado isiwe na makosa na utata wowote.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je! Bibli ina miaka mingapi?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries