settings icon
share icon
Swali

Je! Yesu yuaja hivi Karibuni?

Jibu


Hivi karibuni ni neno lenye uhusiano. Ikiwa unapika chakula, hivi punde itamaanisha kuwa chakula kitakuwa tayari takribani baada ya dakika tano. Ikiwa wangojea kuzaliwa kwa mtoto, hivi punde itakuwa wakati wowote hapa kati kati hadi miezi tisa. Kwa hivyo tunauliza, “Je! anakuja hivi karibuni?” lazima tufafanue maana ya hivi punde.

Yesu mwenyewe alisema anakuja hivi karibuni: “Yeye anayeshuhudia mambo haya asema, “Hakika, naja upesi” (Ufunuo 22:20). Na tena Yohana anaongeza maneno haya: “Amen. Njoo, Bwana Yesu.” Ufunuo wa Yohana uliandikwa takribani miaka elfu mbili iliyopita, ambayo inawafanya watu wengi kustaajabu Yesu alimaanisha nini kwa kusema “hivi punde.”

Neno la Kiyunani tachu, ambalo limetafsiriwa “hivi karibuni” or “kwa upesi,” lamaanisha “bila kukawia.” Halimaanishi “papo hapo.” Neno hilo hilo limetumika mahali kwingine katika Agano Jipya, lakini la kufurahisha, mara nyingi limetumiwa na Yesu katika kitabu cha Ufunuo (Ufunuo 2:16; 3:11; 11:14; 22:7, 12 na 20). Maana yake inaonekana kuwa ya lile tukio ambalo limekwisha anzishwa ambalo linakiribisha ujio wake bila kukawia. Kila kitu kinasonga kadri na mpangilio wa Mungu.

Petro anatuhakikishia kwamba Mungu hafuati nyayo za matukio ya unabii. Wakati wa Mungu ni mkamilifu: “Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake, kama watu wengine wanavyokudhani kukawia. Badala yake, yeye anawavumilia ninyi, maana hataki mtu yeyote aangamie, bali kila mtu afikilie toba” (2 Petro 3:9). Kwa kuzingatia hili, tunaweza kuelewa kwamba ujio wa Yesu uu “karibuni” ni kwamba, mpango wa Mungu unaendelelea na umekawia tu ili kuwaruhusu wateule wote waokoke (Warumi 8:29; Waefeso 1:5)-kuharishwa kunaostahili.

Biblia infundisha kwamba ujio wa Yesu kwa kinisa Lake uu karibu sana, ambayo inamaana kwamba unyakuzi unaweza fanyika wakati wowote. Mtume anaonekana kuamini kuwa Yesu angerudi wakati wao. Mara nyingi walisungumzia “siku za mwisho” (1 Petro 1:20; 1 Wakorintho 10:11; Waebrania 1:2), na kuwasihi waumini kuwa tayari. Inaonekana kuwa Yesu pia alikusudia sisi pia tuamini kuwa ujio wake uu karibu, kwa sababu kira mara aliwahimiza wafuasi Wake “kuwa tayari” (Luka 12:40; 21:34-36; Marko 13:33). Kwa sababu hamna yeyote amejua au kutabiri wakati kamili wa ujio Wake (ona Mathayo 24:36), lazima tuishi tukitarajia kwamba anaweza rudi wakati wowote. Hiyo inaonekana kuwa nia hasa ya Yesu ya kutokuwa na wakati mwafaka wa kurudi. Anataka kila kizazi kiishi na ufahamu wa mawazo kwamba Bwana anaweza kutustukia kwa ghafula na tutatoa hesabu ya jinsi atakavyo tupata tuko (Luka 12:38). Ili tujibu swali, “Je! Yesu yuaja hivi karibuni?” tunasema, “naam, atakuja bila kukawia.”

English

Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je! Yesu yuaja hivi Karibuni?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries