settings icon
share icon
Swali

Je, Mungu bado anatenda miujiza?

Jibu


Watu wengi wanataka Mungu afanye miujiza ili "ajithibitishe" mwenyewe kwao. "Kama Mungu kufanya tu miujiza, ishara, au maajabu, basi nitaamini!" Wazo hili, ingawa, linahitilafiana na maandiko. Wakati Mungu alifanya maajabu na nguvu za miujiza kwa wana wa Israeli, je, alifanya hivyo kuwafanya wamtii? La, Waisraeli mara kwa mara walimuasi na kuishi kinyume na Mungu hata kama waliona miujiza yote. Wale watu ambao walimwona Mungu kwa sehemu tu katia Bahari ya Shamu baadaye wakawa na mashaka kama Mungu alikuwa na uwezo wa kushinda wenyeji wa nchi ya ahadi. Ukweli huu umeelezewa katika Luka 16:19-31. Katika hadithi, mtu katika moto wa Jehanamu anauliza Abrahamu amtume Lazaro nyuma kutoka kwa wafu ili kuwaonya ndugu zake. Abrahamu alimpasa habari mtu huyo, "Kama hawatamsikiza Musa na Manabii, wao wataamini hata kama mtu angefufuka kutoka wafu" (Luka 16:31).

Yesu alifanya miujiza mingi sana, lakini idadi kubwa ya watu hawakumwamini. Kama Mungu alifanya miujiza hii leo vile alivyofanya katika siku za nyuma , matokeo yatakuwa tu vile vile. Watu watastaajabika na waamini katika Mungu kwa muda mfupi. Imani itakuwa hafifu na kutoweka wakati kitu kisizotarajiwa au cha kutisha kikitokea. Imani amabyo msingi wake u juu ya miujiza ni imani isiyokomaa. Mungu alifanya miujiza kuu wakati wote kwa kuja duniani kama Mwanadamu Yesu Kristo akafa msalabani kwa ajili ya dhambi zetu (Warumi 5:8 ) ili kwamba tuweze kuokolewa (Yohana 3:16). Mungu bado anafanya miujiza, miujiza mingi huwa haitambuliwi au kukataliwa. Hata hivyo, hatuna haja ya miujiza zaidi. Tunachohitaji ni kuamini katika muujiza wa wokovu kwa njia ya imani katika Yesu Kristo.

Madhumuni ya miujiza ilikuwa kuthibitisha mtendaji wa miujiza. Matendo 2:22 inasema, "Enyi Wana wa Israeli, sikiliza hili. Yesu wa Nazareti alikuwa mtu wa kibali cha Mungu kwenu kwa miujiza , maajabu na ishara , ambayo Mungu aliifanya kati yenu kwa njia yake, kama ninyi wenyewe mnavyojua " vile vile hayo yamesemwa kuhusu mitume wake: "mambo ambayo ni alama ya mitume ni ishara, maajabu na miujiza yalifanyika kati yenu kwa uvumilivu mkubwa " (2 Wakorintho 12:12). Ikizungumzia juu ya injili, Waebrania 2:4 inasema, " Mungu pia alitoa ushahidi wake kwa ishara, maajabu na miujiza mbalimbali, na vipawa vya Roho Mtakatifu kusambazwa kulingana na mapenzi yake. " Kwa sasa tuna ukweli wa Yesu kumbukumbu katika maandiko. Kwa sasa tuna maandiko ya mitume kumbukumbu katika maandiko. Yesu na Mitume wake, kama vile kumbukumbu katika maandiko anavyosema, ni jiwe kuu la pembeni la imani yetu (Waefeso 2:20). Kwa maana hii, hakuna tena umuhimu wa miujiza, kama ujumbe wa Yesu na mitume wake tayari uliokwisha shuhudiwa kwa usahihi katika maandiko. Ndio, Mungu bado anafanya miujiza . Wakati huo huo, tusitarajie miujiza kutokea leo kama ilivyofanyika katika nyakati za Biblia.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je, Mungu bado anatenda miujiza?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries