settings icon
share icon
Swali

Je! Shetani anaonekanje? Na je! Mapepo wanaonekana aje?

Jibu


Maelezo ya karibu Biblia inafikia katika kuelezea vile Shetani na mapepo wanaonekana yako katika 2 Wakorintho 11:14, “hata Shetani mwenyewe hujigeuza aonekane kama malaika wa nuru.” Mistari ya kabla na baada ya mstari huu inarejelea watumishi wa Shetani wa kibinadamu ambao wanaojifanya kuwa “mitume wa Kristo” na watumishi wa uadilifu.” Kwa muktadha, maelezo haya yanarejelea walimu wa uongo. Lakini kanuni hiyo hakika inatumika kwa mapepo vile vile.

Tatizo moja-na ni kubwa mno- kwa kujaribu kuelezea jinsi Shetani na mapepo wanavyoonekana ni kwamba wao ni mizimu. Mizimu kwa ufafanusi, hawana mwili wa kawaida na ni vigumu kuwapa sehemu za mwili viumbe wasio wa kimwili. Kama viumbe wa mizimu, mapepo hawana mapua, macho, mikono, miguu, mkia au kitu chochote kile tunaweza tafuta katika kutoa maelezo. Hiyo ndio sababu moja ya ni kwa nini Biblia haielezei jinsi Shetani anavyoonekana. Hata elezo la “malaika wa nuru” katika 2 Wakorintho 11:14 hainuii kumaanisha umbo la sura yake, badala yake, inamaanisha kusisitiza asili ya udanganyifu ya Shetani. Ibilisi anataka tuamini kwamba yeye ni wa kweli na ile hali yeye ni mwongo.

Na kwa sababu sasa tumegundua kwamba Shetani ni kiumbe malaika asiye na mwili wa kawaida ambao unaoweza kuhisiwa na hisia zetu, tunaweza kukisia tu. Iwapo Shetani angeamua kuwa na sura ya kimwili-ikiwa atajidhihirisha kwetu kwa njia inayoonekana-atafanya hivyo kwa njia ya udanganyifu.

Ile taswira tamaduni ya mtandao inampendekeza Shetani kama mnyama wa kutisha aliye na pembe kama mbuzi haiko katika Biblia. Kabla ya uasi wake dhidi ya Mungu, Shetani alikua kiumbe mzuri, mwenye utukufu (ona Ezekieli 28:12-15). Jinsi Shetani “anavyoonekana” ni fumbo kwetu. Ingawa hivyo, kulingana na 2 Wakorintho 11:14, tunaweza kujua jambo moja kwa hakika: Shetani aliwadanganya watu kufikiri yeye ni malaika wa nuru. Shetani ajidhihirishe kuwe yeye ni mwovu, kiumbe muuaji itakuwa kinyume madhumuni yake. Watu wengi hawangefuata mtu wa kawaida anayejonyesha kuwa wa chuki, na wa nia mbaya. Kama vile dhambi mara nyingi inaonekana ya kuvutia-na baadaye ikafunuliwa kuwa inaelekeza mautini-vivyo hivyo Shetani atatafuta namna ya kutudanganya kwa kuonekana kuwa kitu kingine kisicho cha uovu

Hiyo ndiyo hali kuhusu mapepo. Mapepo wanaonekanaje? Hamna mtu yeyote katika Biblia aliyewahi ona pepo moja mbali na lile la maono ya Mikaya na Yohan; Mikaya hakutoa maelezo ya kimwili na vile vile Yohana akitumia mfano wa kiishara, aliandika juu ya kuonekana kama “vyura” (ona 1 Wafalme 22:21-22 na Ufunuo 16:13). Ikiwa mapepo yangechukua sura inayoonekana, wangechagua chochote ambacho kingeendeleza udanganyifu wao. Kama malaika walioanguka, mapepo ni viumbe wenye akili na wenye nguvu. Na wanaongozwa na kiumbe mwenye nguvu zaidi (Yuda 1:9), Shetani ambaye ndiye wanahiga mfano wake. Pepo wanaonekana kuwa viumbe wabaya na kwa kweli wao ni wabaya, itazuia lengo lao la undanganyifu na majaribu.

Shetani anaonekanaje? Na mapepo wanaonekanaje? Hakuna njia ya kujua kwa hakika. Ikiwa walionekana, wangechukua mwili unyago. Udanganyifu daima huvaa barakoa. Shetani na mapepo wanajaribu kujionyesha kuwa watumishi, waelekezi na “nuru” kwa watu. Lakini usikosee, “l Mwizi huja ili aibe, kuua na kuangamiza. Mimi nimekuja ili wapate uzima kisha wawe nao tele” (Yohana 10:10).

Haijalishi ikiwa Shetani angependa tufikirie nini kumhusu, tunajua ukweli: “Mwe na kiasi na kukesha, maana adui yenu ibilisi huzungukazunguka kama simba angurumaye akitafuta mtu ili apate kummeza” (1 Petro 5:8). Na tunajua mwisho wake: “Lile joka kuu likatupwa chini, yule nyoka wa zamani aitwaye ibilisi au Shetani, aupotoshaye ulimwengu wote. Akatupwa chini duniani, yeye pamoja na malaika zake” (Ufunuo 12:9).

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je! Shetani anaonekanje? Na je! Mapepo wanaonekana aje?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries