settings icon
share icon
Swali

Biblia inasema nini kuhusu unywaji pombe wa watoto wadogo?

Jibu


Biblia kamwe haitaji unywaji pombe wa watoto walio chini ya umri mdogo. Katika nyakati za Biblia, divai ilikuwa kinywaji bora, kwa kiasi fulani kutokana na ukosefu wa maji katika jangwa la Palestina. Kila mtu alikunywa divai, na hapakuwa na katazo la kitamaduni au la kibiblia dhidi yake. Biblia inakataza dhidi ya ulevi, si dhidi ya kukunywa. Kwa hivyo, hakujatajwa unywaji pombe wa watoto katika Biblia.

Maandiko hayamkatazi Mkristo kunywa pombe, divai, au kinywaji chochote chenye kileo. Kwa kweli, kunywa mara nyingi kunaonyeshwa kwa maneno mazuri katika Maandiko. “Nenda, kula chakula chako kwa furaha, unywe divai yako kwa moyo wa shangwe, kwa maana sasa Mungu anakubali unachofanya” (Mhubiri 9:7). Zaburi 104: 14-15 inasema kwamba Mungu humpa divai “ya kuufurahisha moyo wa mwanadamu.” Amosi 9:14 inazungumzia kunywa divai kutoka kwa shamba lako la mizabibu kama ishara ya baraka za Mungu. Hata hivyo, Biblia inashutumu hasa ulevi na madhara yake (Mithali 23:29-35). Wakristo pia wameamrishwa kutoruhusu chochote kuwatawala (1 Wakorintho 6:12; 2 Petro 2:19). Maandiko yanamkataza zaidi Mkristo kufanya jambo lolote ambalo linaweza kuaudhi Wakristo wengine au kuwatia moyo kutenda dhambi dhidi ya dhamiri zao (1 Wakorintho 8:9-13).

Hata hivyo, ikiwa maneno “unywaji pombe kwa watoto wadogo” yanarejelea kuvunja sheria kwa kuwanywesha watoto pombe au kunywesha watoto wadogo, basi ni wazi kuwa ni makosa na Biblia inashutumu. Warumi 13:1-7 inaweka wazi kwamba Wakristo hawapaswi kuasi sheria za nchi bali tanapaswa kutii serikali ambayo Munug ameweka juu yetu. Mungu aliumba serikali ili kuweka utaratibu, kuadhibu uovu, na kuendeleza haki (Mwanzo 9:6; 1 Wakorintho 14:33; Warumi 12:8). Tunapaswa kutii serikali katika kila jambo-kulipa ushuru, kutii kanuni na sheria, na kuonyesha heshima. Wakati pekee ambao tunaruhusiwa kutotii mamlaka iliyo juu yetu ni wakati mamlaka hizo zinapotutaka tumuasi Mungu. Ikiwa hatuheshimu sheria za serikali yetu, hatimaye tunaonyesha kutoheshimu Mungu, kwa maana Yeye ndiye aliyeiweka serikali hiyo juu yetu. Kwa hiyo, yeyote anayevunja sheria kwa kununua au kusambaza pombe kwa watoto wadogo ana hatia ya uvunjaji wa sheria na anakosa kumtii Mungu. Watoto wanaokunywa pombe kinyume cha sheria, kupitia unywaji wa watoto wado, wana hatia vivyo hivyo.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Biblia inasema nini kuhusu unywaji pombe wa watoto wadogo?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries