settings icon
share icon
Swali

Je! Yesu hakuwa na dhambi?

Jibu


Ndio, Yesu hakuwa na dhambi, na ni kwa sababu Yesu hakuwa na dhambi kwamba tuna tumaini la milele mbinguni. Ikiwa Yesu hakuwa na dhambi, hakutakuwa na dhabihu kwa ajili ya dhambi. Uasi wa Adamu na Hawa kwa Mungu katika Bustani la Edeni ilileta dhambi katika ulimwengu huu (Mwanzo 3: 6). Kwa dhambi yao ilikuja kifo, kama Mungu alivyoonya (Mwanzo 2:17). Matokeo yake, wanadamu sasa wanazaliwa na tabia ya dhambi (Warumi 5: 12-19), na iko pamoja nasi kutoka wakati tunapozaliwa (Zaburi 51: 5). Biblia inaonyesha wazi, hata hivyo, kwamba Yesu Kristo, ingawa alijaribiwa kwa kila namna kama sisi (Waebrania 4:15), hakufanya dhambi (2 Wakorintho 5:21, 1 Yohana 3: 5). Mtume Petro alisema waziwazi: "Yeye hakutenda dhambi, wala neno la udanganyifu halikusikika mdomoni mwake" (1 Petro 2:22). Hakika, kama Yesu Kristo ni Mungu, hana uwezo wa kutenda dhambi.

Kwa kuongezea kuweka kizuizi kati yetu na Muumba wetu, asili yetu ya urithi ya dhambi ilitueka sisi wote kwa kifo cha kimwil cha milele kwa sababu "mshahara wa dhambi ni mauti" (Waroma 6:23). Sasa, ili kuunganishwa na Mungu kulihitaji kuwa na msamaha, na "bila kumwaga damu hakuna msamaha" (Waebrania 9:22). Baada ya Adamu na Hawa kutenda dhambi, Mungu aliwavisha na "nguo za ngozi" (Mwanzo 3:21) kwa kumwaga damu ya mnyama. Hata hivyo, dhabihu nyingi za mifugo zifuatazo, ingawa zinaonyesha kikamilifu kwamba dhambi inahitaji kifo, ilitoa tu kifuniko cha dhambi tu, kwa kuwa damu ya wanyama hao haikuweza kuondoa kabisa dhambi (Waebrania 10: 4, 11).

Dhabihu za Agano la Kale zilikuwa kivuli cha kamili, "mara moja kwa wote" sadaka ya Yesu Kristo (Waebrania 7:27; 10:10). Njia pekee ambayo tunaweza kuidhinishwa na Mungu mtakatifu na mkamilifu ilikuwa kwa sadaka takatifu na kamilifu ambayo hatungalikuwa nayo ikiwa Yesu Kristo hakuwa na dhambi. Kama Petro alivyosema, "Maana mnajua kwamba nyinyi mlikombolewa katika mwenendo wenu usiofaa ambao mliuopokea kutoka kwa wazee wenu,lakini hamkukombolewa kwa vitu vyenye kuharibika: kwa fedha na dhahabu, bali kwa damu ya thamaniya Kristo, ambaye alikuwa kama mwanakondoo asiye na dosari wala doa"(1 Petro 1: 18-19). Kwa kweli, ilikuwa damu isiyo na dhambi ya Kristo peke yake ambayo iliweza kuleta amani kati ya Mungu na wanadamu (Wakolosai 1:20). Na kwa upatanisho huu, tunaweza kuwa "watakatifu kwa macho ya Mungu, bila ya kosa na bila ya mashtaka" (Wakolosai 1:22).

Kifo cha Kristo kisicho na dhambi msalabani huko Kalvari kililipa adhabu kamili kwa ajili ya dhambi ya wote wanaomwamini. Hivyo, kile kilichopotea wakati wa kuanguka kilitolewa huko msalabani. Kama vile dhambi iliingia ulimwenguni kwa njia ya mtu mmoja (Adamu), Mungu alikuwa na uwezo wa kukomboa ulimwengu kwa njia ya mtu mmoja-Yesu Kristo asiye na dhambi.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je! Yesu hakuwa na dhambi?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries