settings icon
share icon
Swali

Je! Ni kwa nini tunahitaji kumwomba Mungu atuokoe kutoka uovuni?

Jibu


Ombi kwamba Mungu “tukomboe kutoka kwa yule mwovu” ni kutoka Sala ya Bwana, iliyorekodiwa katika Mathayo 6:13. Sala ya Bwana pia imeandikwa katika Luka 11:2-4 lakini haijumuishi ombi hilo la mwisho. Katika Kigiriki, neno hilo linatafsiriwa kihalisi kuwa “Mwovu.” Kwa kuwa neno hilo ni bayana, wachanganuzi wengi wanaamini kwamba “uovu” unaorejelewa umefanywa kuonekana kana kwamba ni mtu, yaani, inamrejelea Shetani.

“Utuokoe na uovu” inaunganishwa na ombi lililo mbele yake, “utuokoe kutoka kwa yule mwovu” (Mathayo 6:13). Ombi hili pia lina ugumu fulani. Neno linalotafsiriwa “majaribu” linaweza pia kutafsiriwa “jaribio gumu” na haimaanishi jaribu la kufanya dhambi.

Hatimaye, maana ya “Utukomboe kutoka kwa mwovu” haipatikani katika mgawanyiko wa maneno binafsi lakini katika mwelekeo wa jumla wa kifungu. Hatimaye Shetani ndiye anayesbabisha maovu yote, kwa hivyo tofauti kidogo iwapo tutaomba kukombolewa kutoka kwa uovu kwa ujumla (dhambi) au kutoka kwa yule mwovu, hasa, kwa sababu mambo hayo mawili yanahusiana. Vivyo hivyo, kila wakati wa “majaribu magumu” ni fursa ya kumwamini Mungu au kuafikiana na kusalimu amri ya majaribu ya dhambi na hivyo kwa kiasi fulani kuwa chini ya udhibiti wa dhambi na shetani. Katika Sala ya Bwana, tunaagizwa kusali kwamba Mungu atulinde kutokana na hali ambazo zinaweza kutujaribu kufanya dhambi. Ni ombi kwamba dhambi kamwe isipate nafsi katika maisha yetu.

Yesu aliwafundisha wafuasi wake kusali, “Utuokoe na yule mwovu,” kwa sababu hatuwezi kumpinga shetani kwa nguvu zetu wenyewe. Muumini katika Kristo amekombolewa kutoka kwa adhabu ya dhambi (Warumi 8:1), lakini bado tuko katika vita vya kila siku dhidi ya dhambi na shetani. Tunahitaji kumtegemea Roho Mtakatifu ili atusaidie kupinga majaribu na kushinda dhambi katika maisha yetu. Kuomba “utukomboe na uovu” ni kutambua uwezo wetu wa kiwango na njia ya kumwomba Mungu aingilie kati na kutusaidia. Ingawa tunaweza kusali ili kupata msaada wa kushinda majaribu na dhambi, tunaweza pia kusali kwamba tusiwe katika hali ambayo tunakabiliana na majaribu makali. Mtu ambaye anapambana na unywaji wa pombe anapaswa kuepuka maeneo ambayo pombe inauzwa, lakini pia anapaswa kusali ili asipate mialiko yoyote isiyotarajiwa ya kunywa pombe katika shughuli yake ya siku. Mtu ambaye anapigana kushinda tamaa kwa kawaida anapaswa kuepuka maeneo na shughuli fulani, lakini pia anaweza kusali kwamba hali zilizo zaidi ya uwezo wake zisijitokeze kwake.

Sala kwamba Mungu atukomboe na uovu ina ulinganifu katika amri na ahadi ya Yakobo 4:7: “Mpingeni ibilisi, naye atawakimbia.” Hii inatanguliwa na “jinyenyekezeni kwa Mungu.” Ikiwa tungekabiliana na shetani kwa uwezo wetu wenyewe, tungelemewa. Tunaweza tu kuyapinga majaribu, kuepuka dhambi, na kumshinda mwovu kwa kutegemea nguvu za Mungu. Sawa na vile tunavyohitaji kuuliza “mkate wa kila siku” kwa ajili ya mahitaji yetu ya kimwili, tunapaswa kuuliza “kukombolewa kila siku” kwa ajili ya mahitaji yetu ya kiroho.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je! Ni kwa nini tunahitaji kumwomba Mungu atuokoe kutoka uovuni?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries