settings icon
share icon
Swali

Kutafakari Kikristo ni nini?

Jibu


Zaburi 19:14 inasema, "Mei maneno ya kinywa changu na mawazo ya moyo wangu yapate kibali mbele zako, Ee Bwana, Mwamba wangu, na mkombozi wangu" Basi, huko ndiko kutafakari, na ni jinsi gani Wakristo wanastahili kutafakari? Kwa bahati mbaya, neno "kutafakari" linaweza kubeba maana kitu ambacho ni fumbo. Kwa mwingine, kutafakari ni kusafisha akili wakati umekaa katika nafasi isiyo ya kawaida. Kwa wengine, kutafakari ni kuwasiliana na ulimwengu wa roho unaotusunguka. Dhana kama hizi dhahiri hazibainishi kutafakari ya Kikristo.

Kutafakari kikristo hakuna uhusiano wowote na mazoea ya siri ya Mashariki kama msingi wao. Mazoea ni pamoja na kutafakari yaliyopita, na aina nyingi za kile kinachoitwa sala tafakari. Huu una msingi Nguzo hatari kwamba tunahitaji "kusikia sauti ya Mungu," si kupitia kwa neno lake, lakini kwa njia ya ufunuo binafsi kwa njia ya kutafakari. Baadhi ya makanisa simejaa watu ambao wanadhani kuwa wasikia "neno kutoka kwa Bwana," mara nyingi wanatofautiana wao weneyewe na kwa hiyo kusababisha mgawanyiko ndani mwili wa Kristo. Wakristo hawapaswi kuliacha neno la Mungu, ambalo ni "pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaony awatu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kuwadibisha katika haki; ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema" ( 2 Timotheo 3:16 - 17). Kama Biblia inatosha kabisa kutuandaa kwa kila kazi njema, ni jinsi gani tunafikiri tunahitaji mafumbo au zaidi yake?

Kutafakari Kikristo kunapaswa kuwa katika neno la Mungu na chenye lifunua kuhusu Yeye. Daudi alipata hili kuwa hivyo, na anaelezea mtu ambaye ana "heri" kama mtu ambaye "Bali sheria ya Bwana ndiyo impendezayo, na sheria yake huitafakari mchana na usiku" (Zaburi 1:2). Kutafakari kwa kweli Kikristo ni mchakato wa mawazo ambapo sisi hujitoa kwa kujifunza neno, kuomba juu yake na kumwomba Mungu kutupa ufahamu na Roho, ambaye ameahidi kutuongoza sisi "katika kweli" (Yohana 16:13). Kisha sisi huweka ukweli huu katika mazoezi, kujitolea kwa maandiko kama utawala wa wa maisha na kuweka katika mazoezi tunavyo timiza majukumu yeut ya kila siku. Hii husababisha ukuaji wa kiroho na ukomavu katika mambo ya Mungu kama tunapofundishwa na Roho wake Mtakatifu.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Kutafakari Kikristo ni nini?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries