settings icon
share icon
Swali

Tafakari ya kiroho ni nini?

Jibu


Taamuli ya kiroho ni hatari sana kwa mtu yeyote ambaye anataka kuishi kibiblia, maisha yanayoongozwa na Mungu. Kwa kawaida zinazohusiana na fugufugu ya makanisa yanayoibuka, ambayo yamejawa na mafundisho ya uongo. Pia inatumiwa na makundi mbalimbali ambayo yana kuhusiana kidogo na Ukristo.

Katika mazoezi, tafakari ya kiroho kimsingi inazingatia juu ya kutafakari, ingawa si kutafakari kwa mtazamo wa kibiblia. Vifungu kama vile Yoshua 1:8 kweli inatuhimiza kutafakari: "Kitabu hiki cha torati kisiondoke kinywani mwako, bali yatafakari maneno yake mchana na usiku, upate kuangalia kutenda sawa sawa na maneno yote yaliyoandikwa humo; maan ndipo utakpoifanikisha njia yako, kasha ndipo utakapositawi sana" Gundua lengo la kutafakari lazima liwe kwa neno la Mungu. Tafakari inayoongozwa kiroho hailengi katika kitu chochote hasa. Anaye jaribu anahimizwa kusafisha kabisa akili yake, ili"iwe." Kwa kisio, hii husaidia mmoja kwa kufungua uzoefu mkubwa wa kiroho. Hata hivyo, sisi tunahimizwa katika maandiko kugeuza nia zetu ziwe kama ile ya Kristo, kuwa na akili zake. Kuondoa akili zetu ni kinyume na tendo kama hilo, mabadiliko ya fahamu.

Tafakari ya kiroho pia hutia moyo mwanaharakati za uzoefu wa fumbo na Mungu. Kipagani ni imani kwamba elimu ya Mungu, ukweli wa kiroho, na ukweli wa mwisho inaweza kupata kupitia uzoefu kutawaliwa. Huu msisitizo wa elimu ya uzoefu inasababisha ukosefu wa uhakika wa mamlaka ya Maandiko. Tunamjua Mungu kulingana na neno lake. "Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu na ni muhimu kwa ajili ya kufundisha, kukemea, kuwaongoza na kuwafundisha katika haki, ili mtu wa Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki; ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema" (2 Timotheo 3:16-17). Neno la Mungu li kamili. Hakuna sababu ya kuamini kwamba Mungu anaongeza mafundisho ya ziada au ukweli wa neno lake kwa njia ya uzoefu wa fumbo. Badala yake, imani yetu na chenye tunakijua kuhusu Mungu ni kwa kuzingatia ukweli.

Tovuti ya Kituo cha Taamuli kiroho yafupisha vizuri sana: "Tunatoka katika aina nyingi ya asili ya kidunia na ya kidini na sisi hutafuta kuimarisha safari yetu kwa njia ya mazoezi ya kiroho na utafiti wa mila kubwa za kiroho za dunia. Tunatamani kumkaribia Roho wa upendo ambaye ameenea kwa viumbe vyote na ambaye huwahamasisha huruma yetu kwa viumbe wote." Kikiblia hakuna kabisa malengo kama hayo. Kuisoma duniani "mapokeo ya kiroho," ni zoezi lisilokuwa kwa sababu mila yoyote ya kiroho mbali na ile ambayo inamwinua Kristo ni ya uongo. Njia pekee ya kumkaribia Mungu ni kupitia kwa njia ameiteua, Yesu Kristo na neno.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Tafakari ya kiroho ni nini?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries