settings icon
share icon
Swali

Ina maana gani kwamba Yesu ni mwana wa Daudi?

Jibu


"Ina maana gani kwamba Yesu ni mwana wa Daudi?"

Jibu: Aya kumi na saba katika Agano Jipya zinaelezea Yesu kama "mwana wa Daudi." Lakini swali linatokea, Yesu angewezaje kuwa mwana wa Daudi kama Daudi aliishi karibu miaka 1000 kabla ya Yesu? Jibu ni kwamba Kristo (Masihi) alikuwa kutimiza unabii wa uzao wa Daudi (2 Samweli 7: 12-16). Yesu alikuwa Masihi aliyeahidiwa, maana yake alikuwa Mzao wa Daudi. Mathayo 1 inatoa uthibitisho wa kizazi kwamba Yesu, katika ubinadamu Wake, alikuwa kizazi cha Daudi kwa njia ya Yosefu, baba wa Yesu wa kisheria. Nasaba katika Luka sura ya 3 inatoa uzao wa Yesu kwa njia ya mama yake, Maria. Yesu ni uzao wa Daudi, kwa kuteuliwa kwa njia ya Yosefu, na kwa damu kupitia Maria. Kimsingi, wakati Kristo aliitwa kama mwana wa Daudi, ilikuwa ina maana ya kutaja jina lake la Kimasihi kama Agano la Kale lilitabiri juu yake.

Yesu alitajwa kama "Bwana, wewe mwana wa Daudi" mara kadhaa na watu ambao, kwa imani, walikuwa wanatafuta huruma au uponyaji. Mwanamke ambaye binti yake alikuwa akiteswa na pepo (Mathayo 15:22), watu wawili vipofu karibu na barabara (Mathayo 20:30), na Bartimayo kipofu (Marko 10:47) wote walimwomba mwana wa Daudi kwa msaada . Majina ya heshima waliyompa yalitangaza imani yao ndani yake. Kumwita "Bwana" walionyesha maana yao ya uungu wake, mamlaka, nguvu, na kwa kumwita "Mwana wa Daudi," walikuwa wanamwita kuwa Masihi.

Wafarisayo, pia, walielewa maana ya nini waliposikia watu wakimwita Yesu "mwana wa Daudi." Lakini tofauti na wale walilia kwa imani, walipofushwa sana na kiburi chao wenyewe na ukosefu wa ufahamu wa Maandiko ambayo hawakuweza tazama kile waombaji kipofu angeweza kuona — kwamba hapa alikuwa Masihi walidhani walikuwa wakisubiri maisha yao yote. Walimchukia Yesu kwa sababu Yesu hawezi kuwapa heshima waliyofikiri wanastahili. Kwa hiyo, waliposikia watu wakimtukuza Yesu kama Mwokozi, walikasirika (Mathayo 21:15) na wakaamua kumwangamiza (Luka 19:47).

Yesu aliwafadhaika tena waandishi na Mafarisayo kwa kuwauliza kuelezea maana ya cheo hiki. Inawezaje kuwa Masihi ni mwana wa Daudi wakati Daudi mwenyewe akimwita "Bwana wangu" (Marko 12: 35-37)? Bila shaka, walimu wa sheria hawakuweza kujibu swali hilo. Kwa hiyo Yesu alifunua wasiwasi wa viongozi wa Kiyahudi kama walimu na ujinga wao juu ya kile Agano la Kale kilichofundisha kuhusu hali halisi ya Masihi, na kuwatenganisha zaidi na Yeye.

Yesu Kristo, mwana pekee wa Mungu na njia pekee ya wokovu kwa ulimwengu (Matendo 4:12), pia ni mwana wa Daudi, kwa maana ya kimwili na ya kiroho.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Ina maana gani kwamba Yesu ni mwana wa Daudi?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries