settings icon
share icon
Swali

Shuhudio za Watetezi ni nini?

Jibu


Shuhudio za watetezi ni mtindo wa Wakristo watetezi ambayo inasisitiza ushahidi chanya ambao unapendelea ukweli wa Ukristo. Sehemu ambayo ni ya kipekee ya ushahidi wa watetezi ni hatua moja ya kuanzisha ukanamungu wa Kikristo. Washuhudiaji watatumia ushahidi na hoja kutoka maeneo kadhaa ikiwa ni pamoja na akiolojia, unabii wa kimasihi uliotimia, na hasa kutokana na miujiza.

Tafauti na utetezi wa wanazuoni wa elimu na lugha, mtetezi wa uthibitisho anaamini kwamba matukio ya miujiza ni uthibitisho wa kuwako kwa Mungu.kwa njia hii, mtetezi wa ushahidi haamini kwamba hoja za kifalsafa na za kisanyansi za kuwepo kwa Mungu lazima kimantiki zitangulie hoja kutoka kwa miujiza ili kuonyeisha Ukrito wa kibiblia. Hata hiyvo mtetezi wa ushuhuda hapingi matumizi ya theolojia ya asili kusaidia katika kuthibitisha kuwako kwa Mungu. Hoja hizi ni silaha muhimu katika zana za ushahidi kwa kuwa zinasaidia kutetea kesi ya Ukristo kwa kutoa uthibitisho zaidi kwamba Mungu yupo na ameumba na kuunda ulimwengu wetu. Wana uthibitisho hawaamini kwamba hoja kama hizo lazima ziwasilishwe kable ya kuendelea na ushahidi kutoka kwa miujiza. Kwa njia hii, mtetezi wa ushahidi anaweza kubishana juu ya ukanamungu na Ukristo ukanamungu kwa wakati mmoja bila kuanzisha kuwepo kwa Mungu kwanza. Mtazamo kama huo unaweza kuwa wa manufaa katika uinjilisti wa kibinafsi ambapo wakati unaweza kuwa mdogo.

Watetezi wa uthibitisho hutilia mkazo ushahidi kutoka kwa miujiza, haswa ufufuo wa mwili wa Yesu Kristo. Wana ushahidi watarejerelea wingi wa ushahidi ili kuthibitisha ukweli wa matukio ya baada ya kifo cha Yesu aliyefufuka, pamoja na kugunduliwa kwa kaburi lake tupu. Msisitizo wa ziada mara nyingi huwekwa katika kukanusha nadharia za uasilia zinazojaribu kueleza namna ya ushahidi wa ufufuo wa Kristo. Pindi ufufuo umethibitishwa, ufahamu wa Yesu (na mitume wake) wa tukio hili ndipo unakuwa mfumo sahihi wa kufasiri ambao kupitia kwao tunaelewa umuhimu wake. Kabla ya kusulubishwa kwake, Yesu alisema kwamba ufufuo wake unaokuja utahalalisha madai Yake (Mathayo 12:38-40, 16:1-4). Mtume Paulo alitangaza kwamba ufufuo wa Kristo ulikuwa uthibitisho wa Mungu kwa uungu wa Kristo (Warumi 1:3-4). Katika kitabu cha Matendo ya Mitume, Mtume Petro alidai kwamba ufufuo wa Yesu katika mwili ulikuwa uungwaji mkono wa Mungu kwa kazi huduma ya hadharani ya Yesu (Matendo 2:23-32). Ikichukuliwa katika muktadha huu, ufufuo wa mwili unakuwa uthibitisho wa kimsingi wa madai makubwa ya Yesu kuhusu Yeye Mwenyewe na uthibitisho wa ujumbe wa wokovu wa Yesu.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Shuhudio za Watetezi ni nini?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries