settings icon
share icon
Swali

Biblia inasema nini kuhusu ndoa wazi? Je! Biblia inazungumzia ndoa za washirika zaidi ya wawili kwa wakati mmoja?

Jibu


Ndoa wazi inafafanuliwa kuwa ni ndoa ambayo mmoja wa mwanandoa au wote wawili wanaruhusiana kufanya mapenzi na watu wengine. Aina mbili kuu za ndoa wazi ni wanandoa kukubaliana kuwa na wapenzi nje ya ndoa na wanandoa kuwa na wapenzi maalum nje ya ndoa. Wanandoa wanapokuwa na mahusiano ya nje ya ndoa yanadaiwa kuhusisha mapenzi ya kihisia na kwa upande mwingine ule wa pepeo ni wakati mahusiano ya nje ya ndoa yanahusisha tu ngono ya burudani/ya kawaida.

La! Hakuna mahali popote katika Biblia inazungumzia kuhusu mahusiano ya kingono ya jumla kwa kina, au dhana ya ndoa za jumla. Wazo kwamba mwenzi mmoja anapaswa kumruhusu mwenzi mwingine kufanya ngono na watu wengine ni geni kabisa kwa Biblia. Biblia inazungumza kuhusu ngono ndani ya ndoa kuwa safi (Waebrania 13:4). Biblia inazungumza kuhusu ngono nje ya ndoa kuwa ni uasherati na uzinzi (1 Wakorintho 6:13; 10:8; Wagalatia 5:19; Waefeso 5:3; Wakolosai 3:5; 1 Wathesalonike 4:3).

Swali huibuka kwamba wakati mwingine ikiwa uhusiano wa kimapenzi wa watu wengi unapaswa kuchukuliwa kuwa uzinzi ikiwa mwenzi mwengine ataruhusu, kuidhinisha, au hata kushiriki katika hilo. Jibu ni naam isiyo na shaka, n uzinzi! Mungu ndiye anayefafanua ndoa ni nini na uzinzi ni nini. Mungu, katika Neno lake, ametangaza ngono nje ya ndoa kuwa uzinzi (Kutoka 20:14). Mwenzi kumruhusu mwingine kufanya dhambi hakuivunji Sheria ya Mungu. Hatuna mamlaka ya kuunda ubaguzi kwa yale ambayo Mungu ametangaza kuwa ya dhambi.

Kando na matamko ya kibiblia kwamba mahusiano hayo ni dhambi, ndoa wazi haiwezi kutimiza kile ambacho Biblia inasema ndoa inapaswa kuwa. Wanandoa waliooana hawawezi kuwa “mwili mmoja” Mwanzo 2:24) ikiwa “miili” nyingine inahusika. Wenzi wa ndoa hawawezi kupendana kikamilifu ikiwa upendo huo umegawanywa kati ya watu wengine. Hakuwezi kuwa na urafiki wa kweli ikiwa kile kinachopaswa kuwa cha siri kinashirikishwa na wengine. Uhusiano wa kimapenzi wa zaidi ya watu wawili sio ndoa. Kwa maana hakuna ndoa inapaswa kuwa na shughuli za ngono nje ya ndoa.

Muungano wa kimapenzi kati ya mume na mke unakusudiwa kuwa wa kipekee na “usishirikishwe kamwe”:
“Kunywa maji kutoka kwenye kisima chako mwenyewe,
maji yanayotiririka kutoka kwenye kisima chako mwenyewe.
Je, chemchemi zako zifurike katika barabara za mji
na vijito vyako vya maji viwanjani?
Na viwe vyako mwenyewe,
kamwe visishirikishwe wageni” (Mithali 5:15-17).

Uhusiano wa kishirika kwa kweli ni tamaa tu. Hakuna upendo wowote katika hilo. Upotovu huu wa ndoa ni uthibitisho kwamba “kila mwelekeo wa mawazo ya moyo wake wakati wote ulikuwa mbaya tu,” na kwamba, bila Mungu, “kila mtu alifanya kile alichoona ni sawa machoni pake mwenyewe” (ona Mwanzo 6:5 na Waamuzi 21:25).

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Biblia inasema nini kuhusu ndoa wazi? Je! Biblia inazungumzia ndoa za washirika zaidi ya wawili kwa wakati mmoja?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries