settings icon
share icon
Swali

Agano la Ibrahimu ni nini?

Jibu


Agano ni makubaliano kati watu wawili au vikundi viwili. Kuna aina mbili za msingi za maagano: Yenye masharti na bila masharti. Agano la masharti ni mojawapo ya makubaliano ambayo yanafunga kwa pande mbili kwa utimilifu wake. Vikundi vyote vikubaliana kutimiza masharti. Ikiwa kikundi chochote kinashindwa kufikia majukumu yao, agano hio huvunjwa na hakuna kikundi kinachotimiza matarajio ya agano. Agano la masharti au moja kwa moja ni makubaliano kati ya vilkundi viwili, lakini moja tu ya vikundi hivyo viwili ndicho kinalazimika kufanya jambo. Hakuna kitu kinachohitajika kutoka kwa kikundi hicho kingine.

Agano la Ibrahimu ni agano lisilo na masharti. Mungu alifanya ahadi kwa Ibrahimu ambayo haikuhitaji chochote cha Ibrahimu. Mwanzo 15: 18-21 inaelezea sehemu ya agano la Abrahamu, hususan kuhusu vipimo vya ardhi ambayo Mungu aliahidi Ibrahimu na wazao wake.

Agano halisi la Ibrahimu linapatikana katika Mwanzo 12: 1-3. Sherehe iliyonukuliwa katika Mwanzo 15 inaonyesha hali isiyo na masharti ya agano. Wakati pekee ambao pande zote mbili za agano zilipita kati ya vipande vya wanyama ni wakati kutimiza kwa agano kulitegemea pande zote mbili. Tunapozungumzia kuhusu umuhimu wa Mungu peke yake kusonga kati ya nusu ya vipande za wanyama, ni lazima ieleweke kwamba ni tanuru ya moshi na mwenge uliowaka, zinazowakilisha Mungu, sio Ibrahimu, ambazo ilipita kati ya vipande vya nyama. Kitendo hicho, kinaonekana, kinapaswa kugawanywa kwa pande zote mbili, lakini katika agano hiyo hatua ya Mungu ya faragha haina budi kueleza ukweli kwamba agano hio ilikua ahadi ya Mungu. Anajifunga mwenyewe kwa agano. Mungu alifanya Ibrahimu kupatwa za usingizi ili asingeweza kupita kati ya vipande viwili vya wanyama. Utekelezaji wa agano ulikuja kwa Mungu pekee.

Baadaye, Mungu alimpa Abrahamu ibada ya kutahiriwa kama ishara maalum ya agano la Abrahamu (Mwanzo 17: 9-14). Wanaume wote katika uzao wa Ibrahimu walipaswa kutahiriwa na hivyo kubeba alama yao ya kila siku katika mwili wao kuwa walikuwa sehemu ya baraka ya Mungu duniani. Mtu yeyeote katika uzao wa Ibrahimu ambaye alikataa kutahiriwa alikuwa akijitangaza kuwa nje ya agano la Mungu; hii inaelezea kwa nini Mungu alikasirika na Musa wakati Musa hakumtahiri mwanawe katika Kutoka 4: 24-26.

Mungu aliamua kuita watu maalum kwa ajili yake mwenyewe, na kwa njia ya watu hao maalum angeleta baraka kwa mataifa yote. Agano la Ibrahimu ni muhimu kwa ufahamu sahihi wa dhana ya ufalme na ni msingi kwa teolojia ya Agano la Kale. Agano la Ibrahimu linaelezewa katika Mwanzo 12: 1-3, na (1) ni agano lisilo na masharti. Hakuna masharti yanayoambatana nayo ( Hamna kifungu cha "ikiwa'') kinachoonyesha kwamba utimilifu wake unategemea mtu). (2) Pia ni agano halisi ambalo ahadi zinapaswa kueleweka kwa kweli. Ardhi liyoahidiwa inapaswa kueleweka kwa ufafanuzi wa kawaida wa neno hilo -sio takwimu ya mbinguni. (3) pia ni agano la milele. Ahadi ambazo Mungu alifanya kwa Israeli ni za milele.

Kuna sifa tatu kuu kwa agano la Ibrahimu:

1. ahadi ya ardhi (Mwanzo 12: 1). Mungu alimwita Ibrahimu kutoka Ure ya Wakaldayo kwenda katika ardhi ambayo angeweza kumpa (Mwanzo 12: 1). Ahadi hii inaelezewa katika Mwanzo 13: 14-18; vipimo vyake vinanukuliwa katika Mwanzo 15: 18-21 (kuzuia wazo lolote la hili kutimizwa mbinguni). Kipengele cha ardhi cha agano la Abrahamu kinaelezewa Zaidi katika Kumbukumbu la Torati 30: 1-10, ambalo ni agano la Palestina.

2. ahadi ya uzao (Mwanzo 12: 2). Mungu aliahidi Ibrahimu kwamba atafanya taifa kubwa kutoka kwake. Ibrahimu, aliyekuwa na umri wa miaka 75 na asiye na watoto (Mwanzo 12: 4), aliahidiwa wazawa wengi. Ahadi hii imeelezwa katika Mwanzo 17: 6 ambako Mungu aliahidi kwamba mataifa na wafalme watatoka kwa kwa babu wa zamani. Ahadi hii (iliyoelezewa kwa kina katika agano la Davidi la 2 Samweli 7: 12-16) ingetokea katika kiti cha Daudi na ufalme wa Masihi kutawala watu wa Kiebrania.

3. ahadi ya baraka na ukombozi (Mwanzo 12: 3). Mungu aliahidi kumbariki Abrahamu na familia za dunia kupitia kwake. Ahadi hii imeelezewa kwa kina katika Agano Jipya (Yeremia 31: 31-34; tazama Waebrania 8: 6-13) na inahusiana na baraka ya kiroho na ukombozi wa kiroho kwa wana wa Israeli. Yeremia 31:34 inatarajia msamaha wa dhambi. Hali isiyo na masharti na ya milele ya agano imeonekana kwa kuwa agano limehakikishiwa kwa Isaka (Mwanzo 21:12; 26: 3-4). Maneno "Mimi nitafanya" yanaahidi tena kupendekeza kipengele cha agano isiyo la masharti . Agano limehakikishiwa Yakobo baadaye (Mwanzo 28: 14-15). Ni muhimu kuona kwamba Mungu alithibitisha ahadi hizi katikati ya dhambi za baba zetu, jambo ambalo linasisitiza zaidi hali isiyo na masharti ya agano la Ibrahimu.

Njia ya Mungu ya kutimiza agano la Ibrahimu ni halisi, hata kama Mungu alitimiza sehemu ya agano katika historia: Mungu alimbariki Ibrahimu kwa kumpa ardhi (Mwanzo 13: 14-17), na, karne baadaye, wana wa Ibrahimu walichukua udhibiti wa ardhi: "Basi Bwana aliwapa Israeli ardhii yote aliyoapa kuwapa baba zao, nao wakaimiliki na kukaa pale" (Yoshua 21:43). Mungu alibariki Ibrahimu kiroho (Mwanzo 13: 8, 18; 14: 22-23; 21:22); Mungu alimpa wazao wengi (Mwanzo 22:17; 49: 3-28). Sehemu muhimu ya agano la Ibrahimu, hata hivyo, inahitaji utimilifu wa wakati ujao na utawala wa ufalme wa Mesia:

(1) Israeli kama taifa litamiliki ardhi yote baadaye. Vifungu vingi vya Agano la Kale vinatarajia baraka za Israeli za baadaye na kumiliki ardhi kama alivyoahidiwa Ibrahimu. Ezekieli anaelezea siku ya baadaye wakati Israeli atakaporudishwa kwenye ardhi (Ezekieli 20: 33-37, 40-42; 36: 1-37: 28).

(2) Israeli kama taifa litakubali Yesu kama Masihi na kusamehewa na kurejeshwa (Warumi 11: 25-27).

(3) Israeli watatubu na kupokea msamaha wa Mungu baadaye (Zakaria 12: 10-14). Agano la Ibrahimu linapata utimilifu wake kamili kuhusiana na kurudi kwa Masihi kuokoa na kubariki watu wake, Israeli. Ni kupitia taifa la Israeli ambayo Mungu aliaahidi katika Mwanzo 12: 1-3 kubariki mataifa ya dunia. Hiyo baraka kuu itatoka katika msamaha wa dhambi na ufalme wa utukufu wa Masihi duniani.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Agano la Ibrahimu ni nini?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries