settings icon
share icon
Swali

Kwa nini ukweli wa ufufuo wa kimwili wa Yesu Kristo ni muhimu sana?

Jibu


Ufufuo wa kimwili wa Yesu Kristo ni tukio muhimu zaidi katika historia, inayotoa ushahidi dhahiri kwamba Yesu ndiye alivyodai kuwa — Mwana wa Mungu. Ufufuo sio tu uthibitisho mkuu wa uungu wake; pia ilithibitisha Maandiko, ambayo yalitabiri kuja kwake na ufufuo. Zaidi ya hayo, ilithibitisha madai ya Kristo kwamba angefufuliwa siku ya tatu (Yohana 2:19-21, Marko 8:31; 9:31; 10:34). Ikiwa mwili wa Kristo haukufufuliwa, hatuna tumaini kwamba yetu itafufuliwa (1 Wakorintho 15:13, 16). Kwa kweli, mbali na ufufuo wa kimwili wa Kristo, hatuna Mwokozi, hakuna wokovu, na hakuna tumaini la uzima wa milele. Kama vile mtume Paulo alisema, imani yetu itakuwa "bure" na nguvu za kuhuisha za Injili zitaondolewa kwa pamoja.

Kwa sababu takdiri zetu za milele zinategemea ukweli wa tukio hili la kihistoria, ufufuo umekuwa lengo la mashambulizi makubwa ya Shetani dhidi ya kanisa. Kwa hivyo, uhalisi wa matukio ya ufufuo wa kimwili wa Kristo umechunguzwa na kupelelezwa kutoka kila pembe na kutafitiwa bila mwisho na wasomi wengi, wanateolojia, profesa, na wengine kwa karne nyingi. Na ingawa nadharia kadhaa zimeandikwa ambazo zinajaribu la kupinga tukio hili la maana sana, hakuna ushahidi wa kihistoria wa kuaminika unaoweza kuthibitisha kitu chochote isipokuwa ufufuko Wake halisi wa kimwili. Kwa upande mwingine, ushahidi wa wazi na wenye kushawishi wa ufufuo wa kimwili wa Yesu Kristo umeshinda kabisa.

Hata hivyo, kutoka kwa Wakristo wa Korintho ya kale hadi wengi leo, kutoelewana kunaendelea kuhusiana na mambo fulani ya ufufuo wa Mwokozi wetu. Kwa nini, wengine wanauliza, je, ni muhimu kwamba mwili wa Kristo ulifufuliwa? Je! Ufufuo wake haukuweza kuwa wa kiroho tu? Kwa nini na jinsi gani ufufuo wa Yesu Kristo unahakikisha ufufuo wa kimwili wa waumini? Je! Miili yetu iliyofufuliwa itakuwa sawa na miili yetu ya kidunia? Ikiwa sivyo, itakuwa kama nini? Majibu ya maswali haya yanapatikana katika sura ya kumi na tano ya barua ya kwanza ya Paulo kwa kanisa la Korintho, kanisa ambalo alianzisha miaka kadhaa mapema wakati wa safari yake ya pili ya kimisheni.

Mbali na ukuaji wa vikundi katika kanisa changa la Korintho, kulikuwa na kutoelewana kulioenea kwa baadhi ya mafundisho muhimu ya kikristo, ikiwemo ufufuo. Ingawa Wakorintho wengi walikubali kwamba Kristo amefufuliwa (1 Wakorintho 15: 1, 11), walikuwa na ugumu kuamini wengine wangeweza kufufuliwa. Ushawishi unaoendelea wa falsafa ya Gnostic, ambayo ilishikilia kuwa kila kitu cha kiroho kilikuwa kizuri lakini kila kitu cha kimwili, kama vile miili yetu, kilikuwa kiovu halisi, ilikuwa iwajibika kimsingi kwa kiwewe chao kuhusu ufufuo wao wenyewe. Dhana ya maiti ya kahara kufufuliwa milele ilikuwa, kwa hivyo, ilipingwa vikali sana na wengine na kwa hakika na wafalsafa wa Kigiriki wa siku (Matendo 17:32).

Hata hivyo Wakorintho wengi walielewa kwamba ufufuo wa Kristo ulikuwa wa kimwili na sio wa kiroho. Hata hivyo, ufufuo unamaanisha "kuamka kutoka kwa wafu"; kitu kurudi hai. Walielewa kwamba nafsi zote zingeishi milele (isiokufa) na katika kifo ilienda mara moja kuwa na Bwana (2 Wakorintho 5:8). Hivyo, ufufuo wa "kiroho" haungekuwa na maana, kwa vile roho haikufi na kwa hivyo haiwezi kufufuliwa. Zaidi ya haya, walifahamu kwamba Maandiko, pamoja na Kristo Mwenyewe, alisema kwamba mwili Wake ungeweza kuamka tena siku ya tatu. Maandiko pia yalifanya wazi kwamba mwili wa Kristo hautaoza (Zaburi 16:10; Matendo 24:39), shtaka ambalo halingekuwa na maana iwapo mwili Wake haungefufuliwa. Hatimaye, Kristo aliwambia wanafunzi Wake waziwazi kuwa ni mwili Wake uliofufuliwa: "Kwa kuwa roho haina mwili na mifupa kama mnavyoniona mimi kuwa nayo"(Luka 24:39).

Tena, hata kama, wasiwasi wa Wakorintho ilikuwa juu ya ufufuo wao binafsi. Kwa hiyo, Paulo alijaribu kuwashawishi Wakorintho kuwa kwa sababu Kristo alifufuliwa kutoka kwa wafu, wao pia watafufuliwa kutoka kwa wafu siku fulani, na kwamba fufuo sote mbili — ya Kristo na yetu — lazima isimame au kuanguka kwa pamoja, kwa maana "lakini kama hakuna kiyama ya wafu, Kristo naye hakufufuka"(1 Wakorintho 15:13).

"Lakini sasa Kristo amefufuka katika wafu, limbuko lao waliolala. Maana kwa kuwa mauti ililetwa na mtu, kadhalika na kiyama ya wafu ililetwa na mtu. Kwa kuwa kama katika Adamu wote wanakufa, kadhalika na katika Kristo wote watahuishwa"(1 Wakorintho 15:20-22).

Wakati Yesu Kristo alifufuliwa, akawa "matunda ya kwanza" ya wote ambao watafufuliwa (angalia pia Wakolosai 1:18). Waisraeli hawangeweza kuvuna mazao yao kikamilifu mpaka walipoleta sampuli ya wakilishi (matunda ya kwanza) kwa makuhani kama sadaka kwa Bwana (Mambo ya Walawi 23:10). Hii ndio Paulo anasema katika 1 Wakorintho 15: 20-22; Ufufuo wa Kristo mwenyewe ulikuwa "matunda ya kwanza" ya ufufuo "mavuno" ya wafu waumini. Lugha "matunda ya kwanza" ambayo Paulo anatumia inaonyesha kitu cha kufuata, na kwamba kitu cha kuwa wafuasi Wake — sehemu ya "mavuno." Hivi ndivyo ufufuo wa Kristo unavyothibitisha wetu. Hakika, ufufuo wake unahitaji ufufuo wetu.

Na kutuliza wasiwasi wao kuhusu kuunganisha roho kwa kile kilichoonekana kuwa mwili usiofaa, Paulo aliwaelezea asili ya miili yetu iliyofufuliwa na jinsi gani ingekuwa tofauti na miili yetu ya kidunia. Paulo alifananisha miili yetu ya kidunia na "mbegu," na Mungu hatimaye atatoa mwili mwingine (1 Wakorintho 15: 37-38) ambao utakuwa kama mwili wa utukufu wa Kristo uliofufuliwa (1 Wakorintho 15:49; Wafilipi 4:21). Hakika, kama vile tu na Bwana wetu, miili yetu ambayo sasa si ya kudumu, iliyofedhehesha, dhaifu, na ya asili itafufuliwa siku moja katika miili ambayo ni ya kudumu, yenye utukufu, yenye nguvu, na ya kiroho (1 Wakorintho 15:42-44). Miili yetu ya kiroho itatayarishwa kabisa kwa ajili ya uhai wa mbinguni, usio wa kawaida.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Kwa nini ukweli wa ufufuo wa kimwili wa Yesu Kristo ni muhimu sana?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries