settings icon
share icon
Swali

Je, napaswa kujibu namna gani kwa upendo usiostahiliwa?

Jibu


Upendo bila malipo ni mada ya riwaya mingi, vipindi vya televisheni, na filamu, na watu wengi kupitia kipindi kimoja au mbili ya upendo bila malipo kwa maisha yao. Upendo bila malipo unaeza anza kama mapenzi ya kitoto katika miaka changa, lakini katika utu uzima, hizo hisia zinaweza kuwa na nguvu kwa wingi, kusababisha kufujika kwa uchumba, mahusiano, na huzuni. Wakristo hawajaepuka kupitia upendo usiostahiliwa, hivyo ni jinsi gani tunaweza jibu wakati unatokea?

Kwanza kabisa, tunahitaji kufahamu kwamba upendo bila malipo ni kupoteza. Tunahitaji kukubali ukweli kwamba, wakati tunapenda mtu ambaye hatupendi, tunahuzunika. Huzuni ni mhemuko wa nguvu sana, lakini ni sehemu muhimu ya kuponya moyo uliojeruhiwa. Kuna hasara ambazo huleta uchungu mkubwa wa kibinafsi, kukuzwa na ukweli kwamba mara nyingi hatupendi kuziongelea. Wale ambao wanahuzunika juu ya kifo cha mpendwa wao mara kwa mara wamezungukwa na kusaidiwa na marafiki na familia wenye huruma. Wanaweza jadili hasara zao wasiwasi na kupata huruma. Lakini wakati hasara yetu ni binafsi, kama vile kutoka kwa mimba, kushindwa kitabia, au upendo bila malipo, mara nyingi tunahuzunika pekee.

Kuhuzunikia upendo usiostahiliwa ni sawa na kuhuzunika kupoteza mtoto ambaye hajazaliwa. Tuna huzuni kwa sababu ya kile kilichokuwa. Tunalazimika kuacha ndoto nzuri ambayo kamwe haiwezi timia. Tunahuzunika pia juu ya hisia ya kukataliwa na ya kujihisi hatustahili ambayo inakuja na upendo bila malipo. Inachukua muda kuponya moyo uliovunjika, kama vile inavyochukua muda kuponya maumivu ya kimwili. Lakini hatimaye tutakuwa na amani na ukweli kwamba vitu kamwe havitakuwa jinsi tulivyotaka viwe.

Mara tu huzuni ya mwanzo imepungua, tunaweza endelea kuponya kwa kugeuza uchungu wetu kwa shukrani. Kuna sababu upendo tulikuwa nayo kwa mtu hahukurudishwa, kwa hivyo tunaweza mshukuru Bwana kwa kutukinga kutoka muungano usiostahili. Kwa uwazi, mahusiano hayakupaswa kuwa, hivyo tunaweza geuza moyo mzito hadi moyo wa shukrani kwa kutambua kwamba tumezuhiliwa kufanya makosa kubwa. Tunapaswa kutoa shukrani kwa kila hali, sio kwa sababu Mungu anahitaji shukrani lakini ni kwa sababu tunahitajika kuzitoa (1 Wathesalonike 5:18). Kutoa shukrani, hata wakati tunaumia, inaweka mahusiano yetu na Mungu sawa. Inatukumbusha kwamba Yeye ako katika udhibiti na ana mpango (ona Isaya 46:9-11).

Lazima tuwe macho kwamba tusigeuze upendo bila malipo kuwa kauli kuhusu thamani yetu wenyewe. Hisia za kukataliwa ni kawaida, lakini hatupaswi kuzizingatia sana. Wakati mwingine huzuni na masikitiko ni afya na ni ya muda tu, Shetani angependa tusijithamini. Anapendekeza kwetu kwamba, kwa vile huyo mtu hakutupenda, kamwe hakuna atakayetupenda; kwa kweli hatupendeki. Na Shetani ataonyesha “ushahidi” mwingi wa kutostahili kwetu. Tunahitaji kufahamu mbinu zake na kukataa kimakusudi uwongo zake (2 Wakorintho 10:5). Tunaweza badilisha uwongo wa Shetani na ukweli wa Mungu. Inaweza saidia kuchapisha ukweli kama huu na kuiweka katika kumbukumbu:

• Ninapendwa na Mungu kwamba alitoa Mwanawe kwa ajili yangu (Yohana 3:16).
• Ni Mungu anafanya kazi ndani yangu, na kuniunda jinsi anavyotaka nikuwe (Wafilipi 2:13).
• Kila kitu (hata hiki) kitafanya kazi kwa pamoja kwa uzuri ikiwa nitapenda Mungu na sababu Yake katika maisha yangu (Warumi 8:28).
• Mungu yupo karibu na mimi wakati ninaumwa na hata sasa anaponya moyo wangu (Zaburi 34:18).
• Mungu atatimiza mahitaji yangu yote, hata kwa mapenzi, kwa hivyo ninamwaminia (Wafilipi 4:19).

Muhimu, tunahitaji kuendelea. Upendo bila malipo unaacha jiraha ambalo litakaa kwa muda mrefu, lakini hatuhitaji kuirejelea mara kwa mara katika mawazo yetu. Tunaipigia kwaheri na kisha tunaweka macho yetu kwa yale Mungu ametuwekea katika wakati ujao. Kutakuwa na mapenzi mengine, fursa nyingine, watu wengine ambao hatujui kitu chochote kuwahusu kwa sasa. Kutakuwa na mifurukuta na mipindo, mshangao na furaha, na tunahitaji kutayarisha mioyo yetu kuyapokea yote. Wafilipi 3:13-14 inaweza kuwa maneno ya kurudiwa rudiwa kwa wale wanapona kutoka kwa upendo usiostahili: “Ninasahau mambo yale yaliyopita, nakaza mwendo kufikia yale yaliyo mbele. Nakaza mwendo nifikie ile alama ya ushindi iliyowekwa ili nipate tuzo ya mwito mkuu wa Mungu ambao nimeitiwa huko juu mbinguni katika Kristo Yesu.”

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je, napaswa kujibu namna gani kwa upendo usiostahiliwa?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries