settings icon
share icon
Swali

Je! Wakristo wana mamlaka ya kuwaamrisha malaika?

Jibu


Watu hii leo wanavutiwa na dhana na kusoma kuhusua malaika, inayoitwa "Somo kuhusu malaika". Malaika huonyeshwa katika kila kitu, kutoka kwa mapambo na mapambo ya Krismasi, kwa sinema na vipindi vya Runinga. Wakristo wengi pia wanaamini kuwa wana mamlaka ya kuwaamuru malaika kutii amri zao, hukui wengine wanaamini wanaweza kuwaamuru malaika (na hata pepo) kwa jina la Yesu.

Hakuna matukio katika Maandiko ambapo wanadamu waliweza kutoa amri za malaika, ama kwa jina lao au kwa jina la Yesu. Hakuna vifungu ambapo mtu ana mamlaka juu ya kazi ya malaika. Tunajua kwamba wao ni viumbe wa cheo cha juu, kwa sababu Yesu amejieka yeye mwenyewe "kiwango cha chini kuliko malaika" ili azaliwa na kuteseka kama mwanadamu (Waebrania 2: 7-9; Zaburi 8: 4).

Mafundisho kwamba waumini wana mamlaka juu ya malaika ni uongo. Kanuni zifuatazo za Biblia zinaonyesha kwamba malaika hawatii amri za wanadamu:

• Musa alizungumza wakati wana wa Israeli "Tulimlilia Mwenyezi-Mungu, naye akakisikia kilio chetu, akatuletea malaika aliyetuondoa Misri" (Hesabu 20:16). Waisraeli hawakuamuru malaika kuja kwao. Walimwomba Mungu, ambaye chini ya amri yake malaika hufanya kazi.

Shadraki, Meshaki, na Abednego walikataa kuinamia sanamu ya Nebukadneza (Danieli 3: 17-18). Mungu kwa rehema yake "alimtuma malaika wake na kuwaokoa watumishi wake" (Danieli 3:28). Waebrania watatu hawakuita malaika wa Bwana. Mungu alimtuma. Mungu baadaye "alimtuma malaika wake" kumtoa Danieli kutoka vinywa vya simba katika shimo mwao (Danieli 6:22).

• Kanisa la Yerusalemu lilimwombea Petro alipokuwa gerezani (Matendo 12: 5). Petro alipoachiliwa, alihubiri, "Sasa najua kwa hakika kwamba Bwana amemtuma malaika wake akaniokoa mikononi mwa Herode na kutoka katika mambo yale yote watu watu wa Israeli waliyotazamia" (Matendo 12:11). Wakristo wakiomba kwa ajili ya Petro walishangaa sana alipofika mlangoni mwao karibu wasimruhusu angie ndani. Kwa hakika, hawakuwa wamemwamuru malaika yeyote kumwokoa.

Malaika huitwa "malaika watakatifu" wa Mungu, ambao hufanya kazi yake, sio yetu (Mathayo 25:31; Ufunuo 14:10).

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je! Wakristo wana mamlaka ya kuwaamrisha malaika?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries