settings icon
share icon
Swali

Kwa nini Mungu ataenda kumfungulia Shetani baada ya utawala wa miaka 1,000?

Jibu


Ufunuo 20:7-10, "Na hiyo miaka elfu itakapokwisha, Shetani atafunguliwa, atoke kifungoni mwake; naye atatoka kuwadanganya mataifa walio katika pembe nne za nchi, Gogu na Magogu, kuwakusanya kwa vita, ambao hesabu yao ni kama mchanga wa bahari. Wakapanda juu ya upana wa nchi, wakaizingira kambi ya watakatifu, na mji huo uliopendwa. Moto ukashuka kutoka mbinguni, ukawala. N a yule Ibilisi, mwenye kuwadanganya, akatupwa katika ziwa la moto na kiberiti, alimo yule mnyama na yule nabii wa uongo. Nao watateswa mchana na usiku hata milele na milele." Katika kifungu hiki Biblia inasema uasi mmoja wa mwisho, unaochochewa na shetani, na ushindi wa wazi juu ya uasi.

Mwanzoni mwa milenia, waumini tu watakuwa hai (Ufunuo 19:17-21) – wale ambao wataishi kupitia dhiki na wale ambao watarudi pamoja na Bwana wakati wa kuja kwake kwa mara ya pili. Itakuwa wakati wa amani usio na tofauti katika historia (Isaya 2:4; Yoeli 3:10; Mika 4:3). Yesu atakaa kiti cha enzi cha Daudi, akitawala juu ya viumbe Vyake vyote. Yesu atahakikisha kwamba kila mtu ana mahitaji yote yametimizwa, na hawezi kuvumilia dhambi iliyoenea sana katika jamii ya leo (Zaburi 2:7-12, Ufunuo 2:26-29; 19:11-16). Tunaweza tu kufikiria wakati kama huo wa "mbingu katika dunia."

Inawezekana waumini ambao wataishi kupitia dhiki watakufa na watajaza watu tena dunia wakati wa ufalme wa milenia. Bila uharibifu wa dhambi kuchukua maafa yake, tunaweza kufikiria ukuaji wa idadi ya watu wakati wa milenia itakuwa kubwa sana. Wale wote ambao watazaliwa wakati wa milenia watafurahia faida na baraka za utawala wa Kristo duniani. Hata hivyo, bado watazaliwa na asili ya dhambi na watalazimika kutubu kwa uhuru na kuamini injili, kuchagulia binafsi Kristo kama Mwokozi na Bwana.

Mwishoni mwa milenia, Shetani ataachiliwa kutoka shimo la chini. Ataanza kudanganya umati mkubwa wa watu kumfuata katika uasi mmoja wa mwisho. Inaonekana kwamba dhiki zaidi itarudi nyuma katika historia, ubinadamu zaidi utachukua maisha yao ya amani kwa mzaha; wengine wanaweza hata kuwa na mashaka juu ya wema wa Mungu. Ingawa nambari ya wataasi na Shetani inasemekana kuwa "kama mchanga wa bahari" (Ufunuo 20:8), bado wanaweza kuwa wachache ikilinganishwa na idadi ambayo haitaasi.Kwa kuwa Mungu anajua shida Shetani atasababisha (tena) duniani, kwa nini anamfungua? Maandiko hayatoi jibu la uhakika. Hata hivyo, moja ya sababu inaweza kuwa kuwapa wanadamu mtihani wa mwisho. Kwa miaka 1,000, Shetani atakuwa amefungwa, na watu wengi duniani hawatapata kamwe usoefu wa majaribio ya nje kutoka ufalme wa kiroho. Mungu aliumba binadamu kwa hiari huru, na Yeye anaruhusu mapenzi hayo kupimwa. "Milenia" za baadaye-wale ambao watazaliwa wakati wa ufalme wa milenia-bado watahitaji kufanya chaguo la kumfuata Kristo au kufuata Shetani. Uachiliaji wa Mungu wa shetani utawapa furusa ya kuchagua.

Sababu nyingine inayowezekana ya Mungu kumfungulia Shetani ni kuonyesha kiwango cha asili ya dhambi katika asili ya binadamu wote (ona Yeremia 17:9). Hata baada ya miaka 1,000 ya uungu wa njozi duniani, wanadamu watakuwa na uwezo fiche wa kuasi. Sababu nyingine ya kumfungulia Shetani inaweza kuwa kutufundisha tena jinsi tunavyoweza kudanganywa kwa urahisi. Kama vile Adamu na Hawa walikataa Edeni yao kwa sababu ya maneno machache kutoka kwa mdanganyifu, ndivyo watu wengi wa wazao wa Adamu na Hawa. Sisi ni mwili na damu, na sisi tunadanganywa mara kwa mara.

Katika kumfungulia Shetani kutoka shimoni, Mungu anaweza pia kuonyesha kitu fulani juu ya asili Yake mwenyewe. Kwa miaka 1,000, neema na wema Wake utaonyeshwa daima, lakini mwishoni mwa wakati huo, atakuwa na uvumilivu wa sifuri kwa uasi. Haki yake itaanguka, na Yeye hatatoa "nafasi ya pili" kwa wale wanaochagua kuasi.

Uachiliaji wa Mungu wa Shetani mwishoni mwa milenia pia utaonyesha kwamba Shetani amekuwa na daima atakuwa adui wa binadamu. Vile Mungu ameweka upendo Wake kwetu, Shetani ana chuki maalum kwa ajili yetu. Tangu kuanguka kwa shetani (Isaya 14, Ezekieli 28) amekuwa adui wa waumini, na anaelezewa kwa kufaa kuwa mdanganyifu wa mwisho wa wanadamu (Yohana 8:44). Yote anaweza kutoa au kuahidi mwanadamu ni kifo na uharibifu (Yohana 10:10). Shetani pia ameonyeshwa katika Ufunuo 20 kuwa adui ameshindwa kweli, na hukumu yake ya mwisho ni hakika pamoja na ile ya wote wanaomfuata. Shetani ni mtu aliyeumbwa ambaye hana nguvu mbele za Mungu.

Kwa nini Mungu atamfungulia Shetani mwishoni mwa miaka 1,000? Tunaweza tu kuuliza kwa urahisi kwa nini Mungu anaruhusu Shetani uhuru wowote, hata sasa. Jibu lazima hatimaye kupatikana katika mpango huru wa Mungu wa kufunua ukamilifu wa utukufu Wake. Uhuru wa Mungu huendelea hata kwa Shetani, na Mungu anaweza kutumia chochote-hata matendo mabaya ya Shetani — kuleta mpango Wake takatifu (angalia 1 Timotheo 1:20 na 1 Wakorintho 5:5).

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Kwa nini Mungu ataenda kumfungulia Shetani baada ya utawala wa miaka 1,000?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries