settings icon
share icon
Swali

Je! Biblia ni hekaya tu?

Jibu


Dhana kwamba Biblia ni hadithi au kitabu cha hadithi njema sio mpya. Bila shaka Biblia ni kitabu kinaschoshawishi sana ambacho ulimwengu umewahitambua, kimebadilisha maisha ya watu ambao hatuwezi kuhesabu. Kwa nini basi, swali lolote kwamba Biblia ni hadithi ni mojawapo halali katika mioyo ya wengi duniani kote?

Kutoka kitabu cha Mwanzo hadi kitabu cha Ufunuo, tunasoma hadithi ya mpango wa milele wa Mungu ili kuukomboa ulimwengu ulioanguka.Mungu kama Mwandishi wake, Biblia ni kazi kubwa duniani ya vitabu, na kwa miaka mingi watu wengi wameishi kutangaza ukweli wake. Wengi, kwa kweli, wamejitolea mhanga ili wengine waweze kushika kwa mikono yao nakala ya kurasa zake. Hata hivyo, hakujawahi kuwa na kitabu ambacho kimeshambuliwa vikali kama Biblia. Biblia imekupigwa marufuku, kuchomwa, kutusiwa, na kudunishwa. Wengi wameuawa kwa kuwa na Biblia tu. Lakini bado wazo kwamba Biblia ni hadithi inaendelea.

"Mkuu wa ulimwengu huu" amekuwa akiwaficha watu ukweli tangu mwanzo wa wakati. Alianza "kazi" yake duniani akitikia shaka maneno ya Mungu(Mwanzo 3: 1-5), na amekuwa akifanya hivyo tangu wakati huo. Kila mahali tunapoangalia, mafundisho ya uongo yanaenea-kwenye televisheni na redio, katika vitabu na magazeti, katika shule zetu na vyuo vikuu, na kwa kusikitisha, hata katika makanisa fulani na vyuo vya Kikristo, mahali ambapo ambapo ukweli wa Neno la Mungu unapaswa kulindwa sana . Wakati watoto wanafundishwa kuwa babu zetu walitoka katika bahari miaka mingi iliyopita, je! Hatujachukulia uumbaji wa Adamu na Hawa kuwa ni hadithi? Ni jambo lile lile wakati wanasayansi na wasomi wanatuambia tunapoteza wakati wetu kutafuta "Safina ya Nuhu" ya "wanaoifanya ka hadithi tu".

Kwa kweli, wakati wengi kanisani, ili kuridhisha ulimwengu wa kitaaluma, wanaruhusu kutafsiri tofauti kwa kitabu cha Mwanzo ili kuzingatia mawazo ya kisasa ya mageuzi, ujumbe uliotumwa ulimwenguni ni kwamba Biblia, inaonekana, ina maana ya kitu kingine kuliko kile maneno yake rahisi, ya kawaida yanaonyesha. Wakati matukio ya kawaida ya Biblia yanajulikana kuwa ni madai ya asili, inaeleweka jinsi wale ambao hawajajifunza Biblia wanaweza kuchanganyikiwa kama ukweli wake. Kwa wale ambao hawajui ukweli wa Neno la Mungu, ni vipi wanaweza kuamini katika punda kuzungumza au samaki kumeza mtu na kumtema kwenye pwani au mwanamke aliyegeuka kuwa nguzo ya chumvi?

Hata hivyo, Biblia hakika sio hadithi tu. Kwa kweli, Biblia imeanndikwa kwa uongozi wa Mungu (2 Timotheo 3:16), na hii ina maana kwamba Mungu aliiandika. Waandishi wake wa kibinadamu waliandika kutoka kwa Mungu kama walipokuwa wakiongozwa na Roho Mtakatifu (2 Petro 1:21). Ndio sababu maandishi haya ya miadi ya karibu ya robo tatu ya maneno milioni ni kamilifu kutoka mwanzo hadi mwisho na hayana vikwazo, ingawa vitabu vyake sitini na sita vina waandishi arobaini tofauti kutoka kwa maeneo tofauti ya dunia, yaliyoandikwa katika lugha tatu tofauti, na kuchukua karne kumi na sita kukamilisha. Je, inawezekanaje kuwa na kikundi hiki cha kushangaza ikiwa haikuwa kwa Mungu kuongoza mikono ya waandishi? Mungu mwenye haki hawezi kamwe kusababisha hitilafu. Mungu mwenye haki haitaita Maandiko yaliyo na hitilafu "takatifu na ya kweli". Mungu mwenye huruma hawezi kusema kwamba Neno Lake ni kamilifu kama sio kamilifu, na Mungu mwenye ujuzi aliweza kuandika hivyo kuwa ni muhimu nay a kufaa leo kama ilivyokuwa maelfu ya miaka iliyopita.

Mara kwa mara, historia ya Biblia imethibitishwa na biolojia, jiologia, na elimu ya nyota. Na, ingawa Biblia haiwezi kukubaliana na dhana za asili, haishindani na ukweli wowote wa kisayansi, ulioanzishwa. Katika akaeologia, miaka mia moja iliyopita imetoa ufafanuzi wa dhamana ya ukweli wa kibiblia ambayo wasomi walitilia shaka au wasiwasi kwa karne nyingi, kama vile hati za kuvingirisha za Bahari ya Mauti, jiwe la ngumu nyeusi iliyo na uandishi wa "Nyumba ya Daudi," karne ya 7 BC kitabu ambacho kimeandikwa jina la Mungu, na jiwe ambalo limeandikwa jina na jina la Pontiyo Pilato, gavana wa Yuda ambaye aliamuru kuuawa kwa Yesu Kristo. Biblia bila shaka kitabu kilichoandikwa vizuri zaidi kutoka ulimwengu wa kale, kikiwa na zaidi ya 24,000 maandiko kamilifu au sehemu ya maandiko hayo ya kibiblia. Hakuna hati nyingine ya kale ina ushahidi karibu sana kuthibitisha uaminifu wake.

Uthibitisho mwingine kwa uandishi wa kiungu wa Biblia ni idadi kubwa ya unabii wa kina wa kibiblia ambao umetimizwa kama vile ilivyovyotabiriwa. Tunaona mtunga-zaburi, kwa mfano, akisema juu ya kusulubiwa kwa Yesu Kristo karibu miaka elfu kabla ya kutokea (Zaburi ya 22) na mamia ya miaka kabla ya kusulubiwa kugunduliwa! Kwa kueleza tu, haingewezekana kwa wanadamu kuwa wameona mbali hadi katika siku zijazo kwa usahihi kwa mamia ya nyakati. Kwa hakika ingekuwa haileti maanaa kuamini unabii huu ni kitu chochote isipokuwa kazi ya Mungu. Kwa kushangaza, wataalam yamkini wanatuambia uwezekano wa unabii kuhusu mtu mmoja (yaani Kristo) kutimia ni nadra sana.

Lakini ushahidi mkubwa zaidi kwamba Biblia si hekaya ni idadi ya maisha ambayo yamebadilishwa na kurasa zake. Huku ikitumiwa na Roho wa Mungu, ukweli mtakatifu wa Biblia umegeuza mamilioni ya wenye dhambi kuwa watakatifu. Waraibu wa madawa ya kulevya yameponywa kupitia Neno, washoga wanawekwa huru, waliosusisia majukumu ya malezi wamebadilishwa na Neno la Mungu, wahalifu wamebalishwa na wenye dhambi walikemewa na Neno , na chuki ikageuka kuwa upendo. Kusoma hekaya kama vile "Cinderella" au "snow white'na Seven Dwarfs" hakuwezi kuleta mabadiliko hayo juu ya roho ya mwanadamu. Biblia ina nguvu yenye kubadilisha ambayo inawezekana tu kwa sababu kweli ni Neno la Mungu.

Kwa kuzingatia yale yaliyotangulia, swali kubwa, basi, inawezekanaje kuwa mtu anakosa kuamini ukweli huu unaoshawishi, uliongozwa na Mungu, usio na hitilafu, unaobadilisha maisha? Kuna jibu rahisi la Sali hilo.Mungu amesema kwamba ikiwa hatufungui mioyo yetu kwake, Yeye hatatufungua macho yetu kwa kweli. Yesu aliahidi Roho Mtakatifu atatufundisha (Yohana 14:26) na kutuongoza katika ukweli (Yohana 16:13). Na ukweli wa Mungu unapatikana katika Neno la Mungu (Yohana 17:17). Hivyo, kwa wale wanaoamini, maneno haya matakatifu ni uhai, lakini, kwa wale ambao hawana Roho wa Mungu, Biblia si kitu isipokuwa upumbavu (1 Wakorintho 2:14).

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je! Biblia ni hekaya tu?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries