settings icon
share icon
Swali

Agano jipya ni nini?

Jibu


Agano jipya (au Agano Jipya) ni ahadi ambayo Mungu hufanya na ubinadamu kwamba atasamehe dhambi na kurejesha ushirika na wale ambao nyoyo zao zimemgeukia. Yesu Kristo ndiye mpatanishi wa agano jipya, na kifo chake msalabani ni msingi wa ahadi (Luka 22:20). Agano jipya lilitabiriwa wakati agano la kale lilikuwa bado limefanyika-manabii Musa, Yeremia, na Ezekiel wote wanazingatia agano jipya.

Agano la kale ambalo Mungu alilianzisha na watu wake lilihitaji utii mkali kwa sheria ya Musa. Kwa sababu mshahara wa dhambi ni mauti (Warumi 6:23), Sheria ilihitaji Israeli kufanya dhabihu ya kila siku ili kuangamiza dhambi. Lakini Musa, ambaye kupitia kwake Mungu alianzisha agano la kale, pia alitarajia agano jipya. Katika moja ya anwani zake za mwisho kwa taifa la Israeli, Musa anaangalia mbele wakati ambapo Israeli watapewa "moyo wa kuelewa" (Kumbukumbu la Torati 29: 4).

Musa anatabiri kwamba Israeli wangeweza kushindwa na kushika agano la kale (Kumbukumbu la Torati 29: 22-28), lakini kisha anaona wakati wa kurejeshwa (Kumbukumbu la Torati 30: 1-5). Wakati huo, Musa anasema, "Bwana Mungu wako atautahiri moyo wako na moyo wa uzao wako ili umpende Bwana, Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, upate kuwa hai" (mstari wa 6). Agano jipya linahusisha mabadiliko ya moyo ili watu wa Mungu kwa kawaida wawe kumpendeza.

Nabii Yeremia pia alitabiri agano jipya. "Angalia,siku zinakuja" asema Bwana, 'nitakapofanya agano jipya na nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda. . . . Bali agano hili ndilo nitakalofanya na nyumba ya Israeli, baada ya siku zile, asema Bwana: Nitatia sharia yangu ndani yao, na katika mioyo yao nitaiandika, name nitakuwa Mungu wao, nao watukuwa watu wangu "(Yeremia 31:31, 33). Yesu Kristo alikuja kutekeleza sheria ya Musa (Mathayo 5:17) na kuanzisha agano jipya kati ya Mungu na watu wake. Agano la kale liliandikwa kwa mawe, lakini agano jipya limeandikwa mioyoni mwetu. Kuingia katika agano jipya kunawezekana tu kupitia imani katika Kristo, ambaye alimwaga damu yake ili aondoe dhambi za ulimwengu (Yohana 1:29). Luka 22:20 inasimulia jinsi Yesu, katika chakula ya jioni ya mwisho, anachukua kikombe na kusema, "kikombe hiki kinachomwagika kwa ajili yenu ni agano jipya katika damu yangu."

Agano jipya pia limetajwa katika Ezekieli 36: 26-27, "Nami nitawapa ninyi moyo mpya, nami nitatia roho mpya ndani yenu, nami nitatoa moyo wa jiwe uliomo ndani ya mwili wenu, nami nitawapa moyo wa nyama. Nami nitatia roho yangu ndani yenu na kuwaendesha katika sheria zangu nanyi mtazishika hukumu zangu na kuzitenda . "Ezekieli anataja mambo kadhaa ya agano jipya hapa: moyo mpya, roho mpya, Roho Mtakatifu anaoishi, na utakatifu wa kweli . Sheria ya Musa haiwezi kupeana mambo haya (tazama Warumi 3:20).

Agano jipya lilipeanwa hapo awali kwa Israeli na linajumuisha ahadi ya kuzaa, baraka, na kuwepo kwa amani katika Nchi ya Ahadi. Katika Ezekieli 36: 28-30 Mungu anasema, "Nanyi mtakaa katika nchi ile niliyowapa baba zenu; nanyi mtakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu. . . . Nitaiita ngano na kuiongeza , wala sitaweka njaa juu yenu tena. Nami nitazidisha matunda ya miti, na mazao ya mashamba, msipate tena kutukanwa na mataifa kwa sababu ya njaa. "Kumbukumbu la Torati 30: 1-5 lina maadili sawa yanayohusiana na Israeli chini ya agano jipya. Baada ya ufufuo wa Kristo, Mataifa waliletwa katika baraka za agano jipya, pia (Matendo 10, Waefeso 2: 13-14). Utekelezaji wa agano jipya utaonekana katika maeneo mawili: duniani, wakati wa ufalme wa milenia; na mbinguni, kwa milele.

Sisi hatuko chini ya Sheria tena bali chini ya neema (Warumi 6: 14-15). Agano la kale limefanya kazi yake, na limebadilishwa na "agano bora" (Waebrania 7:22). "Lakini sasa amepata huduma iliyo bora zaidi, kwa kadiri alivyo mjumbe wa agano lililo bora, lililo amriwa juu ya ahadi zilizo bora" (Waebrania 8: 6).

Chini ya agano jipya, tunapewa fursa ya kupokea wokovu kama zawadi ya bure (Waefeso 2: 8-9). Wajibu wetu ni kuonyesha imani katika Kristo, Yeye aliyetimiza Sheria kwa niaba yetu na kumaliza dhabihu za Sheria kwa njia ya kifo chake cha dhabihu. Kupitia Roho Mtakatifu anayetoa maisha ambaye anaishi kwa waumini wote (Warumi 8: 9-11), tunashiriki katika urithi wa Kristo na kufurahia uhusiano wa kudumu, uhusiano thabiti na Mungu (Waebrania 9:15).

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Agano jipya ni nini?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries